Lowassa hajawahi kukataliwa na CCM!!

Lowassa hajawahi kukataliwa na CCM!!

sasa unataka ushahidi gani zaidi ya ule wa kukatwa jina lake na kamati ya maadili ya CCM na sababu za kumkata jina walizisema kwamba sifa hazitoshi
Hiyo unayoiita kamati ya Maadili inayo madaraka hayo ya kukata majina ya wagombea Urais? wewe Umekaririshwa ukaamini unataka na siye wenye IQ ndogo tufuate mkumbo!!
 
Hiyo unayoiita kamati ya Maadili inayo madaraka hayo ya kukata majina ya wagombea Urais? wewe Umekaririshwa ukaamini unataka na siye wenye IQ ndogo tufuate mkumbo!!


Ndiyo maana yake hilo ni chujio la kwanza au wewe ulifikiri kazi ni ipi?
 
dr slaa aliwaambia choo mmehamishia chumbani mkakataa, ona madhara yake sasa, 'mzee' wenu anatamba kwenye media kuwa "nimewapa chadema viti vingi vya wabunge na madiwani" swali linakuja je, ni nani mkubwa kati ya lowasa na chadema?
 
Yawezekana neno kukataliwa lina maana nyingi.

Lowassa alitamani sana kuipeperusha bendera ya CCM kwenye uchaguzi uliopita kama mgombea Urais, alitamani sana kupita hata kuingia top 5 ya candidates lakini kamati ya maadili WALIMKATAA. Pamoja na kuwepo watetezi wake wakimwimba ukumbuni lakini tayari kamati ya maadili walikuwa WAMEMKATAA. Sababu iliyofanya jina lake kukatwa ni baada ya ile kamati KULIKATAA jina hilo kwa moyo mmoja lisipite hata kama amewahi kifadhili Chama kwa namna yoyote.

Na ikumbukwe alilazimika kujiondoa bila kupenda baada ya kukatwa jina lake na kugundua kuwa viongozi wa CCM si kwamba wamelikata jina tuu bali hawampendi na WAMEMKATAA pamoja na akina Nchimbi, Sofia Simba na wengineo kumtetea.

Kiswahili rahisi ni kwamba jina la Edo LILIKATALIWA kupita hata top 5 wakati wa mjadala wa kamati ya maadili ndipo uamuzi wa kulikata ukafuata.
 
Aliminywa na JK kabla ya kuingia uwanja wa mapambano na siyo CCM,unless watuambie kama CCM ni JK!
Jina la lowassa halikufika kwenye kamati kuu,wala halmashauri kuu wala mkutano mkuu!Sasa watuambie vyombo vya maamuzi kiuteuzi chamani ni vipi?Au ni Mwenyekiti?Kama kuna mwanachama yeyote wa ccm aliyepiga kura kumchagua mtu fulani dhidi ya lowassa aje hapa aseme,kiufupi hayupo!Ni sawa na maswali ya multiple choice,umepangiwa uchague a,b,c,d,sasa utasema d ambayo haikuwepo ilikataliwa na waliofanya mtihani!
Kiufupi ccm ilichaguliwa watu na mwenyekiti,ni sawa na uchaguzi ndani ya uteuzi,mnachagua katika walioteuliwa na mfalme!
 
Lete kwanza Ushahdi lini Lowassa aliwahi kukubaliwa na CCM sio "Wanmtandao"!!

1995 Lowassa alikataliwa na Mwl Nyerere na kuridhiwa na Kamati kuu Dodoma.
2007 Lowassa alikataliwa na Bunge lenye 80% Wabunge wa CCM na JK akaridhia kukataliwa kwake.
2015 Lowassa alikataliwa tena na Kamati ya Maadili na ikaridhiwa na CCM kwa jumla.
 
Ndiyo maana yake hilo ni chujio la kwanza au wewe ulifikiri kazi ni ipi?
Kamati ya Maadili haina madaraka hayo na wala haijawahi kuwa nayo na haitakuwa nayo kwa kuwa yenyewe si sehemu (organ) ya mfumo wa kufanya maamuzi ya CCM!!
 
Ishu ilikua ni kwenda ikulu tu ,coz hats alipohojiwa BBC , kwa akishindwa itakuaje? Akadai at agenda chunga ng'ombe name si kukiimarisha chama
 
Na hapo ndipo swala la IQ linapokuja, sasa unataka ushahidi gani zaidi ya ule wa kukatwa jina lake na kamati ya maadili ya CCM na sababu za kumkata jina walizisema kwamba sifa hazitoshi halafu unasema kwamba hakukataliwa na CCM kama hakukataliwa kwa nini basi alihamia chadema baada ya CCM kutokumptisha na siyo kabla?
Nakubaliana na mleta UZI but sikubaliani na wewe, kama hoja ni tume ya Maadili kumkata Lowassa kumbuka na hawa wafuatao nao walikatwa na tume hiyo hiyo; Bilali (makamu wa raisi) Pinda (waziri mkuu) John Ramadhani (Jaji mkuu mstaafu) Kahiga (Waziri wa mambo ya nje wa sasa)
 
1995 Lowassa alikataliwa na Mwl Nyerere na kuridhiwa na Kamati kuu Dodoma.
hizo hekaya za kusema kwamba Nyerere alimkataa Lowassa hamuwezi kuzithibitisha hata chembe. Kama nyerere alikataliwa kuingia kwenye Halmashauri kuu mwaka wakati wa sakata la Tanganyika mpaka akafanya juhudi za ziada kuingia ndiyo kumkataa kwake Lowassa kujadiliwe na Kamati Kuu?
 
Nakubaliana na mleta UZI but sikubaliani na wewe, kama hoja ni tume ya Maadili kumkata Lowassa kumbuka na hawa wafuatao nao walikatwa na tume hiyo hiyo; Bilali (makamu wa raisi) Pinda (waziri mkuu) John Ramadhani (Jaji mkuu mstaafu) Kahiga (Waziri wa mambo ya nje wa sasa)



Lakini walihitajika watano tu, na majina yalikuwa zaidi ya 30 hivyo ilikuwa ni lazima zaidi ya 30 wakatwe, sasa kwanini kati ya hao 30 waliokatwa fisadi Lowasa ndiyo aonekane kaonewa?
 
Sisi tunajua kwenda ukumbini na majina matano mfukoni kuliishushia hadhi ccm
 
Kuna Propaganda zinazoenezwa na CCM na humu JF na "List of 46" wako bize kwa hilo, kwamba Lowassa alijiunga na CHADEMA baada ya kukataliwa na CCM kutokana na "Ufisadi" wake jambo ambalo si la kweli kwa asilimia mia moja. Lowassa alijiunga na CHADEMA baada ya kukataa kuwa Kondoo wa kafara kama walivyofanya kina John Malecela na Gharib Bilal walipoonewa na CCM.

Malecela na Bilal walikubali kukaa kimya hata pale taratibu za chama chao zilipopindwa ili kuwazuia kugombea Urais,lakini Lowassa alijua kuwa "Once beaten twice shy" ni heri kufa umesimama unapigania haki yako kuliko kufa umepiga magoti kwa kusubiria makombo!! Kama kuna mtu ataleta ushahidi hata wa kimazingira kwamba Lowassa aliwahi kukataliwa na CCM kutokana na "Ufisadi" wake naweza kubadili msimamo wangu kuhusu uhalali wa CHADEMA kumpokea Lowassa na kumfanya awe mgombea wake Urais!!

Kwa hiyo tuseme alikubaliwa lakini hakuwemo katika tano bora ya wagombea?

Katika wagombea waliojitokeza CCM, kuna ambao walikuwa na haki zaidi ya kupitishwa kuliko wengine? Kama walikuwepo, kulikuwa na haja gani ya kuwa na mchakato? Sasa hivi keshatangaza anagombea 2020, bila shaka kupitia CDM. Kuna haja ya CDM kuwa na mchakato wa kupata mgombea wakati huo?
 
Watu wa Lowassa iacheni ccm,mmeshahamia chadema mambo ya ccm ya nini? Inaonesha bado mnaipenda mmetoka na kinyongo
 
dr slaa aliwaambia choo mmehamishia chumbani mkakataa, ona madhara yake sasa, 'mzee' wenu anatamba kwenye media kuwa "nimewapa chadema viti vingi vya wabunge na madiwani" swali linakuja je, ni nani mkubwa kati ya lowasa na chadema?
Kuna ukweli kuw mvuto wake umechangia wingi wa wabunge upinzani
 
Kwa hiyo tuseme alikubaliwa lakini hakuwemo katika tano bora ya wagombea?

Katika wagombea waliojitokeza CCM, kuna ambao walikuwa na haki zaidi ya kupitishwa kuliko wengine? Kama walikuwepo, kulikuwa na haja gani ya kuwa na mchakato? Sasa hivi keshatangaza anagombea 2020, bila shaka kupitia CDM. Kuna haja ya CDM kuwa na mchakato wa kupata mgombea wakati huo?
Mchakato ulifuata kanuni ya chama chenyewe!?
 
Back
Top Bottom