mshikachuma
JF-Expert Member
- Dec 2, 2010
- 2,853
- 626
Heshima yenu wana jamvi!
Waswahili usema mwisho wa ubaya ni aibu, na malipo ni hapahapa duniani. Siyo siri HOT NEWS ndani ya wiki hii ilikuwa ni ccm na kujivua gamba. Baada ya vutanikuvute huko Dodoma....ikaishia kwa wah.Lowassa,Chenge na Rostam kuvuliwa nguo hadharani na kutupwa nje ya CC ya ccm kwa tuhuma za ufisadi uliokubuhu bin sugu.
Chenge :alipokuwa mwanasheria mkuu wa serikali alihusika na ufisadi kwenye Rada,na aliita mabillions yake aliyoficha nje ya nchi kuwa ni vijisenti tu! Pia huyu ndiye waziri alieongoza kwa kusaini mikataba fake kwa uroho wa fedha....haitoshi hapa majuzi aliendesha gari yake ambayo haikuwa na bima na ikaishia kuuwa wadada 2 na kesi yake ilighubikwa na mazingira ya rushwa na ikaishia yeye kuachwa huru.
Lowassa :alipokuwa waziri mkuu wa serikali alihusika na ufisadi kwenye project ya Richimond,na inasemekana ana mabiashara makubwamakubwa ndani na nje ya nchi zilizotokana na wizi wake wa kuliibia Taifa....mfano mdogo ni hizi biashara zake zinazoanzia kwa majina ya Alpha....
Rostam :huyu ndiye fisadi nguli papa a.k.a Rais wetu. Alipo kuwa mpambe wa marais wetu na huku akiwa mtunza hazina wa ccm,alihusika na ufisadi ndani ya B.O.T kwa kujichotea mabillions ya EPA na kuyaingiza kwenye kampuni ya kagoda. Pia alihusika na Richimond na sasa yupo hata kwenye Dowans.
Kama tulivyoona na kusikia jana kwenye vyombo vya habari kuwa hawa jamaa 3 hawatakiwi tena ndani ya ccm. -Sasa Je,
1. watarudisha kadi za uwanachama wa ccm na kuachana na siasa moja kwa moja?
2.Hawa wote ni wabunge - ni nini hatma ya majimbo yao na wapigakura wao?
3.Je, wanauthubutu wa kuanzisha chama chao cha siasa na wakakubalika kwa jamii?
4.Je,kuna chama chochote cha upinzani kinachoweza kuwapokea hawa jamaa?
5.Au wafilisiwe tu na kufungwa jela?
Nakaribisha mgongano wa kimawazo na kimtizamo - Ahsanteni
Waswahili usema mwisho wa ubaya ni aibu, na malipo ni hapahapa duniani. Siyo siri HOT NEWS ndani ya wiki hii ilikuwa ni ccm na kujivua gamba. Baada ya vutanikuvute huko Dodoma....ikaishia kwa wah.Lowassa,Chenge na Rostam kuvuliwa nguo hadharani na kutupwa nje ya CC ya ccm kwa tuhuma za ufisadi uliokubuhu bin sugu.
Chenge :alipokuwa mwanasheria mkuu wa serikali alihusika na ufisadi kwenye Rada,na aliita mabillions yake aliyoficha nje ya nchi kuwa ni vijisenti tu! Pia huyu ndiye waziri alieongoza kwa kusaini mikataba fake kwa uroho wa fedha....haitoshi hapa majuzi aliendesha gari yake ambayo haikuwa na bima na ikaishia kuuwa wadada 2 na kesi yake ilighubikwa na mazingira ya rushwa na ikaishia yeye kuachwa huru.
Lowassa :alipokuwa waziri mkuu wa serikali alihusika na ufisadi kwenye project ya Richimond,na inasemekana ana mabiashara makubwamakubwa ndani na nje ya nchi zilizotokana na wizi wake wa kuliibia Taifa....mfano mdogo ni hizi biashara zake zinazoanzia kwa majina ya Alpha....
Rostam :huyu ndiye fisadi nguli papa a.k.a Rais wetu. Alipo kuwa mpambe wa marais wetu na huku akiwa mtunza hazina wa ccm,alihusika na ufisadi ndani ya B.O.T kwa kujichotea mabillions ya EPA na kuyaingiza kwenye kampuni ya kagoda. Pia alihusika na Richimond na sasa yupo hata kwenye Dowans.
Kama tulivyoona na kusikia jana kwenye vyombo vya habari kuwa hawa jamaa 3 hawatakiwi tena ndani ya ccm. -Sasa Je,
1. watarudisha kadi za uwanachama wa ccm na kuachana na siasa moja kwa moja?
2.Hawa wote ni wabunge - ni nini hatma ya majimbo yao na wapigakura wao?
3.Je, wanauthubutu wa kuanzisha chama chao cha siasa na wakakubalika kwa jamii?
4.Je,kuna chama chochote cha upinzani kinachoweza kuwapokea hawa jamaa?
5.Au wafilisiwe tu na kufungwa jela?
Nakaribisha mgongano wa kimawazo na kimtizamo - Ahsanteni