Habari zilizotufikia punde zinasema madaktari wa Lowassa waliopo ujerumani wamemshauri mgonjwa wao asiendelee na shughuli hiyo ya kuwania kwani inamchosha na kufanya ugonjwa wake umtafune kwa kasi.
Madaktari wamefikia uamuzi huo baada ya kuona hali ya mgonjwa wao anayesumbuliwa na ugonjwa wa Parkinson inazidi kudorora kutokana na hekaheka za kuzunguka huko na huko kutafuta wajumbe wa kumuunga mkono kwenye harakati za kugombea urais.
Taarifa ya madaktari hao imepokelewa na mkewe Lowassa mama Regina ambaye alipokuwa nje ya nchi hivi karibuni.
Inasemekana mh. Lowassa alimtuma mkewe kwani yeye alikuwa busy kufitini mchakato wa kupata rasimu ya katiba akihofia ikipatikana rais Kikwete atapata sifa.
Hofu ya madaktari ni kuwa suala mhe la degenerative urais linampa mhe. Lowassa stress ambazo zinafanya ugonjwa wake wa Parkinson usambae kwa kasi zaidi.
Ugonjwa huo unaoshambulia na kuua mishipa ya fahamu na misuli ndio pia unaomsumbua bondia mashuhuri wa zamani mohamed Ali.
Kwa sasa mhe. Lowasa amefikia hali ambayo hawezi kuandika au kunywa supu au uji kwa kijiko kwa vile mikono yake inatikisika sana.
Madaktari wanasema akipuuza ushauri wao basi ifikapo the mwezi wa sita mwakani atashindwa hata kutembea mita mia moja.
Baadhi ya madaktari bingwa wa Tanzania niliozungumza nao kuhusu taarifa hiyo wanasema walikuwa wanafahamu ugonjwa unaomsumbua mhe. Lowassa ambao yeye anafanya siri kubwa kwa vile dalili zipo na kwamba alikuwa ananunua dawa zake katika duka la madawa lililopo oysterbay hotel, dar es salaam.
Taarifa hiyo ya madaktari bingwa wa Ujerumani imepokelewa kwa uchungu na mhe. Lowassa mwenyewe, familia yake na watu wake wa karibu.
Inaelezwa kuwa mhe Lowassa anazidi kupata vikwazo kufikia ndoto yake mahala baada ya kushambuliwa hivi karibuni na mwwnyekiti wa CCM Mwanza mhe Antony Diallo kuwa yeye ni fisadi na anasubiri kumuumbua akijitokeza rasmi kugombea urais.
Stay tune for more information.