Lowassa apigwa shinikizo kali


Hayo makundi yako yote umetaja hawafiki hata 10% ya watu wake lowasa wala wanaompenda... endeleeni kujipa moyo team wapigaji
 


Teh teh teh angekuwa amepita usinge andika hapa.....amtajua tu kuwa hii nchi ni ya watanzania na sio ccm wewe
 

Pole sana kama imekuuma...ila huyo yebo yebo hakanyagi kwa lowasa hata kwa jiki...na safari hii goli la mkono dah itakuwashida...kamera kila kona!
 
Katika hali ya kushangaza Ukawa baada ya kumtukana na kumkashifu Lowassa leo wanamuona Lowassa ni Lulu. Mh. Lowassa chondechonde hao jamaa ni Mafia ukiisha watengenezea mambo yao yakiwa safi watakuua,kwani watakuwa wameishakamata dola na ndio lengo lao kubwa kukamata dola kwa njia yoyote ile iwe ya kheri iwe ya shari. Wanasema wazi kwa sababu una umati mkubwa wa wananchi hivyo wanakuhitaji ili kuiondoa Ccm madarakani. Je what next? Its you. Wameshakuwa wanasema siku nyingi wewe ni mgonjwa hata kampeni zako ulikuwa unapigwa sindano ili uweze kufanikisha,leo kunani wanamtaka mgonjwa,fisadi na mwizi? Wanasema itabidi utubu madhambi kwa Mchungaji Msigwa na hapo Mungu na wao watakusamehe!!! Mh. Lowassa chonde chonde huna usalama huko ni bora anzisha chama au uende kwingine kuliko kwa hao jamaa,kumbuka hao ndio chanzo cha wewe kukosa kuteuliwa kwa kukuhofia na bado watakuwa na hofu ya wewe kukikamata chama wakati wao ndio waliokifikisha hapo kilipo na wameinvest pesa nyingi huko,sasa bila kuwa na mtu wao hapo wa kuzirudisha pesa walizotumia hakutakuwa na amani,solution ni kukuondoa kwa njia yoyote ile,au mkubaliane sasa mliibie taifa wote. Ole wako na chondechode hao jamaa ni Mafia Mob
 
Mbona ccm mnaumia sana lowasa kuhamia cdm??hakyamungu mmekuja kushtuka wakati ishafika jioni
 
Acheni kupotosha Lowassa hapendwi na watanzania, wapambe wake wachache ndiyo wanapenda hela zake. Angekuwa na uwezo angewezesha ushindi arusha na arumeru. Ni wajjinga na wapumbaffu tu ndiyo watadhani anapendeka na eti ana mvuto
 
Acheni kupotosha Lowassa hapendwi na watanzania, wapambe wake wachache ndiyo wanapenda hela zake. Angekuwa na uwezo angewezesha ushindi arusha na arumeru. Ni wajjinga na wapumbaffu tu ndiyo watadhani anapendeka na eti ana mvuto

Makomeo amewezesha ushindi wp? Tulia mbegu ikuingie vizuri. Tripu hii mtalijua jiji.
 
Sasa wewe inakuuma nini? Mbona hukumshauri lolote wakati alipokatwa?
Wewe utamshaurije mtu mwenye dhamira yake njema na Taifa lake? Inamaana wewe una uwezo wa kumkatia mtu malengo yake aliyoyapanga? Huna dhamira njema na Lowassa wewe! Tene unaonekana ni mfitini si mtu mwenye Uzalendo wa Taifa hili.
 
I have never been comfortable with people who surround Lowassa. I think Regina and Rostam are being very sensible.
 
Mbona ccm mnaumia sana lowasa kuhamia cdm??hakyamungu mmekuja kushtuka wakati ishafika jioni

Hamna anayeumia nyie mnasema na sisi tunasema. Nasema tena chondechonde Lowassa utauawa na hao majambazi
 

Leo ndyo mnamuona lowasa hafai? akili nyingine za kilumumba bana kama ushuzi. Lowasa ni mwamba wa siasa za Tz, ukitaja Tz basi jua unamtaja Lowasa
 
Hamna anayeumia nyie mnasema na sisi tunasema. Nasema tena chondechonde Lowassa utauawa na hao majambazi

Mkuu sema ukweli inauma sana kuona lichama lenu bibi kizee(ccm) linaenda kupasuka vipande vipande
 

Wengine 36 ni wanafiki Pia wameahidiwa vyeo mbali mbali kwenye Serikali ya Magufuli ccm walifanya magumashi makubwa Dodoma ndiyo maana wakaamua kuwapoza hao haraka ili wasipaze sauti wakaanika mapungufu ya kamati ya maadili.
 
Lowasa anafahamu siri nyingi za wanaCCM na hasa vigogo na hakuna mtu wa kuthubutu kumsema kama yeye ni fisadi akabaki salama.
 
Nilichojifunza mpaka sasa hakuna fisadi nje ya ccm ,fisadi akitoka ccm kwenda upinzani ametakasika
 

Wewe hofu yako ni kuanguka kwa CCM wala si masaibu ya Lowasa akitoka CCM. Mazingira yamebadilika mno. Lowasa akitoka CCM atakuwa Raila Odinga wa Tanzania kuiangusha CCM na kutokomea katika ramani ya siasa ya nchi. Mimi Binafsi nilimpinga Lowasa kuwa mgombea wa CCM lakini naamini Lowasa akiisaidia nchi kuiangusha CCM atakuwa na historia iliyotukuka karne na karne zijazo katika historia ya nchi yetu.
Maana adui wa nchi kwa sasa ni uongozi mbovu wa CCM na mfumo wao wa utawala unaohodhi madaraka na kutawala kama wakoloni huku umma ukinyimwa fursa ya kuhoji chochote katika utawala. Tumeona kwenye miswada ya gesi tumeona kwenye mchakato wa katiba mpya. Dhambi za CCM ni hatari sana kwa usalama wa nchi. Kama Lowasa ataunga mkono upinzani kwa mwamko wa sasa. Upinzani ukaungana wapinzani wakubwa wote ikiwepo ACT. CCM inaenda kudondoka na nchi itakuwa imepona kidonda cha CCM.
Baada ya hapo ni kuweka mfumo mpya wa utawala kama Kenya walivofanya. Tutawapita mbali wakenya chini ya miaka 15.
 

Ni kweli simpendi EL, lakini kwa hii dharau yako kwa watanzania kuwa ni vilaza hata kutunza kumbukumbu za maisha na mambo yanayo wahusu naona ni mwendelezo wa kilichopelekea jina lake kupigwa mkasi na CCM. Jifunzeni basi!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…