Lowassa aongezewe ulinzi

Lowassa aongezewe ulinzi

Mh. Laigwanan Edward Ngoyai Moringe Lowassa anastahili ulinzi wa ziada ili kumlinda na wabaya wake (CCM) kwani hawa waovu hawakawii kumfanyia kitendo cha kigaidi kama kile walichmomfanyia Horace Kolimba.Ni jambo lililo wazi kwamba CCM hawana namna nyingine ya kupambana na UKAWA zaidi ya kushiriki vitendo viovu kama hiki.

Sasa hivi Mh Lowassa ndiye adui namba moja wa CCM na waovu hawa wako tayari kufanya kila hila yoyote dhidi ya UKAWA bila kuzingatia gharama ya uovu huo.

Baada ya kumchakachua matokeo kwenye kura za maoni na kisha kushindwa kumtisha abaki CCM, kuna kila dalili CCM kufanya kitendo kiovu kwa Mh. Lowassa.

Hivyo basi, ulinzi madhubuti na makini unatakiwa kutolewa na wanaUKAWA na kila mtanzania mpenda maendeleo kwa kuwa Edo ndiye tumaini pekee kwa watanzania kujikomboa kutoka utumwa wa CCM.

Nitoe rai kwa uongozi wa UKAWA kumpa ulinzi wa ziada kiongozi huyu wa kitaifa na kimataifa ili kumlinda na kila uovu na hila za CCM. Ikiwa CCM walitupa mabomu kwenye mkutano wa siasa na kuhatarisha maisha ya raia, hawashindwi kumfanyia ugaidi kama huo kamanda Lowassa.

Lowassa ndiye mboni pekee inayowapa nuru watanzania itakayowaangazia na hatimaye kuwawezesha kutoka msitu wa giza nene (CCM) ambamo wamekuwa wakiogelea tangu enzi na enzi.

Ni jambo la kawaida kwa CCM kucheza rafu ya aina yoyote, bila kujali madhara kwa mhusika au wananchi, ilmradi tu malengo yao ya kisiasa yatimie.

Kwa kuwa tuna uzoefu wa kutosha na hawa waovu, ni bora tahadhari ichukuliwe mapema kuhakikisha kwamba hawapati nafasi ya kuendeleza uovu wao.

Tafakari, chukua hatua!

:israel:

tunamsubili alichowafanya mwakyembe na mwandosya na yeye zamu yake,

 
Tena serikali ndo inatakiwa kumlinda kwa hali na Mali. Jaribio lolote la kumdhuru Edward lowasa hakika litaleta hali ya sintofahamu kwa raia wenye hasira
 
Majizi wa ccm ni wabaya sana lakini mwaka huu wataondoka kama alivyoondoka firauni
 
alichowafanya mwandosya na mwakyembe mungu analipa mwaka huu

Mnaweweseka mpaka mna tia huruma.msumari ulipoingilia ndipo.utapotokea mtasema mengi sana lakini ccm kwisney
 
Kosa limefanyika 2009. Lilikuwa in cold storage. Limeletwa katika foreground Lowassa alipoanza vitisho vyake.kwenda on TV kuwatishia maisha watu milioni 40.

We nawe tupishe na alfu lela ulela zako.. Naskia mnagombea kawe, jiandaeni Halima hana msamaha
 
ccm mambo ambayo walitakiwa wawa fanyie watanzania mwaka2001 wana wafanyia 2014,waliyo takiwa waya fanye2015 tunge wapa nafasi wange fanya 2040 piga chini hao wawaendi na kitu muda
 
Mkuu haya yote yanasababishwa na ccm kukosa waledi.tuungane kuitoa madarakani-tumechoshwa na double standards za ccm
Mkuu hoja yangu si kuwa naikubali CCM hapana...mimi ni mwanamageuzi ninayetaka mabadiliko lakini si kwa mtindo huu....Mimi nina imani na Dk Slaa na wala si LOWASA...Hata kwa kumtazama tu machoni unaweza ukagundua kuwa huyu bwana hayupo pamoja nasi kiroho bali kimwil....huyu yeye ana malengo yake binafsi ya kuupata uraisi ,hayo malengo anayafahamu yeye na wapambe wake ambao wote wana walakini kimaadili......Pia ninaamini katika dhambi ya usaliti....Dhambi ya usaliti haiachani mbali na dhambi ya ubaguzi...kama ameweza kukisaliti chama kilichomlea na kuapa kuwa kamwe hataondoka je atashindwa kutusaliti huyu tukishampa rungu la uraisi....>????
 
Mkuu hoja yangu si kuwa naikubali CCM hapana...mimi ni mwanamageuzi ninayetaka mabadiliko lakini si kwa mtindo huu....Mimi nina imani na Dk Slaa na wala si LOWASA...Hata kwa kumtazama tu machoni unaweza ukagundua kuwa huyu bwana hayupo pamoja nasi kiroho bali kimwil....huyu yeye ana malengo yake binafsi ya kuupata uraisi ,hayo malengo anayafahamu yeye na wapambe wake ambao wote wana walakini kimaadili......Pia ninaamini katika dhambi ya usaliti....Dhambi ya usaliti haiachani mbali na dhambi ya ubaguzi...kama ameweza kukisaliti chama kilichomlea na kuapa kuwa kamwe hataondoka je atashindwa kutusaliti huyu tukishampa rungu la uraisi....>????

Kwa sasa CDM imekuwa chama kinachotaka kuingia Ikulu by any means necessary
Wasichokijua na kuelewa ni kuwa urais hauna ubia .. Lowassa akishaingia Ikulu hakuna wa kumwambia amteue nani wala nini .. sembuse kuwa keshawanunua akina Mbowe!
Tuliodhani kuwa CDM inasimamia itikadi, falsafa na dira aliyoizungumzia Dr Slaa 2010 hatukujua kuwa tulikuwa tunadanganywa tu na kutumika.

Sasa hakuna tofauti kati ya CCM na CDM hata kidogo. Tofauti ni moja - CCM iko madarakani na inahangaika isitoke, CDM bado na inahangaika kuingia madarakani. Hii ya uadilifu, utawala bora, vita dhidi ya ufisadi, kuboresha maisha ya watanzania ni uongo tu wanaotumia kufikia lengo lao kuu
 
Hili wazo muhimu sana... na uhakika Ukawa watalichukulia ktk hali ya tahadhari kubwa ulinzi wa Lowassa....

Dunia ya leo, vitendo vya kihuni ni ngumu kidogo, sbb intelijensia ya Lowassa + Ukawa, ni zaidi ya CCM yote mara 100... so am sure wako macho sana... tulianza na Mungu, tutamaliza na Mungu...

Peopleeeeee's poweeeerrr ...✌✌✌✌
 
Back
Top Bottom