Lowassa aongezewe ulinzi

Lowassa aongezewe ulinzi

Ndugu zangu, maCCM hayaamiki kabisa...ni sawa na fisi mwenye njaa anayemfuata mtu nyuma akitegemea mkono udondoke apate kitoweo. Hawa mafisi ni wa kuwaogopa zaidi ya UKOMA!

View attachment 272531
Mkuu unamaanisha kuwa yule tuliyekuwa tukimpigia debe kuwa apelekwe mahakamani kwa ufisadi na ubadhilifu wa mali za umma huku tukijinadi kuwa tuna ushahidi wa kutosha leo hii tunapigia debe apewe ulinzi na sio kupelekwa jela............
 
Sauli alikuwa Muuaji Mkuu wa Watu wa Mungu baadaye aliongoka na kuitwa Paulo.Wakristo wote wanamheshimu Paulo mpaka Leo.
Bado naendelea kushangaa tu.....kwa mifano inayotolewa kumsafisha huyo bwana...........
 
tpaul

kuna andiko kwenye bibilia linasema bila ulinzi wa BWANA yeye akeshae ni kazi bure.. naamini lowasa bi mkiristu mzuri anayejinadi na kufuata maadili ya ukiristu... naamini hataitaji sana ulinzi, ULINZI WA MUNGU unatosha
 
Last edited by a moderator:
Bado naendelea kushangaa tu.....kwa mifano inayotolewa kumsafisha huyo bwana...........

Ameongoka,Ametubu makosa yake na kuyajutia,Amekiri kwa Kinywa chake kwamba CCM SIO ILE ALIYOLELEWA NAYO.Kama Mafisadi wengi wakitubu kama Lowasa TANZANIA Yenye Maendeleo itapatikana.
 
Nashauri, kwa vile sasa ni rasmi Lowasa yuko Ukawa na Chadema zaidi basi haya yafanyike. Kwanza jukumu la ulinzi sasa liratibiwe na Red Brigade lote kwa ujumla wake, wale waliokuwa walinzi wake akiwa CCM wafanyiwe vetting upya na katika hilo Lowasa hatakiwi kuleta za kuleta kabisa, yeye sasa ni Property ya Chadema na Chadema wanapaswa kuilinda wao kwa kadiri watakavyo ona ni muhimu kama taasisi.
Pia kuna kundi lilikuwa linajiita "Friends of Lowasa" hilo kama lipo na linaendelea basi IWE NI MARUFUKU KULIINGIZA KATIKA RATIBA ZA CHAMA AU KULITAMBUA RASMI. Hilo liendelee na kazi zake lakini nje ya mfumo wa chama maana chama kisipoangalia kundi hilo linaweza kufanya madudu yake na yakakigharimu chama kwa gharama kubwa.
Jambo jingine ni kuhusu kuihusisha familia katika kampeni. Hapo ni mama Regina tuu anayepaswa kuonekana anahusishwa na kampeni za mgombea wetu, hatutaki sijui huyu MTOTO wake mara huyu sijui nani wake, hayo mambo ni ya huko ccm pekee. Hivyo kama kuna Mtoto ( yupo mmoja nasikia kule CCM kahusika sana) tafadhali akae mbali akiachie chama kiratibu mambo yake, hatukumsimamisha Lowasa kugombea Uchifu bali Urais.
 
Mimi msafi. Kwani mimi nimefunguliwa mashtaka ya money laundering? Kwani mimi nagombea urais sasa hivi. Lowassa amesema kama kuna mjinga ana ushahidi aende mahamakani,24 hrs later mtu amekwenda mahakamani.

Ushahidi Unao wa huyo mtu aliyeenda mahakamani? au unaeleza uliyoelezwa?
 
Mimi msafi. Kwani mimi nimefunguliwa mashtaka ya money laundering? Kwani mimi nagombea urais sasa hivi. Lowassa amesema kama kuna mjinga ana ushahidi aende mahamakani,24 hrs later mtu amekwenda mahakamani.

Huyo aliyekwenda mahakamani ametumwa na ccm, lengo ni kumzuia asigombee urais. Siku zote amekuwa akisema mwenye ushahidi aende mahakamani mbona hakuna aliyejitokeza?Leo kwa kuwa amehamia upinzani ndio mtu anajitokeza,huoni kuwa huo ni mchezo wa kisiasa ?Nakuuliza wewe Andrew, jakaya mrisho ni msafi ?
 
Nina imani baada ya kupitishwa rasmi kuwa mgombea wa ukawa,lazima ataongezewa ulinzi wa kutosha
 
plan wanayoweza kutumia ni labda kumuua Dr. slaa kipindi hiki ambacho kuna sintofaham dhidi yake na kusakaxia CHADEMA kuwa ndyo waliomuua. lkn kwa sasa hali imedhibitiwa.

Mkuu hata wakifanya hayo mambo watakuwa wanaogelea kwenye bahari za madhambi,hakuna panaporuhusiwa kuuwa kwa manufaa ya pande fulani,dhambi zitawatafuna hadi kiama
 
Mimi msafi. Kwani mimi nimefunguliwa mashtaka ya money laundering? Kwani mimi nagombea urais sasa hivi. Lowassa amesema kama kuna mjinga ana ushahidi aende mahamakani,24 hrs later mtu amekwenda mahakamani.

Unataka kutuaminisha nini Mheshimiwa ??? Hivi kutokugombea urais ndio usafi ?? Na kufunguliwa kesi ndio mchafu ?? Asante kwa kunielewesha
 
Kwanza nilazima ulimwe, kisha upuliziwe dawa nakupaliliwa ukisha maliza hapo tunakuvuna nakukuwekea dawa yakuku ifadhi, kisha tunakuchambuwa nakupeleka sampo tbs tayari kwa kibali cha mlaji. Sasa ikishindikana hapo lazima ukatwe tangu shambani. Kwa bwana Lowasa alikatwa tangu shambani baada yakujilikana yeye alikuwa ni uyoga wenye sumu kali katikati ya uyoga mzuri.

Mtaelewa tu kwani pembe la ng'ombe halifichiki
 
Naomba tuaminiane kama watanzania tusijenge woga na hofu katika maisha yetu. Tumtangulize Mungu kwa kila tufanyalo, na sidhani tumekuwa mashetani kiasi cha kutafuta roho za wengine kwa sababu ya kutafuta madaraka. Tuwaache wananchi wamchague wanayempenda hapo taifa litakuwa limepata tiba!

Mkuu watanzania tayari wameshaamua kuwa rais wao ajaye ni lowasa,hivyo hapa jamvini ni mbwembwe tu na vikolombwezo vya kupamba ujio wa rais lowasa
 
Kweli usiopingika lowasa ndye mkombozi wa taifa letu kwasasa kutoka kwa mafisadi ccm, anasitahili kulindwa kwa nguvu zote kwani hawa jamaa wamebanwa sio wakuamin hata kidogo...

Mkuu tunaamina red brigade, inatimiza majukumu yao na dua zetu watanzania zitatuvusha watanzania
 
Aongezewe au abadilishiwe? Mbona nimeona bado analindwa na yule Mlinzi wake wa usalama wa taifa Bwana Tendewa.

Acha uwongo mzee Tendewa ameshaondolewa. Itifaki za kiusalama zinahitaji ufahamu wa KUTUKUKA. Hata huyo mrefu yawezekana muda wowote akarudi IDARANI kufanya / kuendelea na shughuli zingine. Kitaratibu sasa inabidi CHADEMA au UKAWA na ikiwezekana sana basi hata MBOWE awe MLINZI binafsi wa Lowassa au kama akiwa busy basi TUNDU LISSU awe bodyguard wa Lowassa japo naona MLINZI binafsi ambaye atamfaa mno na sana kwa KUMLINDA ni Afande EMANUEL MAKAIDI.
 
Back
Top Bottom