Kwa sasa CDM imekuwa chama kinachotaka kuingia Ikulu by any means necessary
Wasichokijua na kuelewa ni kuwa urais hauna ubia .. Lowassa akishaingia Ikulu hakuna wa kumwambia amteue nani wala nini .. sembuse kuwa keshawanunua akina Mbowe!
Tuliodhani kuwa CDM inasimamia itikadi, falsafa na dira aliyoizungumzia Dr Slaa 2010 hatukujua kuwa tulikuwa tunadanganywa tu na kutumika.
Sasa hakuna tofauti kati ya CCM na CDM hata kidogo. Tofauti ni moja - CCM iko madarakani na inahangaika isitoke, CDM bado na inahangaika kuingia madarakani. Hii ya uadilifu, utawala bora, vita dhidi ya ufisadi, kuboresha maisha ya watanzania ni uongo tu wanaotumia kufikia lengo lao kuu