Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,154
- 162,570
Jambo ambalo wengi hawajagundua hapa ni kwamba,JK hamtaki Lowassa na hata ukipima kauli zake mbalimbali utagundua ukweli huu.Ndugu SS kwani hujui JK haaminiki na ni ndumila kuwili wa hali ya juu sana?
Tunachpaswa kutambua ni kuwa,JK hapendi kuonekana mbaya na mara nyingi hutumia walio chini yake kutekeleza yale anayoyataka.
Ndio maana hata mawaziri wake huwa hawachukulii hatua wanapobainika kufanya madudu na badala yake hungoja bunge liingilie kati kwa kutoa maazimio.
Nape hawezi ongea hayo bila kujua msimamo wa boss wake.
Nani mwenye maadili miongoni mwa vigogo wa chama cha magamba leo hii?Wote ni hovyo kuanzia EL mwenyewe na mwenyekiti wao taifa.