Tume ya Katiba
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 4,896
- 1,862
Wadau, tupate taarifa toka kwa mweshimiwa sana ndugu EL
MBUNGE wa Monduli, Edward Lowassa amekuwa akifanya mikutano ya ndani na ya hadhara jimboni humo katika kinachoonekana ni kuzima wimbi lililoibuka hivi karibuni la wanachama wa CCM kuhamia Chadema.
Tangu kujiuzulu kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) wa Mkoa wa Arusha, James ole Millya, limekuwapo wimbi la wana CCM kuhamia Chadema katika mikoa kadhaa nchini.
Mbali na Millya, wanachama wa CCM wakiwamo viongozi wenye nafasi za udiwani, walitangaza kuhamia Chadema ambayo moja ya ngome zake ni Arusha iliko na wabunge wawili; Arumeru Mashariki na Karatu.
Chadema pia ilikuwa ikiongoza Jimbo la Arusha Mjini kabla ya matokeo yake kutenguliwa na Mahakama Kuu ya Tanzania kutokana na kesi iliyofunguliwa na wanachama watatu wa CCM.
Lowassa alifanya mikutano ya ndani jana eneo la Mto wa Mbu na wa hadhara, ambako aliwaambia wananchi, kwamba pamoja na kuwa suala la kujiunga na chama chochote cha siasa ni haki ya yeyote, lakini haoni umuhimu wa wanaCCM kuhama sasa.
Mbunge huyo ambaye alikuwa Waziri Mkuu katika miaka ya kwanza ya Serikali ya Awamu ya Nne hadi alipojiuzulu Februari 2008, alisema CCM ni chama kinachotetea maslahi ya wanyonge na wananchi wa hali ya chini, hivyo akawataka kutathmini katika kipindi chote tangu Uhuru kama CCM imeshindwa kulitimiza hilo.
Aidha, alisema chama hicho kimekuwa kikitekeleza kwa vitendo mchango wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, ambao ni umoja na mshikamano, vinavyoifanya Tanzania kuendelea kuwa kisiwa cha amani.
Mwanasiasa huyo ambaye katika jamii ya Wamasai anaheshimika kwa kuwa kiongozi wao mkuu wa kimila, alisema CCM ni chama ambacho kimekuwa kikitetea maslahi na rasilimali za nchi kutoporwa na wageni.
Aliwaeleza kuwa CCM ni chama kinachotoa nafasi kwa wanachama wake kuwa na haki ya kuchagua na kuchaguliwa bila mizengwe ya ubaguzi wa rangi, ukabila au udini.
Aidha, alisisitiza kuwa chama hicho kina utaratibu wa kujisahihisha makosa kwa kufuata vikao halali, hivyo kwa msingi huo, aliwataka wanachama wanaofikiria kuhama, kutathmini ili wasije kujuta mbele ya safari.
Naye Jasmine Shamwepu anaripoti kutoka Dodoma kuwa CCM imefanya maandamano ya kupinga kauli ya Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema), wakisema ni za kibaguzi na zinaweza kuleta machafuko.
Maandamano hayo yalifanyika mjini humo, huku wana CCM wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali ukiwamo wa "Chadema wanataka kutengana bora watengane wao na familia zao kuliko kuigawa nchi ambayo ina amani."
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wanawake (UWT), Amina Makilagi alisema CCM wanaamini nchi imezoea umoja na mshikamano na kama Chadema hawataki amani, basi wasilete machafuko ambayo yanaweza kuleta mgawanyiko usiokuwa na maana yoyote.
Makilagi alifafanua kuwa kauli iliyotolewa na Nassari kwamba Rais Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wasifike Ukanda wa Kaskazini, ni dhamira yake wala si kwa bahati mbaya.
Hata hivyo Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema kauli hiyo iliyojaa utoto ni ya Nassari binafsi na si ya chama hicho.
"Mwaka 2005 na 2010 katika kampeni zao za uchaguzi, walitangaza kuwa lazima damu imwagike na sasa dhamira yao imeanza kwa kutoa kauli za uchochezi ambazo zinaweza kuleta machafuko," alisema Makilagi.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa, Martini Shigela alimtaka Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa kuchukua hatua kwa kutolea maelezo kuhusu kauli hiyo ya Nassari ambayo inaweza kuleta machafuko na kugawa Watanzania.
"Msajili anatakiwa achukue hatua na asilinyamazie suala hili, kwani ni kubwa na ni kitendo cha kujitenga na kutaka wao wawe Jamhuri ya Kaskazini, kwa jambo hilo tayari Chadema wameshaitenga Zanzibar," alisema Shigela.
sosi: HabariLeo | Lowassa akataza wanachama kuhama CCM
MBUNGE wa Monduli, Edward Lowassa amekuwa akifanya mikutano ya ndani na ya hadhara jimboni humo katika kinachoonekana ni kuzima wimbi lililoibuka hivi karibuni la wanachama wa CCM kuhamia Chadema.
Tangu kujiuzulu kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) wa Mkoa wa Arusha, James ole Millya, limekuwapo wimbi la wana CCM kuhamia Chadema katika mikoa kadhaa nchini.
Mbali na Millya, wanachama wa CCM wakiwamo viongozi wenye nafasi za udiwani, walitangaza kuhamia Chadema ambayo moja ya ngome zake ni Arusha iliko na wabunge wawili; Arumeru Mashariki na Karatu.
Chadema pia ilikuwa ikiongoza Jimbo la Arusha Mjini kabla ya matokeo yake kutenguliwa na Mahakama Kuu ya Tanzania kutokana na kesi iliyofunguliwa na wanachama watatu wa CCM.
Lowassa alifanya mikutano ya ndani jana eneo la Mto wa Mbu na wa hadhara, ambako aliwaambia wananchi, kwamba pamoja na kuwa suala la kujiunga na chama chochote cha siasa ni haki ya yeyote, lakini haoni umuhimu wa wanaCCM kuhama sasa.
Mbunge huyo ambaye alikuwa Waziri Mkuu katika miaka ya kwanza ya Serikali ya Awamu ya Nne hadi alipojiuzulu Februari 2008, alisema CCM ni chama kinachotetea maslahi ya wanyonge na wananchi wa hali ya chini, hivyo akawataka kutathmini katika kipindi chote tangu Uhuru kama CCM imeshindwa kulitimiza hilo.
Aidha, alisema chama hicho kimekuwa kikitekeleza kwa vitendo mchango wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, ambao ni umoja na mshikamano, vinavyoifanya Tanzania kuendelea kuwa kisiwa cha amani.
Mwanasiasa huyo ambaye katika jamii ya Wamasai anaheshimika kwa kuwa kiongozi wao mkuu wa kimila, alisema CCM ni chama ambacho kimekuwa kikitetea maslahi na rasilimali za nchi kutoporwa na wageni.
Aliwaeleza kuwa CCM ni chama kinachotoa nafasi kwa wanachama wake kuwa na haki ya kuchagua na kuchaguliwa bila mizengwe ya ubaguzi wa rangi, ukabila au udini.
Aidha, alisisitiza kuwa chama hicho kina utaratibu wa kujisahihisha makosa kwa kufuata vikao halali, hivyo kwa msingi huo, aliwataka wanachama wanaofikiria kuhama, kutathmini ili wasije kujuta mbele ya safari.
Naye Jasmine Shamwepu anaripoti kutoka Dodoma kuwa CCM imefanya maandamano ya kupinga kauli ya Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema), wakisema ni za kibaguzi na zinaweza kuleta machafuko.
Maandamano hayo yalifanyika mjini humo, huku wana CCM wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali ukiwamo wa "Chadema wanataka kutengana bora watengane wao na familia zao kuliko kuigawa nchi ambayo ina amani."
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wanawake (UWT), Amina Makilagi alisema CCM wanaamini nchi imezoea umoja na mshikamano na kama Chadema hawataki amani, basi wasilete machafuko ambayo yanaweza kuleta mgawanyiko usiokuwa na maana yoyote.
Makilagi alifafanua kuwa kauli iliyotolewa na Nassari kwamba Rais Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wasifike Ukanda wa Kaskazini, ni dhamira yake wala si kwa bahati mbaya.
Hata hivyo Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema kauli hiyo iliyojaa utoto ni ya Nassari binafsi na si ya chama hicho.
"Mwaka 2005 na 2010 katika kampeni zao za uchaguzi, walitangaza kuwa lazima damu imwagike na sasa dhamira yao imeanza kwa kutoa kauli za uchochezi ambazo zinaweza kuleta machafuko," alisema Makilagi.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa, Martini Shigela alimtaka Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa kuchukua hatua kwa kutolea maelezo kuhusu kauli hiyo ya Nassari ambayo inaweza kuleta machafuko na kugawa Watanzania.
"Msajili anatakiwa achukue hatua na asilinyamazie suala hili, kwani ni kubwa na ni kitendo cha kujitenga na kutaka wao wawe Jamhuri ya Kaskazini, kwa jambo hilo tayari Chadema wameshaitenga Zanzibar," alisema Shigela.
sosi: HabariLeo | Lowassa akataza wanachama kuhama CCM