Lowassa aibua vita mpya

Lowassa aibua vita mpya

Wana Jf, jana usiku nikiwa ni melala, kiusingizi kikanichukua kama tulivyo zoea kusema. Nikiwa ktk usingizi mara nikajikuta nikiwa katika mahojiano na lowassa, na mahojiano yetu yalikuwa hivi.

Twijuke. Mheshimiwa pele na majukumu

Lowassa: Ashsante kijana

Twijuke: Mzee wangu naona fahari kukaa meza moja nawe lakina pia nafasi hii adim inayoliliwa na wengi, mzee wangu sina mengi sana bali machache ambayo ningependa kujua juu yako.

Lowassa: Kama yepi hayo kijana ungependa kujua

Twijuke : Mzee wangu kwanza binafsi ningependa kujua kuhusu Richimond, kwani yamenenwa mengi kuhusu zabuni iliyo tolewa kwa kampun ile ya kufua umeme inasadikiwa ulitoa upendeleo na wengine wanaenda mbali na kusema kuwa wewe ndo uliye ileta hapa nchini ile kampuni je! nikweli

Lowassa: Sikiliza kijana kilchotokea kati yangu na mwenzangu kwenye jambo lile la Richimond, ni sawa na babako na mamako wapo kwenye gari moja na mwedeshaji wa gari lile ni babako, na wakiwa safarini babako anamgonga mtu anakufa, sasa babako na mamako wanakubaliana kuwa kwamba hii ni kesi na hivyo tukihojiwa tuseme mama ndo aliye gonga ili babako aweze kushugulikia mabo na hatimaye kumaliza kesi kuliko babako kuwa ndani na mamako ahangaike. Umenielewa?

Twiujuke: Hapa mzee wangu nimekuelewa ila umenifumbua macho japo jibu ni tata linahitaji king'amuzi. Mzee wangu ebu nambie, baada ya misukosuko yote hiyo badaye watu wamezusha kuwa eti wewe na Jk hampatani na sasa kila mtu na mabo yake, je ni kweli?

Lowassa: Sikiliza kijana, achana na mambo ya magazeti, Jk ni bwana mdogo na ni rafiki yangu kitambo, mahusiano yangu naye si ya njiani, mimi ndo nimemfikisha hapo alipo na nakuibia siri, kitendo cha watu kuona hatuelewani hilo ndo hitaji letu.

Twijuke: Aasante sana mzee wangu kuning'amua, ebu nambie mzee wangu kuna suala hili la wewe kuutaka urais mwaka 2015
je unalizungumziaje!

Lowassa: hilo la mimi kuutaka urais halihitaji miwani.

Twijuke: Mara nikastuliwa na Alarm kumbe mida ya kwenda kuusaka mkate ikwa imewadia, ndugu yangu nilikuwa na shehena ya maswali lakini ndo hivyo tena.

Ujumbe mzur sana. Ila ukiota tena mwambie sio vizur kuwadanganya police. Tungemwamin sana angefunguka kipindi kile kuliko sasa ingawa ajachelewa bdo awe mkwel kwenye campen zake. Atapata kura za kutosha
 
Kazi ipo kweli mwaka 2015......ki ufupi patachimbuka sana.....
 
Kikosi cha ccm....goli kipa baba rizi 2 lowasa 3 .Nape nnauye 4.. makonda 5 mwakyembe 6 membe 7 Ngeleja 8 mgana msindai 9 mwigulu nchemba 10 Saada mkuye 11..sita substution.. magufuli..kange lugola..Deo filikunjombe....kessy...maneger...Ali khasan Mwinyi na Kingunge ngimbale Mwiru....
 
Kwa Lowasa, kuliko Membe/Sitta/Mwakyembe kuwa raisi, ni bora CDM wachukue nchi and vice versa. ..
Mkuu Tuko, naungana na wewe, ila ili Chadema iweze kuchukua nchi, huyu jamaa akataliwe CCM, ahamie Chadema, awe ndio mgombea wenu wa urais, vinginevyo kwa Chadema hivi ilivyo, ukimuondoa ZZK, haina mgombea mwingine yoyote, mwenye uwezekano wenye kuwezekanika kuchagulika kuwa rais wa JMT!.

Naomba utofautishe mgombea urais na mgombea mwenye uwezekano wa kuwezekanika kuchagulika kuwa rais wa JMT. Wote waliopo kwa sasa, wana uwezekano wa kuwa wagombea tuu, lakini hakuna mwenye uwezekano wa kuwezekanika kuchagulika!.

This is very bitter truth, you'll have to swallow hike kidoge kichungu, kuwa 2015, ni CCM tena!, unless otherwise!.
Pasco.
 
Rose kamili ametangaza kugombea urais wa tz kupitia chadema
huyo an amfadhaiko wa roho...Dr. akimpigia simu ya salamu mchezo unaisha......ila sijui Lowasa na jinsi vijana watakavyomzodoa na kumpandisha hasira kam CCM itapona haraka.
 
Wakikuhitaji kuthibitisha mahojiano yako na EL,mi nitakuwa shahidi no.1 niliicheki movei mpaka mwisho.
 
Mkuu Tuko, naungana na wewe, ila ili Chadema iweze kuchukua nchi, huyu jamaa akataliwe CCM, ahamie Chadema, awe ndio mgombea wenu wa urais, vinginevyo kwa Chadema hivi ilivyo, ukimuondoa ZZK, haina mgombea mwingine yoyote, mwenye uwezekano wenye kuwezekanika kuchagulika kuwa rais wa JMT!.

Naomba utofautishe mgombea urais na mgombea mwenye uwezekano wa kuwezekanika kuchagulika kuwa rais wa JMT. Wote waliopo kwa sasa, wana uwezekano wa kuwa wagombea tuu, lakini hakuna mwenye uwezekano wa kuwezekanika kuchagulika!.

This is very bitter truth, you'll have to swallow hike kidoge kichungu, kuwa 2015, ni CCM tena!, unless otherwise!.
Pasco.

Never....
Lowassa ni mtu dhaifu sana mbele ya CDM. Rejea uchaguz wa Arumeru
 
Watu wanamtumia lowassa kujitaftia jina, mmemfanya barabara kila m2 anatuhuma ila evidence hanaa, midomoo malii yenuu ongeeni kwanii hamlipii vat, badalaa muongee mambo yanayo kabilii nchii, kuna tatizo la ajira vijanaa mmekaa kimyaa kila siku lowasa sijuii nani aliwachaguwa ninyi muwe viongoziii hawakupima thnkng capacity yenu bali physical 2
 
Ivi Lowasa akiupata urais kwa jitihada zake binafsi, je kuna mtu atamuuliza kitu kweli au ndo atakua anatujibu "urais wangu hauna ubia na mtu"!?
 
Tahadharii kuna watu mnaamka toka usingiziini na kucomment watu wa namna hyo ni hatarii sana, nukuu kuna m2 kasema eti kama aeshindwa monduli, tanzania ndio ataiweza bila shaka huyo ni empty mind, au vepa kbsaa hana alijualo
 
Kwa namna yoyote ile Lowassa hazuiliki kufanya anayotaka ndani ya CCM na kuna madhara makubwa wasipompitisha awe mgombea Urais kwa tiketi ya CHAMA CHA MAPINDUZI.
 
Never....
Lowassa ni mtu dhaifu sana mbele ya CDM. Rejea uchaguz wa Arumeru
Arumeru ni CCM wenyewe kwa wenyewe walihujumiana kwa kumhujumu chaguo la EL ili kumkomoa!. 2015 CCM ikirekebisha makosa, jimbo linarejea kwao!. Tena kiukweli kama Chadema inataka kuyalinda baadhi ya majimbo yake, haina budi kuwasaidia baadhi ya wabunge wake dhaifu katika ufuatiliaji, usimamizi na utekelezaji, vinginevyo 2015, itayapoteza!.
Pasco




 
Back
Top Bottom