Lowassa adaiwa kutaka kuuawa!

Lambardi

Platinum Member
Joined
Feb 7, 2008
Posts
19,989
Reaction score
24,023
Wakuu heshima mbele, kwenye magazeti ya leo imefahamika kuwa Fredrick Lowassa mtoto mkubwa wa EL amereport kuwa UWT wana mpango wa kumuua baba yake kwa kile ambacho hakijawekwa bayana!

Kama ada wanajamvi kwa weledi, tunapenda kujua kimetokea nini ghafla hivyo au ni kujihami baada kushukiwa na kuwalisha sumu baadhi ya wapambanaji wa ufisadi?

Nawasilisha
 
Siwezi changia mpaka nipate detailed information about this issues,otherwise nitatoa mipasho kitu ambacho sikitaki....well,hoja yenyewe ni tamu kama ikipatikana nyama ya kujazia ili ivutie watu kuchangia kwa upana wake...
 
Mkuu kama nakuelewa unachosema ni kuwa Fedriki Lowasa Amedai kwa baadhi ya vyombo vya Habari kuwa Idara ya Usalama wa Taifa ina Njama za Kumuua Baba yake EDUWADI LOWASA Mbunge wa Munduli, Waziri mkuu Aliyejiuzulu baada ya Sakata la RICHIMODI?

Unataka tuelewe hivyo? Tutajie baadhi ya Magazeti yenye Taarifa hizo.
 
Skills heshima mbele sana mkuu,

Mkuu uko humu jamvini since 2008, huwezi kuleta habari kama hii juu juu tuu, hebu toa hii habari kwa kina na mapana zaidi, ikiwezekana quote na hayo magazeti hapa, ili watu wapate picha kamili kabla ya kuchangia hapa.
 
Mkuu,

Leo wakati Wasiwasi Mwabulambo anachambua magazeti (jioni) alisoma hiyo caption sasa mleta mada kaileta bila kujalizia ili ilete full context

Imetoka kwenye local tabloids (labda wenye access watusaidie - huku nabi gate hakuna n'gazeti)
 
Anatafuta huruma za wabongo.... hiyo ni straregy tu kwa wenye akili tunajua, nani atamuua huko UWT wakati wapambe wake hapa kutwa wanatuaminisha usalama wa taifa wanamuunga mkono yeye?
 
Mleta thread ameleta hii taarifa ili kuwafanya watu wahamishie mawazo huko badala kusherehekea xmass. Kama kweli ayataje hayo magazeti
 
Huyu Lowassa mdogo naye si alitajwa katika kumuua Mwakyembe, aliwapelekea mbuzi wale Alshabaab. Sasa anaweweseka baba yake kuuwawa. Tutasikia mengi sana hadi 2015
 
Mwakiembe anataka kujibu mapigo? Ok wapi jkey?
 
EL ndie Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, hivyo TISS iko chini yake unless ni covert oparation kama walivyonfix Imran Kombe!.

thanks pasco, kwa weledi na upeo wako, we unadhani likelihood ya hilo kutokea yaweza kwenda percentage gani?
 
aisee..... Sasa mbona kuna watu wanasema yeye ndio anataka kuua wenzake?? Au ndio political games?
alot of kujichanganya apa mbona mnarukia yale (majamaa machakachuaji ya kura tunazopiga) mashushushu ya pale makumbusho kwa nyuma (uwt) why not... Umoja wa wanawake tanzania, umoja wa walimu tanzania au usalama wa taifa, ebu weka vizuri tutoe pwenti zetu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…