Love story (True story)

Love story (True story)

Rich Pol

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2013
Posts
7,877
Reaction score
5,694
Kianzia leo nitakuwa nawawekea love story ya Faiza Ally mzazi mwenzake na mh. Joseph Mbilinyi (Sugu) anayoendelea kuitoa ktk mtandao wa Instagram na Facebook.

Kwakuwa ni yeye mwenyewe ameutoa sina budi kuwaletea hapa wana JF ambao hawana access au muda wa pupita ktk mitandao hiyo.
Naanza.

Sehemu ya 1

Alinitumia friend request FB baada ya kumkubalia urafiki sikujua kama yeye ni nani na anafanya nini na hii ni kawaida yangu mtu ambae simfahamu na tumekuwa marafiki kwa muda mrefu ndiyo naingiaga katika profile yake.

Tulichat mala kadhaa nikiwa najua ni kijana tu kama vijana wengine, baada ya kuchukua namba yangu ktk kupitia page yangu ya FB mala kadhaa alikuwa ananipigia simu usiku mida ya saa tano na saa sitaakiwa ananiomba tuonane.
Hallo hallo naweza kukuona?

Mimi nilikuwa namshangaa sana inakuwaje ghafla si kiheshima as mtu anakununua nikamjibu unapigaje simu ghafla unataka kuniona usiku?
Akanijibu ndiyo ameingia.

Nikamuuliza kwanini usinipe taarifa kabla ya siku kadhaa kuniona? Mimi siwezi kukurupuka kiasi hicho.
Kumbe yeye alikuwa anatumia umaarufu wake na uongozi wake wakati huo mimi sijui yeye ni nani

INAENDELEAA.
 
Duuuh hivi Sugu asingekuwa maarufu angeandika hiyo story yake mitandaoni! Sometimes we have to be careful with whom we going out with
 
Sehemu ya 2

Aliendelea kunipigia simu usiku ghafla kama kawaida yake na mimi sikuwa naenda halafu nilikuwa namba yake hata sijai save
Kutokana na namna alivyokuwa anaongea kila akinipigia simu namuuliza wewe ni nani?
Akanijibu mimi ni fulani (jina lake silipendi kuliweka hapa) yeye akawa anadhani namjua sasa nikamuuliza cousin wangu Farida unamjua mtu fulani?
Akasema ndiyo.... ndiyo nikaamua sasa kuingia ktk profile yake nikaangalia picha zake....... ndiyo nikamjua na Farida akaniambia anampenda sana huyo, kiukweli sikuwa najua nyimbo zake lakini kuna nyimbo moja nilikuwa naijua ila sikuwa najua kama yeye ndiyo kaimba.
Farida akawa ananiambia nyimbo zake basi tukawa tuna tabasamu......
Tukajiona tuna bahati kumjua pia pia nilitamani kumuona live lakini nilijikaza sana kwa sababu sikupenda ambavyo alikuwa akiniita ghafla usiku ni mtu fulani ambae anatumia jina lake na mimi nikakaza kwa hiyo sikuwahi kwenda kabisa .
Basi nilimpotezea sana kwa muda mrefu kuna siku tulikutanana online akawa ananitongoza rasmi hapo sasa nilikuwa tayari namjua kama yeye ni msanii nikawa namwambia
Bwana mimi naomba tuwe marafiki wa kawaida tu
Nikamwambia mimi nina mpenzi wangu ba hapa nilipo na pete ni mchumba wa mtu.
Alisema ndiyo lama kutoka na mimi basi wewe kama hutaki kutoka na mimi basi tuwe marafiki, wewe kuwa rafiki yangu siwezi.
Mmmmh nilishangaa maana yeye alikuwa ni msanii na niliona kama ananinyima haki ya kuwa shabiki wake nikamtolea mfano wa huyo msanii mwingine.
Nikamuuliza kwani nyie mkoje? Mpaka mlale na mtu ndiyo mjione wanaume? Basi tukaishia hapo kuchat akiwa anasisitiza anataka kuni.... tena anataja lile neno gumu.
Alinistaajabisha yaani nilizoea kutongozwa kistaarabu kwa heshima lakini hapo heshima ilikuwa 0
Itaendelea.....
 
Sehemu ya 2

Aliendelea kunipigia simu usiku ghafla kama kawaida yake na mimi sikuwa naenda halafu nilikuwa namba yake hata sijai save
Kutokana na namna alivyokuwa anaongea kila akinipigia simu namuuliza wewe ni nani?
Akanijibu mimi ni fulani (jina lake silipendi kuliweka hapa) yeye akawa anadhani namjua sasa nikamuuliza cousin wangu Farida unamjua mtu fulani?
Akasema ndiyo.... ndiyo nikaamua sasa kuingia ktk profile yake nikaangalia picha zake....... ndiyo nikamjua na Farida akaniambia anampenda sana huyo, kiukweli sikuwa najua nyimbo zake lakini kuna nyimbo moja nilikuwa naijua ila sikuwa najua kama yeye ndiyo kaimba.
Farida akawa ananiambia nyimbo zake basi tukawa tuna tabasamu......
Tukajiona tuna bahati kumjua pia pia nilitamani kumuona live lakini nilijikaza sana kwa sababu sikupenda ambavyo alikuwa akiniita ghafla usiku ni mtu fulani ambae anatumia jina lake na mimi nikakaza kwa hiyo sikuwahi kwenda kabisa .
Basi nilimpotezea sana kwa muda mrefu kuna siku tulikutanana online akawa ananitongoza rasmi hapo sasa nilikuwa tayari namjua kama yeye ni msanii nikawa namwambia
Bwana mimi naomba tuwe marafiki wa kawaida tu
Nikamwambia mimi nina mpenzi wangu ba hapa nilipo na pete ni mchumba wa mtu.
Alisema ndiyo lama kutoka na mimi basi wewe kama hutaki kutoka na mimi basi tuwe marafiki, wewe kuwa rafiki yangu siwezi.
Mmmmh nilishangaa maana yeye alikuwa ni msanii na niliona kama ananinyima haki ya kuwa shabiki wake nikamtolea mfano wa huyo msanii mwingine.
Nikamuuliza kwani nyie mkoje? Mpaka mlale na mtu ndiyo mjione wanaume? Basi tukaishia hapo kuchat akiwa anasisitiza anataka kuni.... tena anataja lile neno gumu.
Alinistaajabisha yaani nilizoea kutongozwa kistaarabu kwa heshima lakini hapo heshima ilikuwa 0

Itaendelea.....
Ahahaaaa.
Kumbe SUGU heshima zero.
Sasa kama kiongozi heshima zero jee anaowaongoza si ndio vilaza zaidi!!!!
Anyway,ngoja waje wathibitishe.
 
Ahahaaaa.
Kumbe SUGU heshima zero.
Sasa kama kiongozi heshima zero jee anaowaongoza si ndio vilaza zaidi!!!!
Anyway,ngoja waje wathibitishe.

Mbona katumia lugha rahisi sana,amesema amezoea kutongozwa kistaarabu,sasa jiulize kwanini asitoe kwanza story za hao wastaarabu akaanza na huyu?,na hao wastaarabu wake kwanini walimtema/aliwatema?
 
sehemu ya 3

Naada ya kukataa kumuona kwa muda akaanza kuniambia unaniogopa kuniona kwa sababu wewe siyo wa kwenye picha hizo ninazoziona FB kama kweli ni wewe ungeniona.
Haah haah haah.. nilicheka sana nikagundua kumbe kuna watu wanawekaga picha ambazo siyo zao tukawa tunaanza kubishana na mimi nikamwambia ni mimi yeye anasema siyo mimi ..
Na mimi ktk uhalisia ni mbishi na ubishi wangu natakaga mpaka ukweli ueleweke nikahisi kama ametumia njia hiyo lakini na mimi nikaona kwanini anione mimi muongo? Wakati siyo? Lakini bado sikwenda kumuona kwaajili ya hilo.
Sasa ikafikia siku naenda Dodoma kumuona baba yangu alikuwa mgonjwa (mimi mzaliwa wa Dodoma na ndiyo kwetu kwa wazazi wangu nimesoma na kukulia huko)
Nikiwa njiani nikawa namfikiria maana na yeye alikuwa dodoma kikazi.
Nikampigia simu nikamwambia niko njiani naenda Dodoma
Akajibu akaniambia dah... na mimi niko njiani naenda maana kuna vurugu inanibidi nikaotulize lakini kwa jinsi ninavyotamani kukuona kesho hiyo hiyo nageuza hata nikifika usiku nitakushtua.
Nilimjibu powa
Kiukweli mimi Dodoma huwa nikienda napenda sana disco kwasababu huwa nakutana na marafiki zangu tuliosoma nao na watu ninaowafahamu sasa kwa sababu na wewe ni msanii tukitoka wite itakuwa mzuka basi kweli kesho yake akageuza alipofika akanipigia simi kiwa yiko sehemu fulani
Nikamwambia poa na mimi leo naenda club akasema poa basi njoo unichukue nikamwambia poa....
Nikawasha gari mpaka alipo nikampigia simu lakini haikupokelewa nkkaona mmh sijui ndiyo tabia za kisanii? Samahani kwa kusema hivyo mimi naonaga wasanii wengi ni WASHAMBA.
nasema washamba kwanza hawajui ku keep ahadi na wanaonaga kwa aajiri ya jina tu wao ni kila kitu nikasema sasa haya ni mambo gani?
Nikiwa njiani naenda club akanipigia simu uko wapi...
Nikamjibu nimekuja mpaka hapo hukupokea simu naenda zangu club njoo wewe mimi siji tena akasema powa.
Niko club mala nikamuona na marafiki zake sasa nikawa naona noma kwenda nikawa namtizama kwa mbali japo niko karibu nae,
Kiukweli hata mimi nilianza kumtamani kumuona kwa karibu.
ITAENDELEAA...
 
Back
Top Bottom