Lost Decades - In Search of Ujamaa

Zakumi

JF-Expert Member
Sep 24, 2008
5,063
2,471
Wana JF:

Kushindwa kwa siasa kunatokana na sababu za nje na za ndani. Mpaka sasa watanzania wengi wanafikri kuwa Ujamaa ulishindwa kwa sababu za nje. Wanafikri kulikuwa na maadui ambao hawakutaka sisi kuendelea.

Kwa zaidi ya miaka miwili sasa nimefanya kazi ya utafiti na matokeo niliyopata ni kuwa Ujamaa umeshindwa na ulipotezea Tanzania muda wa kupiga hatua kwa sababu ni siasa mbaya. Na hakuna sababu hata moja ya nje yaliofanya ujamaa kushindwa na haya ni maelezo yangu.

Ujamaa ulishika hatamu kati ya mwaka 1967 mpaka 1981. Katika kipindi kulikuwa na matatizo kama vile ukame, vita vya uganda, kuvunjika kwa jumuia ya Afrika mashariki na kupanda kwa bei ya mafuta. Hizi sababu zilitosha kuhujumu siasa za Ujamaa.

Lakini pamoja na hayo katika kipindi hicho hicho, Tanzania ilikuwa ni nchi inayoongoza katika nchi zilizo kusini mwa jangwa la sahara kwa kupokea misaada. Tulipewa zaidi ya dollar billion 3.

Hivyo misaada tuliyopewa ilikuwa ni mikubwa ya kuweza ku-counter balance, negative impacts ya ukame, kupanda kwa bei ya mafuta, vita vya Uganda na kuvunjika kwa jumuia EA.

Vilevile katika kipindi hicho kulitokea expansion ya viwanda. Wafanyakazi wa viwanda waliongezeka kwa asilimia 8 kwa mwaka lakini uzalishaji wao ulipungua kwa 3.5 kwa mwaka.

Kipindi hiki kilikuwa na uhaba wa biadhaa za viwandani. Na waungwana wengi hapa wanasema kuwa ulitokana na wahujumu uchumi. Lakini sources zangu zinaonyesha kuwa viwanda vilikuwa vinafanya kazi kwa kiwango vya asilimia 45 tu. Je hiyo 55 kwanini hatukuweza kuifikia.

Vilevile Tanzania ikaanza kuwa muagizaji wa chakula kutoka nje. Kwenye nchi kama yetu yenye siasa inayojidai kuwa bora kwanini tuagize chakula?
 
Ujamaa/Ubuntu-maniac naomba unitumie mada kamili kwenye barua yangu pepe. Huu muhtasari wako una walakini kihistoria. Hivyo nataka niichambua mada yako kamili katika muktadha wa historia ya uchumi-siasa. Kwanza kabisa Ujamaa haukutekelezwa kati ya mwaka 1967 na 1981. Rejea sera ya uwekezaji ya wakati huo. Pia rejea zile sera za mifugo na maranchi yaliyofadhiliwa na Wamarekani. Hali kadhalika rejea sera za uwekezaji zilizofagiliwa na Benki ya Dunia na Fuko la Fedha Duniani. Ni mwongo mmoja tu wa 1967 -1977 ambao walau unaweza kusema kulikuwa na kamfano ka utekelezaji wa Ujamaa na sio kamwongo kalikopotea - Mwongo uliopotea ni wa 1980 -1990 wakati wa zile sera zenu za kubadilisha mfumo, yaani, Structural Adjustment Programms (SAPs). Naenda kwenye warsha kuhusu eti jukumu la dola katika maendeleo yanayoongozwa na uchumi wa soko. Nikirejea nitamwaga takwimu na hoja nzito sana kuonesha kuwa tulichokuwa tunatekeleza ni 'State Capitalism', yaani, Ubepari wa Dola' na si Ujamaa. Hakika "you cannot say it [Ujamaa] has failed because it has never been tried" (Mwalimu Nyerere, 1998)!

P.S. Dismal 'Import Substitution Industrialization' was also Ujamaa?
 
Wana JF:

Kushindwa kwa siasa kunatokana na sababu za nje na za ndani. Mpaka sasa watanzania wengi wanafikri kuwa Ujamaa ulishindwa kwa sababu za nje. Wanafikri kulikuwa na maadui ambao hawakutaka sisi kuendelea.

Kwa zaidi ya miaka miwili sasa nimefanya kazi ya utafiti na matokeo niliyopata ni kuwa Ujamaa umeshindwa na ulipotezea Tanzania muda wa kupiga hatua kwa sababu ni siasa mbaya. Na hakuna sababu hata moja ya nje yaliofanya ujamaa kushindwa na haya ni maelezo yangu.

Ujamaa ulishika hatamu kati ya mwaka 1967 mpaka 1981. Katika kipindi kulikuwa na matatizo kama vile ukame, vita vya uganda, kuvunjika kwa jumuia ya Afrika mashariki na kupanda kwa bei ya mafuta. Hizi sababu zilitosha kuhujumu siasa za Ujamaa.

Lakini pamoja na hayo katika kipindi hicho hicho, Tanzania ilikuwa ni nchi inayoongoza katika nchi zilizo kusini mwa jangwa la sahara kwa kupokea misaada. Tulipewa zaidi ya dollar billion 3.

Hivyo misaada tuliyopewa ilikuwa ni mikubwa ya kuweza ku-counter balance, negative impacts ya ukame, kupanda kwa bei ya mafuta, vita vya Uganda na kuvunjika kwa jumuia EA.

Vilevile katika kipindi hicho kulitokea expansion ya viwanda. Wafanyakazi wa viwanda waliongezeka kwa asilimia 8 kwa mwaka lakini uzalishaji wao ulipungua kwa 3.5 kwa mwaka.

Kipindi hiki kilikuwa na uhaba wa biadhaa za viwandani. Na waungwana wengi hapa wanasema kuwa ulitokana na wahujumu uchumi. Lakini sources zangu zinaonyesha kuwa viwanda vilikuwa vinafanya kazi kwa kiwango vya asilimia 45 tu. Je hiyo 55 kwanini hatukuweza kuifikia.

Vilevile Tanzania ikaanza kuwa muagizaji wa chakula kutoka nje. Kwenye nchi kama yetu yenye siasa inayojidai kuwa bora kwanini tuagize chakula?

Ujamaa ni nini?
 
Wana JF:

Kushindwa kwa siasa kunatokana na sababu za nje na za ndani. Mpaka sasa watanzania wengi wanafikri kuwa Ujamaa ulishindwa kwa sababu za nje. Wanafikri kulikuwa na maadui ambao hawakutaka sisi kuendelea.

Kwa zaidi ya miaka miwili sasa nimefanya kazi ya utafiti na matokeo niliyopata ni kuwa Ujamaa umeshindwa na ulipotezea Tanzania muda wa kupiga hatua kwa sababu ni siasa mbaya. Na hakuna sababu hata moja ya nje yaliofanya ujamaa kushindwa na haya ni maelezo yangu.

Ujamaa ulishika hatamu kati ya mwaka 1967 mpaka 1981. Katika kipindi kulikuwa na matatizo kama vile ukame, vita vya uganda, kuvunjika kwa jumuia ya Afrika mashariki na kupanda kwa bei ya mafuta. Hizi sababu zilitosha kuhujumu siasa za Ujamaa.

Lakini pamoja na hayo katika kipindi hicho hicho, Tanzania ilikuwa ni nchi inayoongoza katika nchi zilizo kusini mwa jangwa la sahara kwa kupokea misaada. Tulipewa zaidi ya dollar billion 3.

Hivyo misaada tuliyopewa ilikuwa ni mikubwa ya kuweza ku-counter balance, negative impacts ya ukame, kupanda kwa bei ya mafuta, vita vya Uganda na kuvunjika kwa jumuia EA.

Vilevile katika kipindi hicho kulitokea expansion ya viwanda. Wafanyakazi wa viwanda waliongezeka kwa asilimia 8 kwa mwaka lakini uzalishaji wao ulipungua kwa 3.5 kwa mwaka.

Kipindi hiki kilikuwa na uhaba wa biadhaa za viwandani. Na waungwana wengi hapa wanasema kuwa ulitokana na wahujumu uchumi. Lakini sources zangu zinaonyesha kuwa viwanda vilikuwa vinafanya kazi kwa kiwango vya asilimia 45 tu. Je hiyo 55 kwanini hatukuweza kuifikia.

Vilevile Tanzania ikaanza kuwa muagizaji wa chakula kutoka nje. Kwenye nchi kama yetu yenye siasa inayojidai kuwa bora kwanini tuagize chakula?

Zakumi,
Hata kidogo, hatukupoteza ile miaka ya Nyerere, first of all Ujamaa haukubuniwa kama ni socialist/communist way; ilifuata mila na jadi za kwetu. It was about the African way; and in the first decade nyerere made his best. He built industries which you also mentioned and gave it to the people. The mistake Nyerere did was Nationalization of Agriculture and leaving the segment of farmers/peasants unmanaged.
Believe me, after Nyerere we needed a Sokoine factor; he was the man to take over and correct all mistakes which were made in Nyerere era. The "destroyer" of the system was Mr. Mwinyi; he didn't know what he was doing!
 
Last edited:
Zakumi,
Nadhani kuchambua swala hili bila data itakuwa ni malumbano yasiyo na kichwa wala miguu... Kama una data mwaga hapa kisha watu wacompare. Kwa kuanzia mimi nitafanya analysis ya pamoja.

Kwanza tutazame kilimo, baada ya uhuru mwalimu aliamlisha wanunuzi wakuu wa wakuliwa wawe bodi. The National Agricultural Product Board (NAPB)1962 ndio ilikuwa mnunuzi mkuu. Wao ndio walikuwa wanapanga bei ya kununua mazao, na haikuwa forces za demand and supply. Hivyo wakulima walikuwa hawapati incentive yoyote. Kisha 1973 Mwalimu akaanzisha National Milling Corporation (NMC) ambayo ilikuwa haina tofauti kubwa na NAPB zaidi ya NMC wao walikuwa wanatunza mazao pia. Lakini mkulima alikuwa hafaidi na chochote kile.

1967 Mwalimu aliongoza team na kuunda Azimio la Arusha ambalo liliambatana na Vijiji vya ujamaa.. Watu waliamishwa kutoka kwenye makazi yao na kuwekwa pamoja. Idea ya vijiji vya ujamaa ilikuwa inapendeza kwenye makaratasi, lakini mchakato mzima haukufanikiwa. Vijiji vichache vilipata huduma muhimu kama Afya, elimu na maji.

1970s Nationalization ya Makampuni binafsi. Idea ya mwalimu ilikuwa kupunguza gap kati ya walio nao na wasio nao. Vile vile alikuwa akidhani ataongeza kazi na kutransform uchumi wa Tanzania kutoka kwenye Uchumi unaotegemea kilimo kwenda kwenye ule unaotegemea viwanda. Zoezi hili lilifail moja kwa moja, hakukuwa na incentive kwa wale wanaofanya kazi. Na mwalimu alikubali hili alipo hojiwa na Altaf Gauhar 1984 kwani alisema katika makosa uongozi wake ililofanya ni kunationalize makampuni binafsi.

Sera nyingi za Uchumi za Mwalimu zilikuwa failure, na tunaweza kuangalia data. Lakini kwa upande wa pili wa shillingi nawaze kusema kwamba mwalimu alijaribu kadri ya uwezo wake kutokana na kutokuwa na resouces.
 
Ujamaa/Ubuntu-maniac naomba unitumie mada kamili kwenye barua yangu pepe. Huu muhtasari wako una walakini kihistoria. Hivyo nataka niichambua mada yako kamili katika muktadha wa historia ya uchumi-siasa. Kwanza kabisa Ujamaa haukutekelezwa kati ya mwaka 1967 na 1981. Rejea sera ya uwekezaji ya wakati huo. Pia rejea zile sera za mifugo na maranchi yaliyofadhiliwa na Wamarekani. Hali kadhalika rejea sera za uwekezaji zilizofagiliwa na Benki ya Dunia na Fuko la Fedha Duniani. Ni mwongo mmoja tu wa 1967 -1977 ambao walau unaweza kusema kulikuwa na kamfano ka utekelezaji wa Ujamaa na sio kamwongo kalikopotea - Mwongo uliopotea ni wa 1980 -1990 wakati wa zile sera zenu za kubadilisha mfumo, yaani, Structural Adjustment Programms (SAPs). Naenda kwenye warsha kuhusu eti jukumu la dola katika maendeleo yanayoongozwa na uchumi wa soko. Nikirejea nitamwaga takwimu na hoja nzito sana kuonesha kuwa tulichokuwa tunatekeleza ni 'State Capitalism', yaani, Ubepari wa Dola' na si Ujamaa. Hakika "you cannot say it [Ujamaa] has failed because it has never been tried" (Mwalimu Nyerere, 1998)!

P.S. Dismal 'Import Substitution Industrialization' was also Ujamaa?


Companero:

Karibu Muungwana katika mada. Nadhani katika kichwa cha mada nimeandika IN SEARCH OF UJAMAA. Kwa maana hizo sera zote za 1967-1981 zilikuwa na kuandaa kwenda kwenye Ujamaa.

Hiyo quote yako ya Nyerere "you cannot say it [Ujamaa] has failed because it has never been tried" (Mwalimu Nyerere, 1998)! Inanivunja mbavu sana kwa sababu angefanikiwa angesema "We did it because of Ujamaa."

Katika hotuba yake moja miaka ya mwisho wa 70 alisema kwamba our problems aren't internal, are external by nature. Internally we have good policies and leadership.

His failures not to recognize kwamba hatukuwa tuna-practise ujamaa na kwamba matatizo yetu yalikuwa external was a huge mistake.
 
Zakumi,

Ujamaa haikuwa siasa mbaya ila ulikwama katika utekelezaji na ningeshauri ufanye utafiti zaidi ya hapo ulipoishia kwa kuangalia vilevile shinikizo la nje hasa wakati wa vita baridi.

Kwa taarifa yako, ubepari wenyewe umeanza kuporomoka na serikali za Magharibi wanatafuta namna ya kubadili mfumo huo ambao unaelekea kushindwa.
 
I thought you knew.

I don't know if you know... otherwise tunaweza kujikuta tunazungumzia vitu viwili tofauti kabisa. So, kwa vile mada ni yako na ni kuhusu in search of "ujamaa" itakuwa vizuri utueleze Ujamaa unaoutafuta ni upi.
 
Je inawezekana tulijenga jamii imara kwa kutumia Imani ya Ujamaa lakini tukashindwa kujenga Uchumi kwa mfumo wa Kijamaa?

Tunaposema Ujamaa ulifeli, ni lazima tuonyeshe ulifeli wapi. Ndio Kiuchumi hatukuweza kujijenga imara na hata pamoja na kuwa tulipokea misaada mingi, je tulikuwa na uwezo binafsi na msukumo wa kujizatiti kiuchumi kikamilifu?

Kwenye jamii, Ujamaa ulituletea Umoja na kuweza kujenga Utaifa. Nafikiri kama tusingeimba wote kuwa Binadamu wote ni sawa, sidhani kama ingekuwa kwa Mpemba kwenda kuoa usukumani, tungekuwa kama Kenya.

Hivyo kuna yaliyotusaidia na kuna tuliyoboronga.

Sasa kama Wananchi wameshiba Ujamaa wa Imani, ni lipi linatakikana kufanhyika ili kuamsha uzalishaji na kujenga mfumo bora wa Uchumi mahiri? Je kuendelea kuimba Juhudi na Maarifa na kutilia mkazo wa Kujitegemea ndio jibu?

Je tunapolilia Uchumi wenye nguvu na unono, tunaelewekwa kwa wananchi ambao wameshaokoka kwa kuamini kuwa Utajiri au kuwa na ziada ni sumu?

Je tunaweza kutenganisha Siasa za Ujamaa na Mfumo wa uzalishaji wa Kijamaa katika jamii na Uchumi wetu?
 
Zakumi,
Hata kidogo, hatukupoteza ile miaka ya Nyerere, first of all Ujamaa haukubuniwa kama ni socialist/communist way; ilifuata mila na jadi za kwetu. It was about the African way; and in the first decade nyerere made is best. He built industries which you also mentioned and gave it to the people. The mistake Nyerere did was Nationalization of Agriculture and leaving the segment of farmers/peasants unmanaged.
Believe me, after Nyerere we needed a Sokoine factor; he was the man to take over and correct all mistakes which were made in Nyerere error. The "destroyer" of the system was Mr. Mwinyi; he didn't know what he was doing!

Ujamaa ulitungwa na mwafrica lakini haukufuata mila na desturi zetu. Tanzania ina zaidi ya makabila 120, how could he put the traditions of these tribes together? And you notion that "It was about the African way" is a myth. Don't perpetuate it.

Ali-act kama Santa Claus alipowapa watu viwanda. Kiwanda chenye thamani ya mamilioni, kinapewa meneja ambaye maishani mwake hajawahi kuongoza mradi wa kuzalisha angalau magunia mawili ya magimbi au muhogo.

Na kuhusu farmers/peasants tupo kwenye sahani moja. Nadhani makosa mengine makubwa yalikuwa ni mfumo wa tax ambao hakujali bei katika soko la dunia. Sababu kubwa iliyoleta maendeleo Kilimanjaro, Kagera na Mbeya ilikuwa ni kilimo cha kahawa. Mapato ya mazao hayo ilifanya watu kufanya diversification ya kusomesha watoto, kufungua maduka na other ventures.

Kwa watu wa Iringa, Mbeya, Morogoro, Tanga, Pwani na mikoa mingine iliyokuwa na large scale farming walitegemea mashamba makubwa kama engine za maendeleo yao.
 
Zakumi,
Nadhani kuchambua swala hili bila data itakuwa ni malumbano yasiyo na kichwa wala miguu... Kama una data mwaga hapa kisha watu wacompare. Kwa kuanzia mimi nitafanya analysis ya pamoja.

Kwanza tutazame kilimo, baada ya uhuru mwalimu aliamlisha wanunuzi wakuu wa wakuliwa wawe bodi. The National Agricultural Product Board (NAPB)1962 ndio ilikuwa mnunuzi mkuu. Wao ndio walikuwa wanapanga bei ya kununua mazao, na haikuwa forces za demand and supply. Hivyo wakulima walikuwa hawapati incentive yoyote. Kisha 1973 Mwalimu akaanzisha National Milling Corporation (NMC) ambayo ilikuwa haina tofauti kubwa na NAPB zaidi ya NMC wao walikuwa wanatunza mazao pia. Lakini mkulima alikuwa hafaidi na chochote kile.

1967 Mwalimu aliongoza team na kuunda Azimio la Arusha ambalo liliambatana na Vijiji vya ujamaa.. Watu waliamishwa kutoka kwenye makazi yao na kuwekwa pamoja. Idea ya vijiji vya ujamaa ilikuwa inapendeza kwenye makaratasi, lakini mchakato mzima haukufanikiwa. Vijiji vichache vilipata huduma muhimu kama Afya, elimu na maji.

1970s Nationalization ya Makampuni binafsi. Idea ya mwalimu ilikuwa kupunguza gap kati ya walio nao na wasio nao. Vile vile alikuwa akidhani ataongeza kazi na kutransform uchumi wa Tanzania kutoka kwenye Uchumi unaotegemea kilimo kwenda kwenye ule unaotegemea viwanda. Zoezi hili lilifail moja kwa moja, hakukuwa na incentive kwa wale wanaofanya kazi. Na mwalimu alikubali hili alipo hojiwa na Altaf Gauhar 1984 kwani alisema katika makosa uongozi wake ililofanya ni kunationalize makampuni binafsi.

Sera nyingi za Uchumi za Mwalimu zilikuwa failure, na tunaweza kuangalia data. Lakini kwa upande wa pili wa shillingi nawaze kusema kwamba mwalimu alijaribu kadri ya uwezo wake kutokana na kutokuwa na resouces.

Mkuu nashukuru kwa kujazia data. Hila kuhusu Azimio la Arusha. Blueprint nzima ilikuwa ni kazi ya Nyerere pekee yake. Kulikuwa hakuna team iliyounda kuanzisha Azimio la Arusha.

Kama nipo-Wrong naomba mnipe data.
 
Zakumi,

Ujamaa haikuwa siasa mbaya ila ulikwama katika utekelezaji na ningeshauri ufanye utafiti zaidi ya hapo ulipoishia kwa kuangalia vilevile shinikizo la nje hasa wakati wa vita baridi.

Kwa taarifa yako, ubepari wenyewe umeanza kuporomoka na serikali za Magharibi wanatafuta namna ya kubadili mfumo huo ambao unaelekea kushindwa.

Analysis yangu nimefanya kutoka kwenye uchambuzi WanaEconometrics. Mimi si mtu wa Econometrics. Lakini najaribu tu kufanya juhudi zangu kuelewa ni kitu gani kinaendelea katika fani hiyo.

Fani hii inatumia sana namba. Na namba hazidanganyi. Na kwa maoni ya wanaEconmetrics shinikizo la nje wakati wa vita vya baridi sio sababu ya kuvurunda kwa sera za ujamaa.

Nitajaribu kutoa mfano wa analysis zao kwa kutumia maisha yetu ya kawaida.
Kwa kawaida zetu, tunapopata maafa (shinikizo kutoka nje) ni ukweli kuwa ndugu na jamaa (wahisani) watakuja kukuchangia (harambe au misaada). Hivyo kama katika maafa hayo (shinikizo kutoka nje) ulipoteza 1,000,000 lakini kwenye harambe wahisani wakaweza kuchangia 1,100,000 basi huwezi kulalamika kuwa maafa (shinikizo kutoka) nje ndio chanzo cha matatizo yako.

Lakini ukipewa masaada wa 1,100,000 na baadaye ukaanza kubadilisha style yako ya maisha kwa sababu unazozielewa wewe mwenyewe na baadaye kufiriska basi chanzo sio tena maafa. Chanzo ni wewe mwenyewe.

Kumbukumbu zinaonyesha tulipata maafa lakini wakati huohuo, Tanzania iliongoza kupata misaada kuliko nchi yoyote kusini mwa jangwa la sahara. Hivyo shinikizo la kutoka nje sio sababu ya sisi kushindwa. Ni sera tu.

Enlight me if I am wrong.
 
I don't know if you know... otherwise tunaweza kujikuta tunazungumzia vitu viwili tofauti kabisa. So, kwa vile mada ni yako na ni kuhusu in search of "ujamaa" itakuwa vizuri utueleze Ujamaa unaoutafuta ni upi.

Mkuu naogopa hilo jembe maana companero kashanisomea fatwa (mimi infidel wa ujamaa).

In Search of Ujamaa nina-define kipindi nchi ilikupokuwa inautafuta ujamaa. Hatukuwa wajamaa kamili, we were searching.

Hivyo maana ya Ujamaa nini haitasaidia kwa sababu hilo swali la kinadharia.
 
Je inawezekana tulijenga jamii imara kwa kutumia Imani ya Ujamaa lakini tukashindwa kujenga Uchumi kwa mfumo wa Kijamaa?

Tunaposema Ujamaa ulifeli, ni lazima tuonyeshe ulifeli wapi. Ndio Kiuchumi hatukuweza kujijenga imara na hata pamoja na kuwa tulipokea misaada mingi, je tulikuwa na uwezo binafsi na msukumo wa kujizatiti kiuchumi kikamilifu?

Kwenye jamii, Ujamaa ulituletea Umoja na kuweza kujenga Utaifa. Nafikiri kama tusingeimba wote kuwa Binadamu wote ni sawa, sidhani kama ingekuwa kwa Mpemba kwenda kuoa usukumani, tungekuwa kama Kenya.

Hivyo kuna yaliyotusaidia na kuna tuliyoboronga.

Sasa kama Wananchi wameshiba Ujamaa wa Imani, ni lipi linatakikana kufanhyika ili kuamsha uzalishaji na kujenga mfumo bora wa Uchumi mahiri? Je kuendelea kuimba Juhudi na Maarifa na kutilia mkazo wa Kujitegemea ndio jibu?

Je tunapolilia Uchumi wenye nguvu na unono, tunaelewekwa kwa wananchi ambao wameshaokoka kwa kuamini kuwa Utajiri au kuwa na ziada ni sumu?

Je tunaweza kutenganisha Siasa za Ujamaa na Mfumo wa uzalishaji wa Kijamaa katika jamii na Uchumi wetu?

Hapa inabidi nirudi kwenye historia kupinga wazo lako. Kwa miaka mingi eneo linalojulikana kama Tanzania lilishamiri biashara ya utumwa. Katika biashara hii familia zilivunjika na wakati huohuo makabila kuchanganyika.

Hivyo kuna waarabu wa Pemba ambao wana damu ya kisukuma, Kinyamwezi, kinyasa hivyo Ujamaa haukufanya watu wa makabila mbalimbali kuoana. Kuoana ilishakuwa tabia yetu.

Ujio wa wangoni ulisababisha vita mikoa ya kusini. Watu walichanganyika vilevile.

Vita vya majimaji vilichanganya watu sana. Na bado makabila mengi yalipigana yalipigana vita kumpinga mjerumani.

Je unajua kuwa mmoja wa dada zake Mkwawa aliolewa na Mnyamwezi aliyeishi Uheheni. Je unajua kuwa Mkwawa Mwenyewe aliishi Ugogoni. Je unajua kuwa Mirambo alilelewa na wangoni.

Je unajua kuwa Mirambo alikuwa anafanya biashara na Kabaka wa Uganda.

Ukienda Tarime ugomvi mkubwa ni kati ya koo za kikurya na sio waKurya na makabila mengine.

Makabila ya Tanzaia hayakuishi kwenye isolation na kusubiri ujamaa kutuunganisha. We were mobile people and risk takers.
 
Zakumi said:
Hapa inabidi nirudi kwenye historia kupinga wazo lako. Kwa miaka mingi eneo linalojulikana kama Tanzania lilishamiri biashara ya utumwa. Katika biashara hii familia zilivunjika na wakati huohuo makabila kuchanganyika.

Hivyo kuna waarabu wa Pemba ambao wana damu ya kisukuma, Kinyamwezi, kinyasa hivyo Ujamaa haukufanya watu wa makabila mbalimbali kuoana. Kuoana ilishakuwa tabia yetu.

Ujio wa wangoni ulisababisha vita mikoa ya kusini. Watu walichanganyika vilevile.

Vita vya majimaji vilichanganya watu sana. Na bado makabila mengi yalipigana yalipigana vita kumpinga mjerumani.

Je unajua kuwa mmoja wa dada zake Mkwawa aliolewa na Mnyamwezi aliyeishi Uheheni. Je unajua kuwa Mkwawa Mwenyewe aliishi Ugogoni. Je unajua kuwa Mirambo alilelewa na wangoni.

Je unajua kuwa Mirambo alikuwa anafanya biashara na Kabaka wa Uganda.

Ukienda Tarime ugomvi mkubwa ni kati ya koo za kikurya na sio waKurya na makabila mengine.

Makabila ya Tanzaia hayakuishi kwenye isolation na kusubiri ujamaa kutuunganisha. We were mobile people and risk takers.

Zakumi,

..naunga mkono hoja zako. kilimo cha mashamba makubwa kwa kutumia manamba kulileta mchanganyiko wa makabila. kwa mfano: mashamba ya katani Tanga walipendelea kuchukua manamba toka mikoa ya kusini.

..mfumo wa elimu wa wakoloni pia uliwaunganisha wanafunzi wa makabila mbalimbali. Augustino Ramadhani toka ZNZ, Ibrahim Kaduma toka Iringa, Joseph Butiku toka Mara, Geofrey Mmari toka Kilimanjaro, wote walisoma shule ya Tabora Boyz wakati wa mkoloni.

..lugha ya Kiswahili ilikuwa ikitumika maeneo mengi tu ya Tanganyika kabla ya Uhuru. kama kungekuwa hakuna kuchanganyikana kwa makabila kwa shughuli mbalimbali basi Kiswahili kisingekuwa maarufu kiasi hicho.

..samahani nimetoka nje ya mada...kuhusu masuala ya Ujamaa hayo yana wataalamu wake kama Companero,Mwanakijiji,Mkandara,na Kishoka.
 
Zakumi,

..naunga mkono hoja zako. kilimo cha mashamba makubwa kwa kutumia manamba kulileta mchanganyiko wa makabila. kwa mfano: mashamba ya katani Tanga walipendelea kuchukua manamba toka mikoa ya kusini.

..mfumo wa elimu wa wakoloni pia uliwaunganisha wanafunzi wa makabila mbalimbali. Augustino Ramadhani toka ZNZ, Ibrahim Kaduma toka Iringa, Joseph Butiku toka Mara, Geofrey Mmari toka Kilimanjaro, wote walisoma shule ya Tabora Boyz wakati wa mkoloni.

..lugha ya Kiswahili ilikuwa ikitumika maeneo mengi tu ya Tanganyika kabla ya Uhuru. kama kungekuwa hakuna kuchanganyikana kwa makabila kwa shughuli mbalimbali basi Kiswahili kisingekuwa maarufu kiasi hicho.

..samahani nimetoka nje ya mada...kuhusu masuala ya Ujamaa hayo yana wataalamu wake kama Companero,Mwanakijiji,Mkandara,na Kishoka.

JokaKuu:

Huko ndani ya mada. Maana siku zote tunatajiwa mafanikio ya Ujamaa kwenye vitu ambavyo tayari viliota mizizi.

Mpaka 1985 kulikuwa na wanafunzi wachache sana waliopo kwenye shule za sekondari. Sasa kuwachanganya watu 20,000 kwenye mashule za boarding kunafuta vipi ukabila kwenye taifa lenye watu millioni 20.

Kama ni dawa basi Ujamaa ni Placebo.
 
Zakumi said:
JokaKuu:

Huko ndani ya mada. Maana siku zote tunatajiwa mafanikio ya Ujamaa kwenye vitu ambavyo tayari viliota mizizi.

Mpaka 1985 kulikuwa na wanafunzi wachache sana waliopo kwenye shule za sekondari. Sasa kuwachanganya watu 20,000 kwenye mashule za boarding kunafuta vipi ukabila kwenye taifa lenye watu millioni 20.

Kama ni dawa basi Ujamaa ni Placebo.


Zakumi,

..uko sahihi hapo kwenye mfumo wa boarding schools na ukabila. ni kweli kwamba wanafunzi wa boarding school walikuwa wachache sana kuweza kuwa na impact ktk suala la ukabila.

..vipi kuhusu suala la waalimu, mabwana shamba, wauguzi,waganga, na watumishi wengine wa serikali. nadhani hawa wanaweza kuwa na impact kubwa kuliko ile ya wanafunzi.

..ninavyoelewa watumishi wengi wa serikali walikuwa posted kwenye maeneo ambayo hawana asili nayo. utaratibu huo nao ulianza tangu enzi za mkoloni.

..hata harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika zilijumuisha wananchi wa makabila,dini,na rangi mbalimbali.

..sifa ambayo naweza kumpa Mwalimu Nyerere ni ile ya kutokutumbukiza chuki za kikabila miongoni mwa wa-Tanzania. aliwakuta wa-Tanzania hawana ukabila, akaongoza, na kutuacha hatuna ukabila.
 
Zakumi,

..uko sahihi hapo kwenye mfumo wa boarding schools na ukabila. ni kweli kwamba wanafunzi wa boarding school walikuwa wachache sana kuweza kuwa na impact ktk suala la ukabila.

..vipi kuhusu suala la waalimu, mabwana shamba, wauguzi,waganga, na watumishi wengine wa serikali. nadhani hawa wanaweza kuwa na impact kubwa kuliko ile ya wanafunzi.

..ninavyoelewa watumishi wengi wa serikali walikuwa posted kwenye maeneo ambayo hawana asili nayo. utaratibu huo nao ulianza tangu enzi za mkoloni.

..hata harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika zilijumuisha wananchi wa makabila,dini,na rangi mbalimbali.

..sifa ambayo naweza kumpa Mwalimu Nyerere ni ile ya kutokutumbukiza chuki za kikabila miongoni mwa wa-Tanzania. aliwakuta wa-Tanzania hawana ukabila, akaongoza, na kutuacha hatuna ukabila.

Nadhani heshima kubwa ya Mwalimu ni kuto-take advantage ya nafasi yake. Nchi nyingi za kiAfrika zilipigania uhuru kama waAfrika lakini uhuru ulipopatikana watu walianza kutumia nafasi zao kujiendeleza mwenyewe au makabila yao.

Hivyo siwezi kutia doa lolote lile katika integrity yake.
 
Last edited:

Similar Discussions

Back
Top Bottom