Loliondo, OBC, Dowans: The disturbing connection and secrets

email.gif
E-mail this to a friend
print.gif
Printable version
1344.jpg
Honourable Kaika Saning'o Telele [CCM]
Ngorongoro Constituency Session No Principal Question No To the Ministry of Sector Date Asked 10 137 NATURAL RESOURCES AND TOURISM Forestry/Fishery 15 February 2008 Kwa kuwa hivi karibuni Serikali iliongeza na kutangaza viwango vipya vya ada ya leseni ya uwindaji kwa kampuni zenye vitalu vya uwindaji wa kitalii; na kwa kuwa viwango hivyo vipya viliendelea kulalamikiwa na mengi ya kampuni husika kuwa bei hizo ziko juu mno:-

(a)Je, ni kampuni ngapi za uwindaji zinahusika na zoezi nchini?

(b) Je, tangu viwango vipya vya ada vitangazwe ni kampuni zipi zililipa na ni fedha kiasi gani?

(c) Kwa zile kampuni zitakazoghairi kulipa. Je, ni hatua zipi zitachukuliwa dhidi hayo hasa ikizingatiwa kuwa kwa ujeuri wao huo utaathiri Bajeti ya Serikali ya 2007/2008 pamoja na miradi ya wananchi ambayo ingetekelezwa kwa fedha za uwindaji wa kitalii katika maeneo ya vijiji inayozunguka vitalu hivyo?
ANSWERS TO PRINCIPAL QUESTION #137 SESSION # 10
1190.jpg
Answer From Hon. Mwangunga, Shamsa Selengia
NATURAL RESOURCES AND TOURISM WAZIRI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kaika Telele, Mbunge wa Ngorongoro, lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-

(a) Uwindaji wa kitalii unaendeshwa na kampuni 54 katika vitalu 158 vilivyopo katika mapori ya akiba, mapori tengefu na maeneo ya wazi. Hivyo, ongezeko la ada za uwindaji wa kitalii (vitalu na wanyamapori) kama ilivyo katika tangazo la Serikali Na. 159 la tarehe 29/06/2007 linahusu kampuni zote 54 zenye kibali cha kuendesha uwindaji wa kitalii nchini. Tangazo la Serikali Na. 159 la terehe 29/06/2007 liliwafikia wadau rasmi tarehe 11/07/2007. Wakati huo baadhi ya kampuni zilikuwa zimeshalipia vitalu kwa kiwango cha ada za zamani zilizotumika msimu wa mwaka 2006 cha USD 10,000.00 kwa kila kitalu.

(b) Pamoja na hayo kampuni 11 zimelipa nyongeza ya ada (ada za wanyamapori na vitalu) kikamilifu au sehemu yake ambapo USD 622,540.00 zimekusanywa. Kampuni 42 mpaka sasa hazijajitokeza kufanya malipo. Kampuni zilizolipa nyongeza ya ada au sehemu yake ni kama ifuatavyo:-

(i) Ortello Business Corporation (T) Ltd. imelipa ada zote za wanyamapori na vitalu.

(ii) Morogoro Hunting Safaris (t) Ltd. na Grumeti Reserves zimelipa ada kamili za vitalu.

(iii) Kampuni ambazo zimelipia sehemu ya ada za wanyamapori waliowindwa ni; Rana Tours Ltd, Northern Hunting Enterprises, Game Frontiers, Royal Frontiers, Eco Safaris, Intercon Adventure Safaris na Mwanautu & Co Ltd. Kampuni za Mwanauta & Co. Ltd na Bushman Hunting Safari Ltd zimelipia kitalu kimoja kila mmoja kati ya vitalu viwili vinavyomilikiwa na na kila kampuni hizo.

(c) Kanuni ya 11 (2) (a) (iii) ya Kanuni za uwindaji wa kitalii za mwaka 2000 na marekebisho yake, inatoa Mamlaka kwa Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Kampuni inayoshindwa kulipa ada stahili za Serikali. Hatua hizo ni pamoja na kuzifikisha kampuni husika mahakamani na kuzinyang�anya vitalu.

Mheshimiwa Spika, katika hatua za awali, Wizara yangu imewaandikia wenye kampuni za uwindaji wa kitalii wote barua ya kuwataka walipe madeni yao. Aidha Wizara imefanya majadiliano na wawakilishi wa chama cha wenye kampuni za uwindaji wa kitalii (Tanzania Hunting Operators Association (TAHOA) kuhusu suala la ulipaji wa madeni ambapo makubaliano yamefikiwa kwamba utekelezaji wa malipo ufanyike kabla ya kumalizika kwa mwaka wa fedha wa 2007/2008.

Source: http://www.parliament.go.tz/bunge/parl_question.php?pageNum_quest=2&totalRows_quest=13&memberid=1344
 
Dunia ya leo ni kama kijiji, tekinolojia imekuwa kiasi cha kuweza kuyaona hayo unayoyaona, unafikiri wakati wa Nyerere kulikuwa na tekinolojia namna hiyo? ilikuwa haipo na kama ilikuwepo basi tulikuwa wa Tanzania tunanyimwa. TV tu, Karume kaipeleka Zanzibar miaka chungu nzima kabla yetu, tumeanza kuwa na TV baada ya Nyerere kung'atuka.

Mbona mabango yanayotangaza nchi za watu yapo mengi tu na kwa miaka mingi? inaonyesha muheshimiwa huna exposure ya dunia kabisa. Leo ukienda London utakuta matangazo yanayowataka waIngereza watembelee Tanzania, jee kuna tatizo hapo? ukiwa uropa, nchi nyingi utakuta mitandao ya simu inaingiliana, bila matatizo yoyote, jee kuna tatizo hapo?

Naona aliyeandika hii mada ni limbukeni wa tekinolijia au ana sababu za kijinga, za kuwa waArabu ndio waliokodishwa Loliondo. Mambuga mengi yamekodishwa kwa wawekezaji wa nje, mbona huyasemi na mengi mengine kwa wawekezaji wa Tanzania mbona huyasemi.

Hawa jamaa kwa kuvutia biashara yao, wameamuwa kuwaunganisha wateja wao na mitambo ya kwao na wamepata vibali vyote vya mawasiliano na wamefanya hivyo kwa kutumia fedha yao. Nini cha ajabu katika hilo? hiyo ni mbinu ya kibiashara! ambayo kwa limbukeni kama wewe ni shida kuelewa!

Limbukeni wee! na milimbukeni mingine kibao inakuunga mkono, ama kweli, mi Tanzania bado iko nyuma kibiashara.
 
Dunia ya leo ni kama kijiji, tekinolojia imekuwa kiasi cha kuweza kuyaona hayo unayoyaona, unafikiri wakati wa Nyerere kulikuwa na tekinolojia namna hiyo? ilikuwa haipo na kama ilikuwepo basi tulikuwa wa Tanzania tunanyimwa. TV tu, Karume kaipeleka Zanzibar miaka chungu nzima kabla yetu, tumeanza kuwa na TV baada ya Nyerere kung'atuka.

Mbona mabango yanayotangaza nchi za watu yapo mengi tu na kwa miaka mingi? inaonyesha muheshimiwa huna exposure ya dunia kabisa. Leo ukienda London utakuta matangazo yanayowataka waIngereza watembelee Tanzania, jee kuna tatizo hapo? ukiwa uropa, nchi nyingi utakuta mitandao ya simu inaingiliana, bila matatizo yoyote, jee kuna tatizo hapo?

Naona aliyeandika hii mada ni limbukeni wa tekinolijia au ana sababu za kijinga, za kuwa waArabu ndio waliokodishwa Loliondo. Mambuga mengi yamekodishwa kwa wawekezaji wa nje, mbona huyasemi na mengi mengine kwa wawekezaji wa Tanzania mbona huyasemi.

Hawa jamaa kwa kuvutia biashara yao, wameamuwa kuwaunganisha wateja wao na mitambo ya kwao na wamepata vibali vyote vya mawasiliano na wamefanya hivyo kwa kutumia fedha yao. Nini cha ajabu katika hilo? hiyo ni mbinu ya kibiashara?

Limbukeni wee! na milimbukeni mingine kibao inakuunga mkono, ama kweli, mi Tanzania bado iko nyuma kibiashara.

Dar;

This is not PARTIS PRIS, WATU WANAONGELEA jinsi LOLIONDO ilivyochukuliwa na taratibu zote. Jamaa haijulikani wanasafirisha wanyama HAI au wanasafirisha waliokwisha kuwauwa (kama inavyotakiwa).

Hii ni kwa sababu ndege inatua yenye uwezo/ukubwa wa kubeba watu 400 na hakuna serikali wala TRA mle kwenye eneo walilokodisha.

Kwanini tulipangisha hivi VITALU bila kuweka taratibu za kuwasimamia ???

Dar,
Kuna tatizo na zoezi zima sio kuwa hatujui kuhusu simu....

Dont think we have narrow minds.
 
Wewe Fair Player kwa nini wajiba shida, wewe pumzika tu ndg yangu, huwezi badilisha lolote.
 
Hapana,

Unajua kuna mitanzania mingine hawaelewi, tukiwaacha hawa bila ya kuwaelewesha basi miaka ya baadaye itabidi tuwapige risasi.

Nadhani umenielewa
 
MUUNGANO wa Asasi za Kiraia (FemAct) na mitandao ya wafugaji, kwa pamoja wameitaka serikali kusimamisha operesheni ya kuhamisha wafugaji wilayani Loliondo na sehemu nyingine, kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

Wakitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika jana, Makao Makuu ya Mtandao wa Jinsia nchini, (TGNP), Mwenyekiti wa muungano huo, Jesca Mkuchu alisema kitendo cha kuwahamisha wafugaji kwa kutumia vyombo vya dola, ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

“Kitendo cha kuhamisha wafugaji katika Wilaya ya Ngorongoro, Tarafa ya Loliondo, ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu, haki za raia na uvunjaji wa sheria na katiba, ambapo vyombo vya dola vinafanya hivyo kwa maslahi ya kuipendelea Kampuni ya Ortello Business Corporation,” alisema Mkuchu.
Naye Mkurugenzi wa Kituo cha Haki za Binadamu, Francis Kiwanga alisema, nguvu inayotumiwa kuwaondoa raia hao kutoka katika eneo hilo, sheria za utawala bora hazijafuatwa.

Kwa upande mwingine, Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Usu Mallya alisema, kuna mapungufu mengi yaliyojitokeza katika uingiaji wa mkataba kati ya serikali, wawekezaji, halmashauri za wilaya na vijiji husika.

Akielezea ziara waliyoifanya katika eneo hilo, Mallya alisema, walibaini kuwa, mwekezaji huyo amejenga kiwanda cha ndege na kuwepo kwa mawasiliano ya moja kwa moja kutoka eneo la kitalu kwenda nchi za nje na kwamba ndege kubwa zenye uwezo wa kubeba takribani watu 400 na magari hutua katika uwanja huo.

Watanzania je hizi habari ni za kweli!
Au ndo mwendelezo!
Hii habari toka Tanzania Daima

“Hivi unaweza kuwaambia wazawa wa eneo hilo wanaharibu mazingira wakati mwekezaji ndiye wa kwanza kuharibu mazingira na hata kuteka mawasiliano ya makampuni ya simu kama ilivyotokea katika ziara, simu zetu zilibadilika na kuandika karibu katika Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu?” alihoji Mkurugenzi huyo.

Akielezea zaidi suala hilo, Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake, Ananilea Nkya alisema, kutokana na uingizwaji wa magari yasiyo na namba za Tanzania, haijaeleweka kama kumekuwa na utaratibu upi wa ukusanyaji wa kodi.
Alishangazwa na hatua ya kampuni hiyo kupewa hadhi ya kidiplomasia, huku ikiwa imesajiliwa kama kampuni kwani kambi ya kampuni hiyo hulindwa na Jeshi la Polisi.
 
Wanaijeria waliunda vikosi vya kutetea haki zao katika maeneo yenye mafuta baada ya kuona serikali yao haiwajali kama wanaLoliondo sasa sijui kama hali hiyo itajirudia kwa Morani!! nafkiri nchi hii kwa sasa imeshafikia pabaya. migogoro ni kila pahala jee wadanganyika watakapoamua kutumia moto kudai haki zao itakuwajeee??
Tuombe sana,
Amani.
 
Mimi siku hizi siwaonei huruma watanzania wenye matatizo kwani tunayataka wenyewe, chama kibovu kianuza kila kitu halafu tunaendelea kuwaqpa madara, tunalalama kwanini sasa.

Hacha tukione cha moto ndio tutajua kuwa CCM haifai hata kidogo
 

Attachments

  • FemAct Loliondo 270809 English.doc
    62 KB · Views: 53
  • FemAct August 27 09 Loliondo.doc
    58.5 KB · Views: 89
Nchi hii, basi tu. Ni pale Mumba atakaposhusha moto uteketezao. Watu wadogo/raia hawana tena haki. Inasikitisha tulipofikia hapa kiasi hata cha rais kukumbuka shuka wakati kunakucha kuwa kama hakuna haki kwa walalahoi, basi hakuna utawala wa sheria. Sasa sijui ni kwa vipi vyombo vya sheria vitatekeleza sheria, wakati ni jukumu la serikali kuhakikisha kuwa sheriz zinafuatwa!
 
Hapana,

Unajua kuna mitanzania mingine hawaelewi, tukiwaacha hawa bila ya kuwaelewesha basi miaka ya baadaye itabidi tuwapige risasi.

Nadhani umenielewa

Nadhani kuna baadhi ya wenzetu wanadhani biashara ikishakuwa na kijifaida basi unaachia mambo yajiendee tu! Huko Ulaya anakokutaja hana habari kuwa wao wanavovitendea kazi vya vya kisasa vya ku-monitor movements zote za mfanyabiashara na vifaa vyote vya usafiri. Tanzania hatuna bado uwezo huo, hapo ndipo nashindwa kuelewa hapa ni nani limbukeni?? Ukiviona vinaelea siyo kwamba vimejazwa upepo mzee!! Tafadhali fikiri kwa mapana zaidi. Halafu jaribu kujiuliza kizazi kijacho tunakiachia nini? Yule Mtoto wa kimasai pale Loliondo amekwisha kuwa an Internally Displaced Person (IDP) in his own Country.
 
Ni sheria zetu za ku-copy n cut from India and UK ndio zinatupa taabu!!
 
Dar;

This is not PARTIS PRIS, WATU WANAONGELEA jinsi LOLIONDO ilivyochukuliwa na taratibu zote. Jamaa haijulikani wanasafirisha wanyama HAI au wanasafirisha waliokwisha kuwauwa (kama inavyotakiwa).

Hii ni kwa sababu ndege inatua yenye uwezo/ukubwa wa kubeba watu 400 na hakuna serikali wala TRA mle kwenye eneo walilokodisha.

Kwanini tulipangisha hivi VITALU bila kuweka taratibu za kuwasimamia ???

Dar,
Kuna tatizo na zoezi zima sio kuwa hatujui kuhusu simu....

Dont think we have narrow minds.

Wewe unaona jidege la watu mia nne, wenzako wanaokwenda hapo Loliondo hilo ni private la kubeba mtu na familia yake na wafanya kazi wake wawili watatu.

Tena ulimuona nani anapakia wanyama katika ndege ya abiria?

Jamani, hata hilo mnashindwa kuelewa?
 
Hapana,

Unajua kuna mitanzania mingine hawaelewi, tukiwaacha hawa bila ya kuwaelewesha basi miaka ya baadaye itabidi tuwapige risasi.

Nadhani umenielewa

Criminal minds! ndio maana mkayafilisi mashirika na mawavinda yote ya umma.
 
Nadhani kuna baadhi ya wenzetu wanadhani biashara ikishakuwa na kijifaida basi unaachia mambo yajiendee tu! Huko Ulaya anakokutaja hana habari kuwa wao wanavovitendea kazi vya vya kisasa vya ku-monitor movements zote za mfanyabiashara na vifaa vyote vya usafiri. Tanzania hatuna bado uwezo huo, hapo ndipo nashindwa kuelewa hapa ni nani limbukeni?? Ukiviona vinaelea siyo kwamba vimejazwa upepo mzee!! Tafadhali fikiri kwa mapana zaidi. Halafu jaribu kujiuliza kizazi kijacho tunakiachia nini? Yule Mtoto wa kimasai pale Loliondo amekwisha kuwa an Internally Displaced Person (IDP) in his own Country.

Na katika vitalu vya kuwindia zaidi ya 50 vilivyogawiwa Tanzania wewe umemuona mtoto wa ki Masai tu kuwa ndio kawa displaced, wacheni hayo. Donge hapa si Loliondo wala wa Masai, Donge linajulikana lakini mnashindwa kuweka kinaga ubaga. Hint, yote hayo ni katika agenda za siri, tunajuwa!
 
Lakini wacha wavune walicho kipanda.Waliirudisha CCM madarakani .Na wanaweza tena kumpa Mbunge wa kura arudi na wao kuendelea huhangaika .Waamue leo na mwaka 2010 wamalizie kabisa .

Lunyungu una matatizo kweli wewe,kati wafugaji na wewe nani aliyeirudisha CCM madarakani?

Hii laana ataibeba Ali Hassani Mwinyi, kwa ulimbukeni wake wa kutetemekea waarabu.

Naona na dogo JK anaendeleza uharamia wa mzee wake Mwinyi.
 
Kutokana na serikali kushindwa kuona na kusoma alama za nyakati, mimi nimefikia wakati wa kutangaza vita vyetu wenyewe na serikali yaani kama Burundi, Kongo, Nigeria, na nchi nyingine ambazo hupigana mara kwa mara. Mambo huanza hivi hivi taratibu wakati serikali ikidhani bado watu/wananchi wake ni wajinga nikimaana haelewi kitu. Hebu jamani someni habari hii ya Ijumaa kutoka Tanzania Daima ya tarehe 28, August 2009.
''MUUNGANO wa Asasi za Kiraia (FemAct) na mitandao ya wafugaji, kwa pamoja wameitaka serikali kusimamisha operesheni ya kuhamisha wafugaji wilayani Loliondo na sehemu nyingine, kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

Wakitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika jana, Makao Makuu ya Mtandao wa Jinsia nchini, (TGNP), Mwenyekiti wa muungano huo, Jesca Mkuchu alisema kitendo cha kuwahamisha wafugaji kwa kutumia vyombo vya dola, ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

"Kitendo cha kuhamisha wafugaji katika Wilaya ya Ngorongoro, Tarafa ya Loliondo, ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu, haki za raia na uvunjaji wa sheria na katiba, ambapo vyombo vya dola vinafanya hivyo kwa maslahi ya kuipendelea Kampuni ya Ortello Business Corporation," alisema Mkuchu.

Naye Mkurugenzi wa Kituo cha Haki za Binadamu, Francis Kiwanga alisema, nguvu inayotumiwa kuwaondoa raia hao kutoka katika eneo hilo, sheria za utawala bora hazijafuatwa.

Kwa upande mwingine, Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Usu Mallya alisema, kuna mapungufu mengi yaliyojitokeza katika uingiaji wa mkataba kati ya serikali, wawekezaji, halmashauri za wilaya na vijiji husika.

Akielezea ziara waliyoifanya katika eneo hilo, Mallya alisema, walibaini kuwa, mwekezaji huyo amejenga kiwanda cha ndege na kuwepo kwa mawasiliano ya moja kwa moja kutoka eneo la kitalu kwenda nchi za nje na kwamba ndege kubwa zenye uwezo wa kubeba takribani watu 400 na magari hutua katika uwanja huo.

"Hivi unaweza kuwaambia wazawa wa eneo hilo wanaharibu mazingira wakati mwekezaji ndiye wa kwanza kuharibu mazingira na hata kuteka mawasiliano ya makampuni ya simu kama ilivyotokea katika ziara, simu zetu zilibadilika na kuandika karibu katika Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu?" alihoji Mkurugenzi huyo.

Akielezea zaidi suala hilo, Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake, Ananilea Nkya alisema, kutokana na uingizwaji wa magari yasiyo na namba za Tanzania, haijaeleweka kama kumekuwa na utaratibu upi wa ukusanyaji wa kodi.

Alishangazwa na hatua ya kampuni hiyo kupewa hadhi ya kidiplomasia, huku ikiwa imesajiliwa kama kampuni kwani kambi ya kampuni hiyo hulindwa na Jeshi la Polisi''

Tanzania itajengwa na watu wenye mtazamo kama wanaJF, naomba kuwasilisha hoja jamani.
 
Hili suala la Loliondo ni miongoni mwa mambo mengi tutakayoyaangalia upya mara baada ya UHURU. Tutarudisha kila kilichoporwa kwa wana wa nchi, na wote waliohusika katika uuzaji huu haramu wa nchi yetu na uporaji uliokithiri wa raslimali zetu tutawapeleka gerezani! Baada ya hapo tutaweka utaratibu mzuri wa wana wa nchi hii kunufaika na utajiri wao waliojaliwa na Mwenyezi Mungu.
 
Vita sio kitu cha mchezo ndugu yangu, wala usiombee. Najua hasira ulizonazo kutokana na ubabaishaji mwingi ndani ya serikali. Lakini lazima utambue kwamba haya yote yanafanyika kutokana na serikali yetu kukumbatia ufisadi na kusahau maslahi ya wananchi wake. Humu kwenye JF tumekuwa tukijadili namna ya kuubadilisha mfumo wa utawala, ili tuondokane na ufisadi, lakini sio kwa njia ya vita. Tunapambana hivi sasa kujenga hoja kwa wananchi kwamba lazima tuwachague watu waadilifu watuongoze kuelekea kwenye mafanikio. Jukumu hilo ni letu sote.
 
Back
Top Bottom