Loliondo kwachafuka, watu wauana na kuchinjana kama kuku!

mhh usikute hawa jamaa wauza unga wa makanisa yetu ya kiroho wamekosa mwelekeo wameamua kutishia watu wasije huko kwa babu maana sadaka zimepungua sana imani za watu zimeamia kwenye kikombe
 
Sidhani kama Mwarabu anahusika, yeye Loliondo kaichukulia kama sehemu ya kuficha uovu kulingana na maadili ya dini yake. Hana shida kimsingi.

Wewe umeleta mada nzuri ya kutujuza yanayoendelea Loliondo mara ghafla umewarukia kuonesha mfano Waarabu na umeona haitoshi unaingiza na dini yao sasa? Wamekufanya nini Waarabu na dini yao? Na maovu yepi ya dini yao wanayokuja kuyaficha Loliondo?
 
Wewe umeleta mada nzuri ya kutujuza yanayoendelea Loliondo mara ghafla umewarukia kuonesha mfano Waarabu na umeona haitoshi unaingiza na dini yao sasa? Wamekufanya nini Waarabu na dini yao? Na maovu yepi ya dini yao wanayokuja kuyaficha Loliondo?
Huwa sipendi kusema uongo FF ukitaka niPM nitakujuza mwarabu anachokuja kukifanya Loliondo lakini si uwindani kama inavyofahamika.
 
Babu si mtume wa Loliondo hawezi kuwaombea mji ukatulia? au na yeye kamba zake zimeisha
 
WanaJF,
Poleni na shughuli za ujenzi wa Taifa letu.
Habari ambazo nimezipata sasa hivi kutoka Loliondo kuwa hali ya mji huo imechafuka baada ya watu zaidi ya saba kuuwawa katika muda mfupi usiozidi mwezi mmoja! Vyanzo vya vifo hivyo bado havijawa wazi mpaka saizi! Mwanzo wa matukio ulianza hivi;
  • Katikati ya mwezi wa tisa jamaa mmoja alipigwa risasi karibu kabisa na guest moja maarufu kama Blue Park. Ukiwa unaelekea guest hiyo ya Blue Park kuna kajiduka ka huyo marehemu ambapo alipigwa shaba na kufa hapo hapo! Kabla ya kumuua marehemu huyo, kulikuwa na mtu mwingine ambaye alikuwa na marehemu lakini yeye hao jamaa hawakumdhuru wala kuiba kitu chochote kile. Tukio hili lilitokea Loliondo mjini.
  • Kabla ya tukio hilo halijakaa sawa, akapigwa tena shaba mwl wa Shule ya Msingi ambaye yeye alinusurika kifo baada ya kukikimbizwa hospitali ya Wasso kwa matibabu. Katika tukio hilo, mwalimu huyo alipigwa shaba maeneo ya tumboni ambapo risasi hiyo ilimjeruhi (kuparaza) na mguuni. Tukio hili lilitokea Wasso nje kidogo ya mji wa Loliondo kama 9Kms hivi, hali kadhalika matuhumiwa hao hawakuchukua kitu chochote na kutokomea kusikojulikana.
  • Watu wakiwa wanajiuliza kunani, usiku wa tarehe 10.10.2011 vijana wawili tena walipigwa shaba na kufa hapo hapo! Tukio hili limetokea mji wa Waso.
  • Usiku wa kuamkia leo ndiyo umeshuhudia mauaji ya kutisha baada ya watu watano kuuawa kwa kupigwa risasi na wengine kunjinjwa na kuacha majeruhi kadhaa ambao wapo hospitali ya Wasso wakiendelea na matibabu. Juhudi za kuwahoji majeruhi ziligonga mwamba baada ya kila walipohojiwa kushindwa kueleza chochote zaidi ya kulia tu, inatia huruma sana jamani!
Mpaka sasa bado haijaeleweka nini chanzo cha mauaji hayo, maana awali kwa yule kijana wa karibu na Blue Park pamoja, Mwl wa shule ya msingi na hao vijana wawili ilidhaniwa labda ni biashara/ dili ambazo walidhulumiana! Lakini hili tukio la usiku wa kuamkia leo linazidi kuongeza mkanganyiko wa chanzo.
Kutokana na hali jinsi ilivyo, watu saizi katika mji wa Wasso na Loliondo imejaa mashaka sana, yaani hofu tupu ya kuogopa kuuwawa!
Pamoja na hayo, vyombo vya ulinzi na usalama bado havijatoa tamko rasmi licha ya jitahada kubwa zinazoendelea za kutafuta wahusika wa matukio hayo yote.
Nawakalisha kwa masikitiko makubwa.
Nitazidi kuwajuza kwa kadri chanzo kitavyokuwa kinanyetisha toka Loliondo.


Wana JF,

Kuna jambo mmoja huwa lanishangaza sana katika Jeshi letu la Police je huwa ni uzembe wa kufatilia matukio au ni kuwa hawana knowledge ya kutathimini matukio na jinsi ya kuyakabili au ni kukosa vitendea kazi?

Swala la ulinzi jamii ndio kabisa police wakishapewa taarifa kurespond kwao huwa kwa kutegemea mambo mawili kuchelewa eneo la tukio au kuwahi eneo la tukio na kama wakiwahi basi mjue ni mkono wa mkuu umeshinikiza kuwahi na kama wakichelewa hiyo issue iliyo tokea wao wanaipuuzia na kuwaacha wananchi wanamalizana na ni matukio mengi ya namna hiyo hutokea na kuwafanya wananchi kuhisi kuwa police walihusika katika hilo tukio walilo chelewa.

Kinacho wakela wananchi ni pale tu kukiwa na maandamano utasikia kauli kutoka juuu zaidi ndani ya jeshi la police IGP mwenyewe ooh maandamano hayato kuwepo sababu za ki intellijensia khaaaa ebhooooo wewe IGP hiyo intellijensia umeipataje kuwa kuna matukio ya hatari yatakuwepo kwenye maandamano wakati nyie mko kulinda raia na mumejipanga kuhakikisha njia zote watakazo pita waandamanaji ziko salama na zimelindwa na ulinzi wa kutosha? inashangaza sana

Ukirudi upande mwingine sasa ambao wao police ndio wahusika wakuu na ni wajibu wao hilo neno intellijensia huwa halipatikaniki katika matukio kama hayo ya wizi wa siraha za moto au mauaji kama hayo ya waso huko loliondo wataka kuniambia police upelelezi wao ni wa maandamano tuu lakini huko uraiani katika matukio hawafanya hizo intellijensia zao na hata baada ya tukio la mauaji au wizi wanapotezea hiyo intellijensia yao au??

My Take;

IGP anatakiwa kuamka na kuja proactive procedures kwa wananchi na sio kuwa na siasa za kujitetea au kulinda jeshi lake na kama kuna mapungufu ni swala liko wasi kukubali mapungufu na kuya sawazisha kabisa na wananchi kweli watakupa support ila matukia yakitokea mkiambiwa nyie ni kukimbilia kiji defend kwanza.

Na tatizo kubwa linalo yumbisha vyombo vyetu vya dolla ni si ha sa hizi za viongozi watu wanasahau uwajibikaji wao katika Taifa wanawatumikia viongozi wa serikali na kutanguliza siasa mbele, Jambo ambalo lina shusha hadhi kwa vyombo vya ulinzi na usalama.

Nashangaa tunapo kimbiza report ya haki za bianadamu na kujidai ati nasi tua Siasa Safi Viongozi bora ili hali ni kinyume chake siasa chafu zikiongozwa na viongozi waliopo madarakani viongozi legelege wasio fuata sheria wala katiba iliyo ya nchi kwa kuijinufaisha wao na kuwa nyonya wananchi. Nadhani kuna haja Hizi report za haki za bianadamu zikishafika huko UN irudishwe yuipigi kura kama yaliyo pelekwa ni kweli au ni viongozi kujisafisha wao kwenye makaratasi.

Poleni sana wananchi wa waso kwa matukio ya kutisha
 
Babu si mtume wa Loliondo hawezi kuwaombea mji ukatulia? au na yeye kamba zake zimeisha
Kwa suala la babu na kikombe chake kwa kweli sijui imeishia wapi, ni imani yangu wagonjwa bado ni wengi lakini hali si kivile kama hapo awali.
 


Hebu tujuze nasi tujue kama sio uwindaji ni nini? au kunauchimbaji pia nini?
Mwarabu wa Loliondo hana shida ya pesa, yeye ile ni sehemu yake ya kupumzikia tu. Ukifika muda wa kuja huku anakuja yupo full equipped basi ni kula raha kwa kwenda mbele.
 
Mwarabu wa Loliondo hana shida ya pesa, yeye ile ni sehemu yake ya kupumzikia tu. Ukifika muda wa kuja huku anakuja yupo full equipped basi ni kula raha kwa kwenda mbele.

Ndio hiyo raha watu wanasema huja na vyombo vya kuwastarehesha toka Italy,France nini ???? wana kula Bata kwa kwenda mbeleeeee
 
Polisi bado wanaendelea na uchunguzi, na siyo polisi bali kamati nzima ya ulinzi na usalama inahaha kutafuta chanzo sahihi cha mauaji hayo na kikubwa zaidi ni kuwakikishia raia kuwa hali imerejea kama awali.
..Hivi huko si ndiko kuna wakati walikuwa wanatawaliwa na wasomali kutoka Kenya na polisi walishindwa kupambana na hao wasomali hadi JWTZ wakapelekwa ndio kukawa na amani? Yaelekea watu wa huko kulipuana shaba ndio zao...
 
Ndiyo hivyo ndugu yangu watu tunafikiria waarabu pekee ndiyo wanaweza kutenganisha vichwa na viwili wili kumbe hata bongo tumefikia huko!

Tena wabongo mumekwenda mbali zaidi. Kwani wao wanaweza kumchuna ngozi mtu huku akiwa hai na kukata viungo vya Albino pasi na shaka wala uoga wa kuuwa vikongwe.
 
UPDATES:
Taarifa zisizo na mashaka zinasema chanzo cha ugomvi ulipelekea mauaji ni MGOGORO WA ARDHI BAINA YA WASONJO NA WAMASAI. Wamasai wa kijiji cha Magaiduru waliwaua vijana wawili wa kisonjo kwa kutumia bunduki aina ya SMG. Wasonjo nao wa kijiji cha Mgongo Mageri walikwenda kulipiza kisasi cha kuuwawa ndugu zao. Vijiji hivi vya Magaiduru na Mgongo Mageri ni vijiji vilivyo karibu. Katika zoezi hilo la kulipa kisasi watu watano waliuawa ambao ni vibarua wawili (Wairaq), Mgeni mmoja (Mmasai), Mama mmoja na mtoto mmoja ambao wote ni wakazi wa kijiji cha Magaiduru. Zoezi la kusuluhisha mgogoro huo wa ardhi linaendelea kwa viongozi wa serikali toka Arusha kuelekea Loliondo na wale waliopo Loliondo lakini suluhu bado haijapatika.
Kuhusu wapi wanapozipata hizo silaha, taarifa zinaweka wazi kuwa silaha zinanunuliwa toka Kenya. Kutoka Loliondo hadi mpakani na Kenya haizidi 100kms na barabara ipo ambayo inapitika bila shida karibu kipindi chote cha mwaka.

Kwa wale yule kijana niliyesema ameuwa karibu na Blue Park guest vyanzo vinatema kuwa ni mambo ya kibiashara ambapo inaonekana walidhulumiana


WanaJF,
Poleni na shughuli za ujenzi wa Taifa letu.
Habari ambazo nimezipata sasa hivi kutoka Loliondo kuwa hali ya mji huo imechafuka baada ya watu zaidi ya saba kuuwawa katika muda mfupi usiozidi mwezi mmoja! Vyanzo vya vifo hivyo bado havijawa wazi mpaka saizi! Mwanzo wa matukio ulianza hivi;

  • Katikati ya mwezi wa tisa jamaa mmoja alipigwa risasi karibu kabisa na guest moja maarufu kama Blue Park. Ukiwa unaelekea guest hiyo ya Blue Park kuna kajiduka ka huyo marehemu ambapo alipigwa shaba na kufa hapo hapo! Kabla ya kumuua marehemu huyo, kulikuwa na mtu mwingine ambaye alikuwa na marehemu lakini yeye hao jamaa hawakumdhuru wala kuiba kitu chochote kile. Tukio hili lilitokea Loliondo mjini.
  • Kabla ya tukio hilo halijakaa sawa, akapigwa tena shaba mwl wa Shule ya Msingi ambaye yeye alinusurika kifo baada ya kukikimbizwa hospitali ya Wasso kwa matibabu. Katika tukio hilo, mwalimu huyo alipigwa shaba maeneo ya tumboni ambapo risasi hiyo ilimjeruhi (kuparaza) na mguuni. Tukio hili lilitokea Wasso nje kidogo ya mji wa Loliondo kama 9Kms hivi, hali kadhalika matuhumiwa hao hawakuchukua kitu chochote na kutokomea kusikojulikana.
  • Watu wakiwa wanajiuliza kunani, usiku wa tarehe 10.10.2011 vijana wawili tena walipigwa shaba na kufa hapo hapo! Tukio hili limetokea mji wa Waso.
  • Usiku wa kuamkia leo ndiyo umeshuhudia mauaji ya kutisha baada ya watu watano kuuawa kwa kupigwa risasi na wengine kunjinjwa na kuacha majeruhi kadhaa ambao wapo hospitali ya Wasso wakiendelea na matibabu. Juhudi za kuwahoji majeruhi ziligonga mwamba baada ya kila walipohojiwa kushindwa kueleza chochote zaidi ya kulia tu, inatia huruma sana jamani!
Mpaka sasa bado haijaeleweka nini chanzo cha mauaji hayo, maana awali kwa yule kijana wa karibu na Blue Park pamoja, Mwl wa shule ya msingi na hao vijana wawili ilidhaniwa labda ni biashara/ dili ambazo walidhulumiana! Lakini hili tukio la usiku wa kuamkia leo linazidi kuongeza mkanganyiko wa chanzo.
Kutokana na hali jinsi ilivyo, watu saizi katika mji wa Wasso na Loliondo imejaa mashaka sana, yaani hofu tupu ya kuogopa kuuwawa!
Pamoja na hayo, vyombo vya ulinzi na usalama bado havijatoa tamko rasmi licha ya jitahada kubwa zinazoendelea za kutafuta wahusika wa matukio hayo yote.
Nawakalisha kwa masikitiko makubwa.

Nitazidi kuwajuza kwa kadri chanzo kitavyokuwa kinanyetisha toka Loliondo.

Mzee wa Rula, mi sidhani kama kuna juhudi zozote za kusuluhisha huo mgogoro maana ni siri iliyowazi kuwa hao jamaa wamekuwa katika tension kubwa kwa kiindi kirefu huku kila upande ukijiandaa kwa mapigano (soma post yangu ya kwanza) Habari kuwa wamekuwa wakinunua silaha sio siri wwala haihitaji uchunguzi nenda baa yeyote pale wasso au loliondo ukiuiliza utaambiwa hizi taarifa sasa sembuse wazee wa intelijensia kushindwa kujua kuna vita/mgogoro unafukuta wachukua hatua za kuzuia usitokee...
 
Mbona mauaji kila pembe ya nchi? Ni nani anawaua wakazi wa Loliondo na kwa ajili ya faida gani?
 
Back
Top Bottom