Wana jf, nilikua nyumbani kwa siku 5 zilizopita kwa pasaka. Nilijumuika na ndugu na rafiki zangu kuanzia Jumamosi hadi jumatatu. Haya ndio nilioyaona.Jamaa zangu wa karibu ni ma dealers wa madini ya Tanzanite hivyo mkwanja sio haba. siku za nyuma walikua wanajihisi hisi na kaugonjwa haka kakali basi miezi 2 iliyopita walikuwa wa kwanza kwanza kutinga Samunge na kupata ki cup. Nakikubali kikombe sababu wazazi wangu wamepona moyo na miguu.
Jumamosi tukawa club AQ tulikuwa 6 hivi basi staili ya kuchukua totoz ni 'aah mi nimeshapata kikombe bwana so anti usijali sina ngoma, demu nae aah hata mimi nimetoka wiki iliyopita kwa hiyo niko safi' Wakaanza kusimuliana ya Loliondo .muda ukafika wakaondoka jamaa zangu 3 kwa staili hiyo na kilevi tena. nadhani wote hawakutumia tena kale kakinga ketu. mi mgeni nikalala doro.
Jumapili tukawa pale Triple A mambo kama ya jana yake ila mademu wengine kabisa. Mh kengele zikavuma kichwani kwangu. nikajua ndio kawaida ya baadhi ya vijana wa A town.
wajameni kikombe hakitolewi mara 2 na haina maana kurudia maisha yale ya nyuma. Baada ya kikombe TUBADILIKE. Bado sijaenda kwa kikombe ila siku ikifika ntaaga wanajf.
Jumamosi tukawa club AQ tulikuwa 6 hivi basi staili ya kuchukua totoz ni 'aah mi nimeshapata kikombe bwana so anti usijali sina ngoma, demu nae aah hata mimi nimetoka wiki iliyopita kwa hiyo niko safi' Wakaanza kusimuliana ya Loliondo .muda ukafika wakaondoka jamaa zangu 3 kwa staili hiyo na kilevi tena. nadhani wote hawakutumia tena kale kakinga ketu. mi mgeni nikalala doro.
Jumapili tukawa pale Triple A mambo kama ya jana yake ila mademu wengine kabisa. Mh kengele zikavuma kichwani kwangu. nikajua ndio kawaida ya baadhi ya vijana wa A town.
wajameni kikombe hakitolewi mara 2 na haina maana kurudia maisha yale ya nyuma. Baada ya kikombe TUBADILIKE. Bado sijaenda kwa kikombe ila siku ikifika ntaaga wanajf.