Logical reasoning iwe silaha kuyaamini ya wazungu

Logical reasoning iwe silaha kuyaamini ya wazungu

padlock

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2013
Posts
329
Reaction score
509
Wakati tuko shule ya Tulifundishwa historia ya vitu mbali mbali hasa kuhusu sisi waafrika na mambo yetu, mojawapo ya hoja au misingi ya somo hili ni kuelezea ugunduzi wa vitu mbali mbali na wazungu vilivyomo uku kwetu barani Afrika

Msingi huu ulipelekea somo hili kutuelezea mambo meengi ya ugunduzi wa wazungu kutambua maliasili na rasilimali zetu, lakini swali ni Je hayo yote yalikuwa kweli???

Tuanze kwa kuangalia mzungu wa kwanza kuuona mlima Kilmanjaro kulingana na msingi wa somo alikuwa John Rebman lakini je ni nani alieweza kujua kuwa huyu ni John Rebman?? na ni kweli hakukuwa na mwingine aliewahi kuuona kabla yake?? na nn kilitumika kupeleka huyu kutamkwa wa kwanza?

Si hayo tu ni mengi sana yanahitaji LOGICAL REASONING KUAMINI WANACHOSEMA.
 
Mi mzungu ninayemuamini ni huyu aliyekitengeneza kitu na kinatumika(mfano Facebook,forums,whatsaap,taa,umeme,gari,ndege n.k) lkn hao sijui wa kwanza kuliona ziwa Victoria,ml Kilimanjaro nawaona wanatuzingua tu
Nalog off
 
Logic ( mantiki) ya ugunduzi huo ni kwamba kabla ya hao, wanaotajwa hakukuwa na mtu mwingine mwenye ngozi nyeupe aliyefanikiwa kufika mahali hapo na kuona kwa macho matupu na hata kunusa harufu ya pale panapotajwa, kisha akawapasha habari wenzake, wa huko kwao au ugenini. Kumbuka, watu hao walisaidiwa na wapagazi na walughalugha ambao ndiyo walikuwa wenyeji wa maeneo hayo.
 
Yaani mlima Kilimanjaro ulionwa na mzungu kabla ya muafrika mwenyewe wa pale Moshi?au unamaanisha wa kwanza kwa wazungu pekee?
 
Kuna haja ya kuandaa mitaala iendane na sisi,hata simulizi zetu zingine hazitufai kwa kipindi hiki mfn kiuchumi inatusaidia nini kukaririshana kwamba walitutesa wakati huuhuu tunashirikiana nao?tunazitesa fikra na hisia za watoto hivi vitabu vyingine viwekwe maktaba tu kama hadithi au vya ziada visiwe kiada
 
So *** the classes in school
*** John rebman and the fool
That said they found Mount Kilimanjaro
They've been lying to you.

Edited from Burna Boy's album Titled TWICE AS TALL..
SONG: Monsters You've made
 
Lugha sahihi ni Mzungu wa kwanza kuona mlima, ziwa. Sasa watu wetu walishindwa kuisema hiyo wakasema kuvumbua...
 
Back
Top Bottom