Ni kweli mkuu sijawahi kushabikia Yanga maisha yangu yote na sitakuja kushabikia lakini mimi sina wivu wa hivyo na wala sina ushabiki wa mihemuko penye ukweli tunasema hata jana kama ulifuatilia ule uzi wa Simba na Kagera baada ya kipindi cha kwanza nilisema Simba pamoja na kuongoza hawakucheza vizuri kwa hiyo sina upofu wa kishabiki, mnaweza kuwa bora kwa sababu mnafunga magoli na sasa mnaongoza ligi lakini ukitaka kujiridhisha kama ni bora kweli angalia kwenye timu tatu zinazofuatia mmechukua pointi ngapi?
Kwa sasa ukiniuliza kikosi imara kabisa kwenye ligi yetu nitakwambia Azam, Mbeya City sijawaona hata Coastal sijawaona hivyo siwezi kucomment, offcourse hata nyie ni bora kuliko sisi lakini kumbukeni mnawakilisha nchi kwenye ligi ya mabingwa kosa kosa zenu mwaka juzi ziliwacost dhidi ya Zamalek, mlistahili kushinda uwanja wa Taifa tena kwa magoli mengi, lakini kwa kukosa umakini mkaishia droo na ugenini wenzenu wakashinda na kutupwa nje ya mashindano round ya kwanza.
Acha kulinganisha na Chelsea wenzetu wanajua wanachokifanya na wachezaji wao ni first class wanaweza kucheza timu yoyote hapa duniani, wanapozuia waakuwa wanajua wanafanya nini na ndo maana wana nidhamu ya kukaba.
Ubingwa wa Kagame mara mbili mfululizo wakati Tenga akiwa m/kiti wa CECAFA sio wa kuringia sana, kumbuka mwaka ule kuingia robo fainali na nusu fainali penati zilivyokuwa zinarudiwa rudiwa, ile hali sio hali ya kawaida.
Pamoja na yote hayo nawapongeza kwa ushindi wa leo na kuongoza ligi.