About time Diamond akabidhiwe kwa management ya kimataifa au yenye upeo huo itakayompeleka mbele zaidi, kwasababu hao jamaa alionao ni wazi uwezo wao umefika mwisho, na wamejitahidi sana, so big-up kwao.
Diamond ni brand sasa, na ni Icon ya taifa, but he still conducts himself like a hoodrat he is, cuz he's surrounded by the likes. Jamaa anatakiwa kuwa na PR team itakayo-monitor chochote anachosema popote, kwa maslahi yake na ya taifa kwa ujumla. Cuz let's face it, you can change a wardrobe but not the man under the clothes. Hizi drama na vitu zake za zamani sio level yake kwa sasa, na zinamshushia heshima.
Jana Nigerians wameonyesha jinsi walivyo wamoja na wakomavu, D'Banj licha ya tofauti walizokuwa nazo na Don Jazzy, aliutambua mchango wake bado. Hawa jamaa wanaelekea sayari nyingine kimuziki kwa sababu wana umoja. Wasanii wakishaonyesha umoja, hata mashabiki wao wataungana pia. Tusipochukua hatua za haraka, muda si mrefu tutabaki kuwa watazamaji tu, kama kwenye michezo.