LIVE UPDATES: Mkutano wa CCM Morogoro

LIVE UPDATES: Mkutano wa CCM Morogoro

Wee unat... a nini?
Unawafahamu wazazi wangu? unajua maana ya neno masikini.
Usinifanye nipate ban hapa ..@?"3 sana wee
CCM mmeamua matusi yawe sera zenu kwa sababu mmekosa political tolerance.

Acheni hasira jibuni hoja chama chenu kimeshazama kwenye tope zito ili kujinasua mnahitaji akili na sio matusi mnayotukana bungeni, jukwaani na mitandaoni.

Sikutegema kama ccm ingekufa kirahisi na mapema namna hii.


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
matusi hayafai mkuu.bora utukane hivi

CCM imegeuka kuwa chama cha upinzani.
Hongereni ccm kwa kujiandaa vema kuwa wapinzani kabla ya 2015.

Kuweni wavumilivu msitumie 'F' words kwenye mijadala kama Mbunge wenu Serukamba.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Ujamaa na kujitegemea ni kauli mbiu ya TANU ambayo CCM imeendeleza kama sera yake kuu...
CHADEMA hakiamini katika ujamaa bali kinaamini katika mrengo wa kati...yaani ujamaa na ubepari...kuwatumia mabepari kujenga uchumi imara kuwainua maskini kuwa katika tabaka la kati bila kumuumiza mtu....
Hii ni sera ambayo inatumiwa na mataifa makubwa yaliyokuwa yakiamini katika ujamaa ambao umekufa..
Kwa hiyo mkuu unataka kuniambia sera ya CHADEMA ni ujamaa na ubepari?

Kabla hatujaenda mbali, nikuulize tena, ARE YOU SURE?
 
Mimi huwa ninajiuliza, hivi CCM wanapoitisha mikutano kama hiyo wanawaambia nini wananchi? Maana tangu watuahidi maisha bora kwa kila mtanzania mwaka 2005, hali yetu ya maisha imekuwa mbaya kuliko ya awali, sasa wakija kwa wananchi wanasema nini?

Wanawapa sababu za maisha kuwa magumu zaidi, wanawaambia wavumilie hali inarekebishwa au wanawaambia CHADEMA wamekwamisha utekelezaji wa sera za CCM? Na wananchi tuna nini cha kutufanya tuwaamini hawa watu ambao ndiyo chanzo cha umaskini wetu?

Kinana kaongea utumbo mtupu,toka mwanzo mpaka mwisho hotuba yake ni kuwaongelea CHADEMA tu.Magamba wamekosa kiongozi
 
Miongoni mwa wasanii waliokuwepo ni Diamond,Tmk wanume,Kinana,Nape na wasanii wengine kibao kwa kuwa ilkuwa hamna kiingilio watu walikuwepokuwepo japokuwa ni wa kuletwa na maloli.

Diamond juzi tu kwenye instagram alikuwa analalamika wasanii wanakuwa used kwenye kampeni wakati hailipi,namshangaa leo
 
CCM imegeuka kuwa chama cha upinzani.
Hongereni ccm kwa kujiandaa vema kuwa wapinzani kabla ya 2015.
Naona unajifurahisha
Kuweni wavumilivu msitumie 'F' words kwenye mijadala kama Mbunge wenu Serukamba.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
angalia hapa mkuu
 
Kinana kaongea utumbo mtupu,toka mwanzo mpaka mwisho hotuba yake ni kuwaongelea CHADEMA tu.Magamba wamekosa kiongozi
Sio kweli, amezungumzia matatizo ya wakulima wa miwa kiwanda cha kilombero na mtibwa, migogoro ya wakulima na wafugaji, miundombinu ya barabara inayojengwa mkoani morogoro kuunganisha na mikoa mingine, katiba mpya na amani ya nchi...mwishoni kabisa ndio amezungmzia chadema..sala haiwezi kukamilika bila kumlaani shetani
 
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka serikali pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), kufanya uchunguzi wa ufisadi wa kutisha wa zaidi ya Sh bilioni 1, uliofanywa na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, chini ya Mkurugenzi wake, Sara Linuma, ili wafikishwe katika vyombo vya sheria.


Fedha hizo zilitolewa na Serikali Kuu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hali iliyowafanya madiwani wa halmashauri hiyo kuandika barua kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ili amhamishe Mkurugenzi huyo na kuamuru fedha hizo zilirejeshwe kwa mujibu wa sheria.


Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Turiani, wilayani Mvomero juzi jioni, Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Nape Nnauye, alisema malalamiko ya wizi wa fedha hizo yamekuwa mengi na katu hayawezi kuachwa bila kuchukuliwa hatua zozote.


Nape alisema kuna baadhi ya watumishi wa Halmashauri nchini wamekuwa mchwa wa kutafuna fedha za umma ambazo ni mali ya walipa kodi ambao kila kukicha wamekuwa wakitegemea kupata neema ya maendeleo katika maeneo yao.


Awali Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Jonas Vanzeland, alisema kuwa uchunguzi wa awali ulifanywa na mkaguzi wa ndani wa halmashauri hiyo na Tume iliyoundwa Januari mwaka huu umebaini jumla ya Sh bilioni 1.42 zimeibwa katika akaunti za halmashauri kwa awamu tofauti katika tawi la benki ya NMB Mvomero.


Alisema uchunguzi huo ulionesha kuwa siku moja Idara ya Uhasibu ya


Halmashauri hiyo ilitoa zaidi ya awamu 20 fedha kwa kutumia vocha tofauti za kughushi na kuzipeleka kusikojulikana.


"Takwimu zinaonesha sehemu ya fedha hizo zililetwa katika Halmashauri ya Mvomero kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, lakini badala yake zote ziliishia mifukoni mwa wajanja wachache.


"Mchanganuo wa fedha zilizoibiwa na wajanja wachache, wakiongozwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ni Sh milioni 290 zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi wilayani Mvomero, Sh milioni 300 za miradi ya kilimo, Sh milioni 83 za ujenzi wa barabara, Sh milioni 72 za ujenzi wa Daraja la Kisala lililopo katika Kata ya Sungaji na Sh milioni 400 za kodi ya uvunaji wa miti aina ya mitiki iliyopo katika wilaya yetu hii," alisema.


Vanzeland alisema hata kikao chao cha Baraza la Madiwani wameazimia kwamba hawamtaki Mkurugenzi huyo na kwamba tayari walikwisha muandikia barua Waziri Mkuu Pinda kuhusu suala hilo.


---
via gazeti la MTANZANIA


Source: wavuti.com - wavuti
 
CCM inashinda 2015 kwa kishindo sana na hii inatokana na timu waliounda. CCM itashinda tena sana.

Bila kumsahau MLETA WATEJA bila yeye nadhani NAPE na KINANA wangekuwa wanaangaliana na MAGARI yao ya kifahari na Wanamlipa VIZURI haswa angalia picha yake CHINI...
5.+DIAMOND+AKITUMBUIZA+UWANJANI.jpg
 
Bila kumsahau MLETA WATEJA bila yeye nadhani NAPE na KINANA wangekuwa wanaangaliana na MAGARI yao ya kifahari na Wanamlipa VIZURI haswa angalia picha yake CHINI...
5.+DIAMOND+AKITUMBUIZA+UWANJANI.jpg

Mleta wataje na ye ameanza kuponda serikali ya sasa.
Kuna thread imeletwa hapa analalamika "Wanatumiwa tu " na hawanufaiki na
chochote.. ahadi waliahidiwa ni debe tupu ....
 
Mleta wataje na ye ameanza kuponda serikali ya sasa.
Kuna thread imeletwa hapa analalamika "Wanatumiwa tu " na hawanufaiki na
chochote.. ahadi waliahidiwa ni debe tupu ....

acha wakipate.vijana walivyo bado wanakuli kutumika na magamba yaliyofikisha nchi hii yenye maziwa na asari(kilakitu)hapa ilipo.shame onthem.
 
Back
Top Bottom