Live update: Simba SC vs Kagera Sugar

Live update: Simba SC vs Kagera Sugar

Mimi nadhani hizi reply zinazooneshwa kwenye tv iliyo ndani ya uwanja wa taifa, sisi hazitufai, kwani mashabiki bado hawajawa na uvumilivu wa kutosha pindi pale refa anapokosea, sana sana kwenye maamuzi ya penalti kama leo.
Ipo siku hizi replay zitatuletea balaa zaidi!
 
sasa wale vizabi zabina waliokuwa wanasema oooh Mbeya city wanavurugu..oh sijui wanywa viroba,sasa mmewaona wanywa viroba wa kweli?
 
sasa wale vizabi zabina waliokuwa wanasema oooh Mbeya city wanavurugu..oh sijui wanywa viroba,sasa mmewaona wanywa viroba wa kweli?

MCC ni tofauti, hupiga magari ya timu pinzani hata kabla ya mechi. SSC wamefanya vurugu baada ya kuchomekewa bao tata. Ni kweli wameonewa, hatua waliyochukua haikubaliki pia. Ni lini MCC walionewa zaidi ya kuwapiga wapinzani mapema ili kuwachanganya kisaikolojia.
 
MCC ni tofauti, hupiga magari ya timu pinzani hata kabla ya mechi. SSC wamefanya vurugu baada ya kuchomekewa bao tata. Ni kweli wameonewa, hatua waliyochukua haikubaliki pia. Ni lini MCC walionewa zaidi ya kuwapiga wapinzani mapema ili kuwachanganya kisaikolojia.

kweli simba na yanga mmevurugwa,mkifanya nyie sahihi ila wakifanya wengine makosa,sasa ndio ustaarabu gani wa kungoa viti uwanjani?tena inabd mpigwe tu..eeh nasema mpigwe tu maana mmezidi.
 
kweli simba na yanga mmevurugwa,mkifanya nyie sahihi ila wakifanya wengine makosa,sasa ndio ustaarabu gani wa kungoa viti uwanjani?tena inabd mpigwe tu..eeh nasema mpigwe tu maana mmezidi.

MCC acheni kupiga timu pinzani lakini kabla ya kuacha nipigieni basi la Simba ikiwa ni fidia ya viti vya U/Taifa, baada ya hapo muache kabisa hako ka mchezo, mmenielewa?
 
Mkuu Katavi sijatukana mie, inaudhi sana nchi maskini tunajiongezea gharama za kukarabati uwanja, mwamuzi kavurunda na bado yupo uwanjani kwa nini msimcharaze? Mnaong'oa viti kwa kosa gani? Tafakarini njia zenu.



Lakini simba wana nguvu sana wanastahili pongezi kwa kuweza kong'oa viti vilivyofungwa kwa bolt.
 
Last edited by a moderator:
tambwe ndo kafunga , kagera wamesawazisha kwa penati dakika ya 90 +4. Baada ya hapo mashabiki wa simba wakaanza kungoa viti baada ya tv kuonyesha replay ambayo inaonyesha madhambi yalifanyika nje ya 18. Hata hivyo ffu walifanya kazi yao ipasavyo.
Baadhi ya mashabiki wa Simba wanaamini ilikuwa ni penalti, lakini mwamuzi alipaswa kuimezea kwa sababu ilitokea katika dakika za mwishoni. Swala langu kwao ni iwapo mzee wa miaka 100 anapoua kwa kukusudia, ndio asihukimiwe kifo?
Baadhi yao wanaamini madhambi yalifanyika nje ya eneo la penalti. Swala langu kwao ni iwapo wana habari ya goli hewa (ghost goal) lililoiwezesha Bayern Leverkusen kuishinda Hoffeinhem 2-1 kwenye Bundesliga wiki iliyopita. Ilithibitishwa pasi shaka yoyote kwamba mpira ulipitia kwenye tobo la wavu wa pembeni. Na bado likatosha kuipa ushindi Leverkusen. Seuze faulo ya kweli (hata kama ni nje kweli ya 18) tena iliyolazimisha sare tu?

hakuna sababu yoyote itayotosha kuhalalisha upuuzi uliofanywa na mashabiki kwenye Uwanja wa Taifa leo.
 
Back
Top Bottom