Freeland utabiri wako kiboko. Nilidhan unatania kumbe kweli yametimia. Ndala wanabid tu wapande boat kurudi kwa Mzizima pale Twiga street kwenye matete yale ya Bonde la Mto Msimbazi aka Jangwani. Poleni sana watani. Muliambiwa kuwa mulikuwa kundi la vibonde mukabisha! Yuko wapi Jerry Muro afisa habari wa Yanga maana nae ni kama yule waziri wa habari enzi za utawala wa hayati.Saddam Husein! Kwa propaganda anatisha. JERRY anakuambia kwa sasa habari ya Mujini Goli 4-0 kila.mechi. Leo wameshindwa hata goli moja. Poleni Watani, leo utasikia lugha za kujifariji nyingi tu. Wazee wa media hawa!
Mmefungwa kwa taabu! Daah, kumbe you planned to lose! Kwa maana hiyo mechi nyingine huwa mnafungwa kwa urahisi!Tumejitahidi sanaa, tumefungwa kwa taabu sana;
umeshika tama sawa vile umefungwa wewe?
tumelala unono
tumelala unono
Ni kweli kabisa. Si bado kaswekwa ndani. Labda ndio mganga wao yule. Sasa heshima itarudi maana walizidi sana hawa kwa kuzifunga zile timu za daraja la pili.
Ova
leo mjini kumetulia sijui kuna msiba..
Ahsante everlenk long time, toka world cup miss u.
nyie mna maneno kama mmemeza kanda za wahengaNi kweli mmelala unono maana Yanga ilikuwa tishio kwenu. Hata hivyo mvua huwa haikimbiwa itakupata tu, tutakutana kwenye ligi tumalizie hasira zetu kwenu, kwa kuanza tunaelekea Mbeya kufanya mauaji ya halaiki.
Tumefungwa tu, ni hali ya mchezo.
Mimi nilianza kuona dalili baada ya Polisi kuing'oa KCCA. I presume Simba au Mtibwa au wote wawili (w)atacheza mechi ya kutafuta mshindi wa 3. Siwatakii mabaya nataka mchue tahadhari maana Wazanzibar wamechoka kuwa kichwa cha mwendawazimu. Sasa hivi mnaonekana kama vile mmechukua kombe, mnashangilia tu badala ya kujiandaa a mechi. Kajiandaeni kesho mna mechi ngumu sana.
Huyo jamaa alilala lupango night moja tu, siku iliyofuata aliingia mtaani na alionekana akila nchi kama alivyonaswa na kamera za wadau, kong'oli hapa:
KOCHA WA YANGA NA MPISHI WA BAO LA COUTINHO JUZI - BIN ZUBEIRY
Ni kweli mmelala unono maana Yanga ilikuwa tishio kwenu. Hata hivyo mvua huwa haikimbiwa itakupata tu, tutakutana kwenye ligi tumalizie hasira zetu kwenu, kwa kuanza tunaelekea Mbeya kufanya mauaji ya halaiki.