Live: Mansour Himid , Dk Slaa na Hassan Moyo

Live: Mansour Himid , Dk Slaa na Hassan Moyo

Naomba ufafanuzi kidogo

.... Makosa ya Mansour ni

1 - kuisaliti ilani ya uchaguzi ya chama chake

2 - kushindwa kutekeleza kazi kwa ufasaha

3 - Kukiuka na kukaidi katiba ya chama chake


.... Hayo ndio yamefanya chama kimfute uanachama.

Kumbukumbu zinaonesha kuwa chama chake hakikuwa na ajenda ya KATIBA katika ilani yake. Na taarifa

rasmi ni kuwa MWENYEKITI ndiye aliyeanzisha mchakato wa katiba bila kupitia kikao chochote rasmi.

Tafsiri ya ili ni nini? Je si kukiuka katiba? Je si kusaliti ilani ya uchaguzi?

Miaka kadhaa iliyopita kuna wanachama wa chama tawala waliaanza mkakati wa kuanzisha chama chao

wakakwaa kisiki. Baadhi wa waasisi wa huo mkakati sasa ni watu wazito serikalini na chamani, mmoja

ni Waziri, mwingine ni mtendaji wa juu wa chama. Je huu haukuwa kukiuka katiba ya chama? Je huu si

usaliti wa ilani ya uchaguzi (tendo lao linamaanisha hawaikubali ilani iyo)??

Na mwisho, chama kilitoa ahadi kedekede 2005 na 2010, ushahidi upo wazi wa kushindwa kutekeleza

asilimia zaidi ya 60 ya ahadi hizo. Je kwa kigezo hiki, si kosa kwa uongozi mzima wa juu wa chama

maana umeshindwa kusimamia utekelezaji wa ilani? Je si kushindwa kutekeleza kazi kwa ufasaha??
 
Kutokana na hayo hoja za kumfukuza mwanachama Mansour zina mashiko?

The same ruling party, the same leadership has set enough precedence for the above

allegations not to hold against any of its current and future members unless reversed.
 
Naomba ufafanuzi kidogo

.... Makosa ya Mansour ni

1 - kuisaliti ilani ya uchaguzi ya chama chake

2 - kushindwa kutekeleza kazi kwa ufasaha

3 - Kukiuka na kukaidi katiba ya chama chake
hapo sioni kama ni kosa kubwa maana binadamu na akili zetu tunakua na ukuaji mzuri ni ule wa kuboresha mambo badala ya kurudi kinyume. Ndio maana wengi wetu tuliishi kwenye nyumba za nyasi na madongo hapo hapo kabla lakini baada ya exposure na maendeleo ya dunia yasiyotoa nafasi kwa mtu kubaki nje yake, tukaongeza bidii kujenga nyumba za tofali na bati, ninaamini huu haukuwa usaliti kwa mababu. Mengine labda....
 
History as a phenomena tends to recurr and is very conservative.

The world has watched so many individuals, organisations and businesses set the path to self

distruction. I believe we have seen every possible sign that the ruling party has set course to self

distruct and steaming ahead at full speed. It is now evident that this gigantic entity is

wobbling and tumbling and wont be long enough before it eventually self distruct as is hard for any

master to sustain this course for over two years.

The Mansour episode has just set the countdown............
 
Slaa na baraghasia.

...mbona mwenyekiti wa TLP Mrema anava "baraghasia" siku nyingi tu lakini hamjawai kupanua midomo yenu mkasema?...umbea kwa mwanamke ni sunna lakini kwa mwanaume ni zaidi ya unafki...jitambue ili uche kutumika...
 
Hivi Lile jambazi Sugu lililofanya Ushenzi Mkubwa na Mauwaji Bara hasa Tanga ambae ni mwanawe Hassan Moyo ambae kila akifungwa kwa mauaji ya kijambazi anaachiwa yupo ndani kwa mauaji ya mwisho?
 
Dr.Slaa, mambo ya Zanzibar yana muhusu nini wakati Tundu Lissu kupitia tamko la chama alisema Zanzibar siyo nchi.

anajadili rasimu kwa kuungana na wanzanibar kupendekeza serikali 3.
umechukia??
 
Yanayo ikumba Tanzania si bahati mbaya bali ni ushaidi wa wazi wa kukithiri kwa uozo na dalali ya

ulegelege wa ngazi mbalimbali za uongozi. Kuanzia suala la EPA, Meremeta, Kilimo Kwanza, Suti za

Movenpick, Waziri kuibiwa Moro, Suala la dawa za kulevya, Kifo cha Mwangosi, Mateso ya Ulimboka na

Kibanda, Kufungiwa magazeti, Hali tete ya Muungano, Madawa feki ya HIV, Kashfa za utoroshaji madini,

Kasha za meno ya tembo, zogo na Rwanda, Zogo na Malawi, Ukuaji deni la taifa, Serikali kukopa benki

binafsi, Gari za masafara wa Rais kuwekewa mafuta machafu, Bunge kuwa maigizo, Kodi ya laini za simu,

Wizi wa shaba na mizigo mingine bandarini, akaunti za Uswisi, Waziri mkuu kwenda kinyume na katiba na

haki za binadam, Ukwepaji kodi, mabom kulipuliwa kanisani na katika mikusanyiko n.k

Hivi ni baadhi ya viashiria ambavyo ama kwa kujua au kutokujua tumefumbia macho kwa ujumla
 
Mbaya wetu sote ni ccm, tupiganie tanganyika yetu, vile wazanzibar wapiganie zanzibar yao. Hapo ndio tutapata muungano wa maana.
 
Kinara wa kundi la kina Mansoor ni KARUME JR sasa mbona yeye hafukuzwi
 
Back
Top Bottom