Lita ya mafuta ya kula imefika Tsh elfu 10. Rais Samia ajulishwe na aingilie kati

We ni muongo Lita ya alizeti ni elfu 5 km unabisha njoo Pm uje na hela yako nikuletee mafuta acheni KUANDIKA habari za kusimuliwa
Korie lita 18 ni shilingi 90,000 hiyo alizeti ya lita elfu 5 iko wapi.

Vile wamesema tunawapigia kelele tukomae tu.
 
Yeah serious problem, mafuta yanapanda Bei Kila kukicha yaan wapishi wakina mama wanatumia sana daah sasa hvi kutatokea na effect ya Bei ya vyakula vinavyo tumia mafuta haswa mtaani!!
Ni kipi ambacho hakijapanda bei ?
 
Umpigie kura usimpigie kura bado atatangazwa kuwa Rais tu, kura kuamua nani awe kiongozi mkuu wa nchi ni mpaka kuwe na "constitutional reform" ambayo pia alisema anajenga kwanza nchi...

Option ni
1. Kuidai katiba mpya kwa useriaz kabisa mpaka kura iwe na uwezo wa kuamua kiongozi mkuu wa nchi

2. Tuendelee kutulia na kuvumilia maamuzi yao dhidi ya walio wengi
System ikimkubali inatosha , wengine mtaishia kubishana vijiweni tuu
 
Ndo maana mi nimeamua kujitengenezea mafuta ya kupikia locally: nanunua mashudu ya alizeti,kisha nayachemsha,napata mafuta.

Simple like that.Tabu ya nini?
 
Ni kipi ambacho hakijapanda bei ?
Ambavyo havijapanda Bei ni mazao ya vyakula tuna mshukuru mungu sana unga wa sembe bei nzuri, mchele bei nzuri na pia now days watu wanatumia gas katika kupika so life is simple( ila unatakiwa ufanye kazi sio simple kihvo)

Kwa hapo tunashukuru serikali ya awamu ya sita!!
 
Sundrop 5 litre ni 37000 Dar sasa anasema litre ni 5000 yy ananunua wapi?
Mkuu hiyo 5litre kwa 37,000 ni maeneo gani hapa Dar. Manake kwingine tunanunua kwa 28,000, wastani wa 5,600 kwa lita.
 
Mwambieni mama yenu mheshimiwa Rais kuwa lita moja ya mafuta ya kupikia ya Alizeti imefika elfu 10

Mwambieni nyama kilo ni hadi elfu 10 kwa sasa

Imagine mafuta ya alizeti lita imefika elfu 10 haya mafuta mengine ya mgando sijui makorie ndo lita 6000

Na hayo makorie wengine huwa hatugusi kabisa tuna allergy kali sana tukila tu tukilala tunaamka tukiwa hoi mijipu mwili nzima kama mtu ana tetekuwanga hadi wife nimemkataza asinunue hayo makorie maana navimbaga balaa

Nyama ndo haigusiki sasa sijui ambao hawatomudu nyama inakuaje au mwenye mzazi alojifungua anayehitaji nyama kila siku inakuaje

Kweli huu mfumuko ni balaa mafuta lita elfu 10 shikamoo Samia Suluhu Hassan unaupiga mwingi haswa tatizo letu wabongo ni wasahaulifu hadi 2025 watakua washasahau haya madhira na watakupa kura tena hii nchi ngumu doh
Kaziendelee
 
Back
Top Bottom