figganigga
Platinum Member
- Oct 17, 2010
- 26,691
- 59,193
Heshim kwenu wakuu,
Mbunge Tundu Lissu, amehoji Maswali Mawili;
1. Kama Rais Magufuli hawezi kusafiri nje kwa kuogopa wapigaji, maana yake ni kwamba serikali yake yote, kuanzia Makamu wa Rais, ni wapiga dili.
2. Hivi Juliana Shonza na MaCCM wenzake wataweza kuja kutoa ushahidi mahakamani kwa mashtaka ambayo wamewafungulia wabunge wa CHADEMA leo?
WAKATI utawala wa Rais Dk. John Magufuli ukikaribia mwaka wa pili, huku akiwa amesafiri nje ya nchi mara chache ikilinganishwa na watangulizi wake, amevunja ukimya akisema kwamba anataka kwanza kumaliza wapiga dili ambao akiondoka wataweza kufanya mambo ya ajabu.
Amesema tangu aingie madarakani amepata mialiko zaidi ya 60 kwenda nje ya nchi, lakini ameikataa kwa sababu anataka kuishughulikia Tanzania kwanza.
Rais Magufuli alitoa kauli hiyo jana wakati akizindua mradi wa uboreshaji maji wa Sengerema akiwa katika ziara yake mkoani Mwanza.
“Ndiyo maana mimi sitembei sana, nikienda huko watafanya ya ajabu, ngoja nidili nao kwanza, lazima nihakikishe nasafisha kwanza.
“Leo (jana) nilitakiwa niwe Ethiopia kwenye mkutano wa AU, nimeona nimtume makamu wangu (Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan), ameniwakilisha na anafanya kazi vizuri, mimi ngoja nidili na ya watu kwa sababu nilichaguliwa kwa ajili ya Watanzania, safari nitaenda nikishastaafu.
“Ngoja nizifanyizie safari humu humu ndani kwani ningejuaje kama kuna Sh bilioni mbili za maji zimeibwa na kama wapo walioziiba waanze kuzirudisha.
“Kabla sijaondoka vyombo vyangu vitaanza kufuatilia kwa sababu nina Serikali iko hapa. Lazima mali za watu masikini ziende kuwanufaisha watu, ndio wajibu wangu na ndio haki yao,” alisema.
Wakati huo huo leo Viongozi wa Juu na Wabunge wa Chadema wamefurika nje ya jengo la Makakama Kuu Mjini Dodoma kusubiri kesi ya shambulio la mwili inayomkabili Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea.
Kubenea anashitakiwa kwa kosa la kumshambulia Mbunge wa Viti Maalum, Juliana Shonza.
Mbunge Tundu Lissu, amehoji Maswali Mawili;
1. Kama Rais Magufuli hawezi kusafiri nje kwa kuogopa wapigaji, maana yake ni kwamba serikali yake yote, kuanzia Makamu wa Rais, ni wapiga dili.
2. Hivi Juliana Shonza na MaCCM wenzake wataweza kuja kutoa ushahidi mahakamani kwa mashtaka ambayo wamewafungulia wabunge wa CHADEMA leo?
WAKATI utawala wa Rais Dk. John Magufuli ukikaribia mwaka wa pili, huku akiwa amesafiri nje ya nchi mara chache ikilinganishwa na watangulizi wake, amevunja ukimya akisema kwamba anataka kwanza kumaliza wapiga dili ambao akiondoka wataweza kufanya mambo ya ajabu.
Amesema tangu aingie madarakani amepata mialiko zaidi ya 60 kwenda nje ya nchi, lakini ameikataa kwa sababu anataka kuishughulikia Tanzania kwanza.
Rais Magufuli alitoa kauli hiyo jana wakati akizindua mradi wa uboreshaji maji wa Sengerema akiwa katika ziara yake mkoani Mwanza.
“Ndiyo maana mimi sitembei sana, nikienda huko watafanya ya ajabu, ngoja nidili nao kwanza, lazima nihakikishe nasafisha kwanza.
“Leo (jana) nilitakiwa niwe Ethiopia kwenye mkutano wa AU, nimeona nimtume makamu wangu (Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan), ameniwakilisha na anafanya kazi vizuri, mimi ngoja nidili na ya watu kwa sababu nilichaguliwa kwa ajili ya Watanzania, safari nitaenda nikishastaafu.
“Ngoja nizifanyizie safari humu humu ndani kwani ningejuaje kama kuna Sh bilioni mbili za maji zimeibwa na kama wapo walioziiba waanze kuzirudisha.
“Kabla sijaondoka vyombo vyangu vitaanza kufuatilia kwa sababu nina Serikali iko hapa. Lazima mali za watu masikini ziende kuwanufaisha watu, ndio wajibu wangu na ndio haki yao,” alisema.
Wakati huo huo leo Viongozi wa Juu na Wabunge wa Chadema wamefurika nje ya jengo la Makakama Kuu Mjini Dodoma kusubiri kesi ya shambulio la mwili inayomkabili Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea.
Kubenea anashitakiwa kwa kosa la kumshambulia Mbunge wa Viti Maalum, Juliana Shonza.