SAGAI GALGANO
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 43,703
- 60,777
Ujue wameshadhulumiana posho kama walivyotifuana hapa hii mijitu ya hovyo kuwahi kutokea dunianiNaona makada mnatifuana humu bila shaka hamjuani
Ujue wameshadhulumiana posho kama walivyotifuana hapa hii mijitu ya hovyo kuwahi kutokea dunianiNaona makada mnatifuana humu bila shaka hamjuani
Unataka kusema,waliomuminia risasi 36 ni hawa hawa wanaojifanya wapenzi wa Mungu?Mungu ndie ajuaye dhamira yake na visasi vilivyomsonga moyoni mwake hawezi pata hata kura mil 2,atajuta na atakuwa amepotea kisiasa.
Mshaurini vizuri hatokuja kuamini!
Umeanza kujisogeza kijana unaijua fursa!
Mkuu mtoa mada ni kada mwenzio ujueUmeandika kwa maumivu makubwa maana unajua unajidanganya wewe na huyo mungu wako wa maboksi
Nimeuza gunia la mpunga ndiyo nimepata fweedha sasa utanikoma hapa jamvini sina shidaaNaona ushawekewa bundle umerudi sasa!
Umenena vema,hii ndiyo Great Thinking tunayoihitaji hapa.Natamani hizi nondo kungekuwa na namna ya kuwafikishia Watanzania wote ili watambue uhalisia.Watawala wanatuongopea,wakosoaji wanakiona cha moto na washangiliaji wakipew tuzo.Umeandika mengi; mengine kwa mtazamo wangu naona umekosea, na mengine naona umepatia.
Mfano
Maendeleo jimboni kwake; hapa umenishangaza sana, kama mtu anaeonekana ana uelewa kama wako nae anaamini mbunge, tena wa upinzani ana jukumu la kupeleka maendeleo jimboni kwake!, Lissu hakusanyi kodi.
Kwa utawala huu wa Magufuli anavyochukia wapinzani; na hasa Lissu, ulitegemea hayo maendeleo jimboni kwa Lissu yapelekwe kweli?! mara ngapi tumemsikia Magufuli akisema hapeleki maendeleo kwa wapinzani? hapa naona umeyumba.
Nakubaliana nawe zaidi kwenye ajenda ya kiuchumi ya Lissu - hapa tuko pamoja; lakini hata kwenye suala la makundi kati ya Lissu na Mbowe kulikosababisha kufukuzwa Zitto, Kitila, na wenzake; hapa nakupinga kwa hoja nzuri tu: NINAZO, tatizo muda.
Mwisho kabisa, lazima ujue kazi ya Rais sio binafsi, Rais ana washauri, ana wasaidizi, ni jukumu lake kuwasikiliza hao washauri ili awe Rais bora, hivyo wote mnaom-judge Lissu kwamba atakuja kuwa kama Magufuli au sio presidential material hii hoja yenu haina msingi, hakuna binadamu aliekamilika asilimia 100.
Kinachomuharibia zaidi Magufuli ameshathibitisha kwa vitendo hataki ushauri wa mtu, anafanya anayoyapenda, hivyo mpaka Lissu nae atapopewa nafasi ndio tutahakikisha kama na yeye kweli ana tabia kama za Magufuli, na anayatenda kama Magufuli; na zaidi anaogopwa na wasaidizi wake kama Magufuli, na hakuna wala hapatatokea candidate yeyote wa nafasi ya Urais nchini ambae atakuwa hana fani yoyote ili tumuamini akipewa madaraka ata-perform kwa asilimia zote kwenye kila angle.
Kusikiliza wengine ndiko kunamfanya Rais awe bora, huwezi kumhukumu mtu kabla ya kumpa nafasi ya kutenda, hili ni sawa na wanaosema wapinzani hawastahili kupewa nchi watafanya kama CCM, How! wapeni nafasi muone mapungufu yao mthibitishe, kama Lissu nae anavyostahili kupewa hiyo nafasi, msihukumu kwa hisia.
Hakuna binadamu asie na Weakness na Strengths, wote tunazo; hizi ni sawa na tabia, kila mwanadamu ana tabia zake, huwezi kupingana na hili utakuwa against nature, hivyo hakuna sababu ya kumuogopa mtu just because of that.
Kama yupo wa kuipinga hoja yangu ajitokeze; ataje sifa za Rais kuitwa "presidential material" tuzijue, halafu tuone ni Rais yupi kati ya tuliowahi kuwa nao alikuwa na hizo sifa zote, na akazitekeleza baada ya kupewa majukumu.
Lazima mjue jambo moja, hata Rais kuwa mpole kupitiliza kama Kikwete, bado hakumfanyi kuwa Rais bora, zaidi ataacha wajanja wachezee rasilimali za taifa kama ilivyotokea awamu iliyopita, hivyo kumbe hata huyu nae alitakiwa kusikiliza washauri wake, inavyoonekana japo alikuwa mpole, but hakuwa anasikiliza kila alichoshauriwa na wasaidizi wake.
Majibu yako anayo yule viti maalumu!Bora urogwe kuliko kujiroga kisa msosi fanya kazi kwa bidii ipo siku mtaambiwa mgonoke kukinusuru chama
Kama mtu sio albino ukimuita albino hapo ni tatizo.Mkiitwa tu ma albino mnafungua kesi
Hatutaki walemavu ikulu sisi
Hoja uliyoileta inafikirisha zaidi.Sisi Watanzania kama wote kwa kutumia akili zetu,nguvu zetu na weledi wetu tukakubaliana kuwa tumekwama kwa sababu tunaongozwa kwa mifumo iliyokwama na kuanza upya tungeweza kusonga mbele kwa kasi kubwa.Ndiyo maana pamoja na raslimali lukuki bado nchi imekwama tunatumia nguvu nyingi bila matokeo chanya.Asante sana nami nakubaliana nawe kabisa...
Na hiki kinachoitwa huyu ni "presidential material" na huyu siyo "presidential material" ni cha kushangaza kidogo...
Na maana ya hawa ni kuwa "all presidential material personnels" wapo na lazima watokane na CCM tu. Ndiyo hoja yao....
Huu ni upogo mwingine was kimawazo na hapa ndipo lilipo tatizo letu na kukwama kwetu kama taifa kwa kuwa na watu wenye mawazo na dhana hizi potofu na ndiyo wenye dhamana ya utawala na mamlaka kisiasa.....
Tangu Uhuru 1961 hadi leo (kama miaka 60 sasa) Tanzania imeongozwa na "the so called presidential material personnels" wanne na huyu aliyepo ni watano na wote toka chama kilekile - CCM...!
What did they do? How much did they do to change Tanzania from worse to better?
Kwa maoni yangu wamefanya kidogo sana. Tunaogelea mlemle. Tunaenda mbele hatua kumi na kurudi nyuma hatua 15. Kila aliyekuja alifuta mengi ya mwenzake na kuanzisha yake mapya. Yaani tunaanza moja tena...!
Hawa ambao tunaambiwa walikuwa ni "presidential materials" ni watu wa chama kilekile lakini hawana "connectivity" na "continuity" ya kilichoanza na huyu kiendelezwe na huyu. Vipi kama wakiwa toka vyama tofauti?
Likely, kuna hatari ya mambo kuwa mabaya zaidi. Ndiyo maana inahitajika mabadiliko ya mfumo mpya wa kisheria na kikatiba kuweka utaratibu usiobadilika wa mambo haya yasiwe hivi yalivyo....!
Tanzania kwa umri wa miaka 60 sasa ya uwepo wake kama taifa huru, hatukupaswa kuwa hapa tulipo kimaendeleo, KIJAMII na KIUCHUMI....
Hii Tanzania ya leo kama tukiifananisha na binadamu kwa umri wake wa miaka 60 maana yake huyu MTU kwa sasa eti ndo tu anaanza kujifunza kutembea badala awe ameshaoa, kuzaa na kupata na wajukuu.....!!
Maana yake na tafsiri yake ni kuwa, huyu mtu - mtoto lazima atakuwa ana tatizo la kiafya linalopaswa kushughulikiwa na madaktari bingwa hasa. Tanzania ina tatizo hili. Inahitaji kiongozi atakayeliona na kulishughulikia..!!
Tatizo la nchi yetu siyo MTU kuwa "presidential material" ama kutokuwa.....
Tatizo ni mfumo wetu wa kikatiba na kisheria ndiyo kikwazo cha kupiga hatua za haraka za maendeleo yetu ya kijamii na kiuchumi....
Tukikubali na kukaa pamoja kama taifa kufanya reforms za nguvu za kisheria na kikatiba, tutaona Tanzania mpya ktk kipindi kifupi sana...
Tundu Lissu ni mwanasheria kitaaluma. Magufuli ni mwalimu wa somo la Chemistry kitaaluma...
Tumeona akitumia taaluma yake ya ualimu wa Kemia na matokeo yake kila mtu anaona....
Hebu tuone Tundu Lissu kama atatumia taaluma yake ya sheria kutuletea mabadiliko ya mifumo ya kiutawala kisheria na kikatiba kwa ajili kufungua milango ya maendeleo ya taifa hili ambalo ni kama limesimama, limedumaa.....
Kuandaika tu tabu vijana wa hungumalwa bhana mkipata pakulia tu mnakuwa kama misukuleKuna maswali kidogo ya kumuuliza ndugu lissu je katika yale mambo aliyokuwa anautangazia uma kila mara kwenye nyaraka zake yametekelezwa
1. Mara kadhaa alisikika hawezi kurudi nchi hii mpaka ahakikishiwe usalama na serikali ya nchi hii kwa kuwa walitaka kumuua na ameihirisha mara kibao na hata kusamehe ubunge,sasa ameamua kurudi kuja kugombea uraisi kama atapitishwa na chama chake.
Je amehakikishiwa usalama na serikali au wale aliokuwa hana imani nao wote wameondolewa pamoja na serikali ya awamu ya tano!
2.Katiba mpya imepatikana,alisikika mara kadhaa katiba mpya ndio suluhu je imeshapatikana mpaka imempa msukumo wa kugombea si hii ya zamani
3.Tume huru,je kumeundwa tume huru itakayo muhakikishia yeye kushinda mara kadhaa amenukuliwa akisema tume hii kwa upinzani ni ndoto je kuna nyingine inayomuhakikishia yeye kushinda?.
Najua atachelewa kujibu ila ruksa kwa wafuasi watiifu kumjibia hapa sabuni imetiwa nyingi ili povu nalo liwe jingi!
Kaka unataarifa na mswada was kuongeza Kinga zaidi kwa viongozi wa mihimili ya nchi??Kuna maswali kidogo ya kumuuliza ndugu lissu je katika yale mambo aliyokuwa anautangazia uma kila mara kwenye nyaraka zake yametekelezwa
1. Mara kadhaa alisikika hawezi kurudi nchi hii mpaka ahakikishiwe usalama na serikali ya nchi hii kwa kuwa walitaka kumuua na ameihirisha mara kibao na hata kusamehe ubunge,sasa ameamua kurudi kuja kugombea uraisi kama atapitishwa na chama chake.
Je amehakikishiwa usalama na serikali au wale aliokuwa hana imani nao wote wameondolewa pamoja na serikali ya awamu ya tano!
2.Katiba mpya imepatikana,alisikika mara kadhaa katiba mpya ndio suluhu je imeshapatikana mpaka imempa msukumo wa kugombea si hii ya zamani
3.Tume huru,je kumeundwa tume huru itakayo muhakikishia yeye kushinda mara kadhaa amenukuliwa akisema tume hii kwa upinzani ni ndoto je kuna nyingine inayomuhakikishia yeye kushinda?.
Najua atachelewa kujibu ila ruksa kwa wafuasi watiifu kumjibia hapa sabuni imetiwa nyingi ili povu nalo liwe jingi!
Lissu atakuua ndugu yangu. Achana nae😂😂😂
Maana si kwa kujaribu huku kupambana nae.
Katiba ya Tanzania ijazungumzia kuanzia 45 and abavo eti ila Haina mwishounaujua umri wa Slaa ?
Typing errors kibao halafu unataka tujadili thread yakoNi hakika na kweli ndani ya ccm akiondoka mgombea wao huyu 2025 hawana mtu wa kushindana na Tundu Lissu zaidi ya Dr Slaa.
Kama yupo mtajeni
Najua ntatajiwa mtu kam simbachawene wingiru nchemba au Dr kigwangara au nani sasa?
Jipangeni chadema mbaya wenu hiyooo 2025.