CHIPESI NAMISUKU
Member
- Oct 7, 2019
- 51
- 156
Niliwahi kuandika kuhusu nia ya Lissu kuutaka Urais wa Tanzania 2020. Huenda
chama chake kikampitisha 2020 badala ya Msigwa. Huyu ni msomi mzuri, ni mwanaharakati na ni mpinzani haswa haswa. Kwa sifa hizo anatosha sana kupeperusha bendera za Chadema Kwa sasa.
TWENDE SAWA
Huyu hakuwahi kushika nafasi kubwa za kiuongozi ila ni mwanasiasa mkubwa sana kwenye ukanda huu wa Africa Mashariki.. angelikuwa CCM huyu ni dhahiri angeliteuliwa kushika nafasi kubwa kabisa za Kiuongozi.
Ili nimzungumzie kwa haki kabisa Lissu nitatumia SWOT analysis ambayo itatupatia mambo makuu matatu (Strength,Weakness, na threats) hii ni kanuni ambayo haidanganyi na ambayo hutumiwa sana kupata uhalisia wa kitu kabla ya kuamua kufanya jambo. SWOT ya Lisu itaisaidia Jamii ambao ni walengwa wa huduma na nafasi anayoitaka Lisu kwa maana ya kwamba jamii itamfahamu kwa undani kabla ya kumchagua au kutikumchagua, itamsaidia yeye peke yake kujijua na itakisaidia Chama chake mwenyewe.
STRENGTH
1. Ni mzuri katika kujenga hoja, ukikutana naye kwenye hoja hasa zilizo na uelekeo wa fani yake ya Kisheria atakupoteza kabisa. Tuneshuhudia Bungeni mara nyingi akitoa somo la kutosha kuhusu kanuni za bunge na matumizi yake.
2. Akiwa kama wakili ameshinda kesi nyingi sana zake binafsi na zile alizosimamia watu wengine. Lisu ni mojawapo ya mawakili ambao wakisimamia kesi yako unakuwa na uhakika wa kushinda.
3. Ana jiamini sana katika kile anachokiamini, hata kama wengine wote watakataa kumuunga mkono yeye atapambana mwenyewe.
4. Ana ujasiri wa aina yake, Lissu sio mtu mwoga anaweza kupambana na yeyote yule bila kujali status kwenye jamii. Kwa hali ya kawaida ni vigumu kumshambulia Rais wa nchi lakini Lisu alijitoa kufanya hivyo. Ni watu wengi toka mataifa mbalimbali ambao hawawezi hiki kitu.
5. Hutimiza majukumu yake kisiasa sio kiutendaji ipasavyo, kuna wakati watu walimtilia Shaka kuwa Lisu si Mzalendo lakini kwa nature ya kazi yake ndani ya Upinzani alikuwa sahihi kutukosoa. Kilichotakiwa kufanywa kilikuwa ni kuchukua alichokuwa anakisema na kukifanyia kazi.
WEAKNESS
1. Kipingamizi cha kwanza cha Lissu hana agenda ya msingi ya Kiuchumi ya kumpeleka Ikulu zaidi ya kuwa mkosoaji mkubwa. Lisu anapaswa sasa kuanza kuonyesha Plan B zake katika maswala ya kitaifa yaani kama jambo limefeli yeye kama yeye angelifanyaje.
Naamini na ndivyo ilivyo kiongozi mzuri ni yule mwenye maono yake juu ya mambo flan yaani mawazo yake binafsi na sio ya kuandikiwa (Ilani) na ndio maana hata Rais wetu kuna saa anaweka ilani Pembeni na kunyoosha kwa namna anavyoamini yeye.
Lisu anatakiwa sasa atuonyeshe nje ya Ukosoaji wake nini plan na Dira yake kwa taifa hili.
2. Tundu Lissu ni mojawapo ya wanasiasa ambao wanapatwa na jazba kwa haraka hasa pale wanapotaka kuzidiwa na hoja.
Amekuwa akitamka maeneo ambayo mara nyingi huleta ukakasi masikioni mwa watu. Mara nyingi na kiutamaduni huwa tunasema Marehemu huwa hashambuliwi lakini Lisu bila kujali aliwahi kumshambulia Mwl Nyerere kipindi cha bunge la Katiba. Kwa heshima ya Mwl Nyerere Lisu hapa alikosea.... na anapaswa kujirekebisha.
3. Udhaifu mwingine wa Lisu ni makundi na urafiki usioeleweka alio nao na mwenyekiti wa chama chake. Kwa ufahamu wa sheria alionao Lissu alishindwa kuonyesha ni wapi kina Mwigamba, Kitila na Zitto walikosea hadi akasimamie kesi zao za kufukuzwa Chadema. Lisu ana Urafiki mkubwa sana na nwenyekiti na mwenyekiti amekuwa akimtumia Lisu kwa maslahi yake binafsi kuliko kukisaidia Chama.
Kama Lissu angelisimama katikati bila kutekwa na kundi la Mwenyekiti huenda angelinusuru kina Zitto kufukuzwa na angelikuwa amekisaidia sana chama kwa kuwabakisha watu muhimu sana kwenye chama. Lisu anaonekana kama anamwogopa sana Mwenyekiti na ushauri anaompa mwenyekiti ni lazma uwe na manufaa kwa Mwenyekiti.
OPPORTUNITY
1.Lisu bado ana fursa inayomzunguka na fursa kuu ni Tukio lililomtokea. Yaani tukio la kupigwa marisasi kwake ni fursa number moja. Kwa lugha ya malkia tunasena CONFLICT has two sides one At the best it Provides an opportunity to learn and a chance for innovation. And second At the worst it destroys individual, block up families and halts production Within organisation. Kwa tafsiri isiyo rasmi Mgongano na Misuguano INA pande mbili unaweza kutumia kujijenga na unaweza kukuharibia kabisa. Kama Lisu atachanga karata zake vizuri tukio like litamjenga zaidi na limeshaanza kumjenga.
2. Fursa ya pili ni kuwa watu wenye age yake kisiasa ndani ya Chama wameanza kupotea kwa Hoja. Watu kama Mnyika walikuwa wanaweza kumletea Upinzani ndani ya Chama ila siku hizi Mnyika ni Togwa.
THREATS
1. Jimboni kwake mambo si mazuri sana, yaani kwa umaarufu alionao haulingani na maendeleo aliyoyapeleka kwenye jimbo lake. Bado jimbo lake ni mojawapo ya majimbo maskini kimiundombinu na hata kipato cha mtu mmoja mmoja. Hii inatokana na yeye kutumika mno Kitaifa na kusahau jimboni kwake. "Kuna msemo unaosema Charity begins at Home" Lisu anatakiwa afanye mambo makubwa ambayo yatafanya kila mtu Jimboni kwake amkubali na hata Singida yote.
2.Kipingamizi kikubwa cha Lisu kwa sasa ni Afya yake. Lisu anatakiwa kwa sasa apiganie zaidi Afya yake kuliko kitu kingine kile.
3. Lisu yupo kama Mwigulu Ndani ya CCM kuwa haamini kuna mawazo Productive njee ya Chama chake. Yaani yeye anaamini kila siku CCM Inakosea hii si sifa ya kiongozi mzuri.
4. Hatari nyingine kwa Lisu ni kitendo chake cha kupenda kuattack Personalities badala ya kujikita kwenye hoja za nchi hii inatakiwa iende wapi. Tuliona alivyokuwa anamkosoa Personally Rais Magufuli badala ya kukosoa Sera na kuonyesha njia. Hata juzi juzi alikuwa anaongelea kitu personally sana kuhusu Kiingereza cha Rais. Mtu anayetaka urais anatakiwa kuwaza mbali sana sio vitu vidogo kama hivyo.
5. Ukaribu unaotaka kujitokeza kati yake na Zitto, who knows Zitto katumwa? Mara nyingine tu hata Upinzani wenyewe wamekuwa wakimtuhumu Zitto kuwa haaminiki. Zitto anaweza kutumia pia yeye Lissu kama ngazi yake ya kisiasa. Kwa sasa ACT wameshalisoma gape na hata Chadema wenyewe wameshaanza Minongono kuwa Zitto hapaswi kuunda ushirika na Lissu. Kwa sasa Brand ya Lisu ni Kubwa kuliko Zitto hivyo hatujui Hesabu za Zitto zipoje. Makachero wa Chadema wanapaswa kufuatilia hili kwa umakini mkubwa.
6.Mwisho kabisa hatari aliyonayo Lisu ni CCM, sio kwamba CCM imelala kutaka kuzima ndoto za Lisu kuendelea kushine kwenye Siasa. CCM bado ina Deal naye kwa umakini mkubwa kuhakikisha Lisu hachanui zaidi ya hapo Bali anazidi kufifia kisiasa.
chama chake kikampitisha 2020 badala ya Msigwa. Huyu ni msomi mzuri, ni mwanaharakati na ni mpinzani haswa haswa. Kwa sifa hizo anatosha sana kupeperusha bendera za Chadema Kwa sasa.
TWENDE SAWA
Huyu hakuwahi kushika nafasi kubwa za kiuongozi ila ni mwanasiasa mkubwa sana kwenye ukanda huu wa Africa Mashariki.. angelikuwa CCM huyu ni dhahiri angeliteuliwa kushika nafasi kubwa kabisa za Kiuongozi.
Ili nimzungumzie kwa haki kabisa Lissu nitatumia SWOT analysis ambayo itatupatia mambo makuu matatu (Strength,Weakness, na threats) hii ni kanuni ambayo haidanganyi na ambayo hutumiwa sana kupata uhalisia wa kitu kabla ya kuamua kufanya jambo. SWOT ya Lisu itaisaidia Jamii ambao ni walengwa wa huduma na nafasi anayoitaka Lisu kwa maana ya kwamba jamii itamfahamu kwa undani kabla ya kumchagua au kutikumchagua, itamsaidia yeye peke yake kujijua na itakisaidia Chama chake mwenyewe.
STRENGTH
1. Ni mzuri katika kujenga hoja, ukikutana naye kwenye hoja hasa zilizo na uelekeo wa fani yake ya Kisheria atakupoteza kabisa. Tuneshuhudia Bungeni mara nyingi akitoa somo la kutosha kuhusu kanuni za bunge na matumizi yake.
2. Akiwa kama wakili ameshinda kesi nyingi sana zake binafsi na zile alizosimamia watu wengine. Lisu ni mojawapo ya mawakili ambao wakisimamia kesi yako unakuwa na uhakika wa kushinda.
3. Ana jiamini sana katika kile anachokiamini, hata kama wengine wote watakataa kumuunga mkono yeye atapambana mwenyewe.
4. Ana ujasiri wa aina yake, Lissu sio mtu mwoga anaweza kupambana na yeyote yule bila kujali status kwenye jamii. Kwa hali ya kawaida ni vigumu kumshambulia Rais wa nchi lakini Lisu alijitoa kufanya hivyo. Ni watu wengi toka mataifa mbalimbali ambao hawawezi hiki kitu.
5. Hutimiza majukumu yake kisiasa sio kiutendaji ipasavyo, kuna wakati watu walimtilia Shaka kuwa Lisu si Mzalendo lakini kwa nature ya kazi yake ndani ya Upinzani alikuwa sahihi kutukosoa. Kilichotakiwa kufanywa kilikuwa ni kuchukua alichokuwa anakisema na kukifanyia kazi.
WEAKNESS
1. Kipingamizi cha kwanza cha Lissu hana agenda ya msingi ya Kiuchumi ya kumpeleka Ikulu zaidi ya kuwa mkosoaji mkubwa. Lisu anapaswa sasa kuanza kuonyesha Plan B zake katika maswala ya kitaifa yaani kama jambo limefeli yeye kama yeye angelifanyaje.
Naamini na ndivyo ilivyo kiongozi mzuri ni yule mwenye maono yake juu ya mambo flan yaani mawazo yake binafsi na sio ya kuandikiwa (Ilani) na ndio maana hata Rais wetu kuna saa anaweka ilani Pembeni na kunyoosha kwa namna anavyoamini yeye.
Lisu anatakiwa sasa atuonyeshe nje ya Ukosoaji wake nini plan na Dira yake kwa taifa hili.
2. Tundu Lissu ni mojawapo ya wanasiasa ambao wanapatwa na jazba kwa haraka hasa pale wanapotaka kuzidiwa na hoja.
Amekuwa akitamka maeneo ambayo mara nyingi huleta ukakasi masikioni mwa watu. Mara nyingi na kiutamaduni huwa tunasema Marehemu huwa hashambuliwi lakini Lisu bila kujali aliwahi kumshambulia Mwl Nyerere kipindi cha bunge la Katiba. Kwa heshima ya Mwl Nyerere Lisu hapa alikosea.... na anapaswa kujirekebisha.
3. Udhaifu mwingine wa Lisu ni makundi na urafiki usioeleweka alio nao na mwenyekiti wa chama chake. Kwa ufahamu wa sheria alionao Lissu alishindwa kuonyesha ni wapi kina Mwigamba, Kitila na Zitto walikosea hadi akasimamie kesi zao za kufukuzwa Chadema. Lisu ana Urafiki mkubwa sana na nwenyekiti na mwenyekiti amekuwa akimtumia Lisu kwa maslahi yake binafsi kuliko kukisaidia Chama.
Kama Lissu angelisimama katikati bila kutekwa na kundi la Mwenyekiti huenda angelinusuru kina Zitto kufukuzwa na angelikuwa amekisaidia sana chama kwa kuwabakisha watu muhimu sana kwenye chama. Lisu anaonekana kama anamwogopa sana Mwenyekiti na ushauri anaompa mwenyekiti ni lazma uwe na manufaa kwa Mwenyekiti.
OPPORTUNITY
1.Lisu bado ana fursa inayomzunguka na fursa kuu ni Tukio lililomtokea. Yaani tukio la kupigwa marisasi kwake ni fursa number moja. Kwa lugha ya malkia tunasena CONFLICT has two sides one At the best it Provides an opportunity to learn and a chance for innovation. And second At the worst it destroys individual, block up families and halts production Within organisation. Kwa tafsiri isiyo rasmi Mgongano na Misuguano INA pande mbili unaweza kutumia kujijenga na unaweza kukuharibia kabisa. Kama Lisu atachanga karata zake vizuri tukio like litamjenga zaidi na limeshaanza kumjenga.
2. Fursa ya pili ni kuwa watu wenye age yake kisiasa ndani ya Chama wameanza kupotea kwa Hoja. Watu kama Mnyika walikuwa wanaweza kumletea Upinzani ndani ya Chama ila siku hizi Mnyika ni Togwa.
THREATS
1. Jimboni kwake mambo si mazuri sana, yaani kwa umaarufu alionao haulingani na maendeleo aliyoyapeleka kwenye jimbo lake. Bado jimbo lake ni mojawapo ya majimbo maskini kimiundombinu na hata kipato cha mtu mmoja mmoja. Hii inatokana na yeye kutumika mno Kitaifa na kusahau jimboni kwake. "Kuna msemo unaosema Charity begins at Home" Lisu anatakiwa afanye mambo makubwa ambayo yatafanya kila mtu Jimboni kwake amkubali na hata Singida yote.
2.Kipingamizi kikubwa cha Lisu kwa sasa ni Afya yake. Lisu anatakiwa kwa sasa apiganie zaidi Afya yake kuliko kitu kingine kile.
3. Lisu yupo kama Mwigulu Ndani ya CCM kuwa haamini kuna mawazo Productive njee ya Chama chake. Yaani yeye anaamini kila siku CCM Inakosea hii si sifa ya kiongozi mzuri.
4. Hatari nyingine kwa Lisu ni kitendo chake cha kupenda kuattack Personalities badala ya kujikita kwenye hoja za nchi hii inatakiwa iende wapi. Tuliona alivyokuwa anamkosoa Personally Rais Magufuli badala ya kukosoa Sera na kuonyesha njia. Hata juzi juzi alikuwa anaongelea kitu personally sana kuhusu Kiingereza cha Rais. Mtu anayetaka urais anatakiwa kuwaza mbali sana sio vitu vidogo kama hivyo.
5. Ukaribu unaotaka kujitokeza kati yake na Zitto, who knows Zitto katumwa? Mara nyingine tu hata Upinzani wenyewe wamekuwa wakimtuhumu Zitto kuwa haaminiki. Zitto anaweza kutumia pia yeye Lissu kama ngazi yake ya kisiasa. Kwa sasa ACT wameshalisoma gape na hata Chadema wenyewe wameshaanza Minongono kuwa Zitto hapaswi kuunda ushirika na Lissu. Kwa sasa Brand ya Lisu ni Kubwa kuliko Zitto hivyo hatujui Hesabu za Zitto zipoje. Makachero wa Chadema wanapaswa kufuatilia hili kwa umakini mkubwa.
6.Mwisho kabisa hatari aliyonayo Lisu ni CCM, sio kwamba CCM imelala kutaka kuzima ndoto za Lisu kuendelea kushine kwenye Siasa. CCM bado ina Deal naye kwa umakini mkubwa kuhakikisha Lisu hachanui zaidi ya hapo Bali anazidi kufifia kisiasa.