Mkuu, uzi wako una title nzito sana, nilitarajia utawatendea Haki Tundu Lissu na Profesa Kabudi, kwa angalau kufanya kautafiti kidogo ili kujenga hoja kwamba kweli nani zaidi kati ya hao wawili. Naweza kusema yafuatayo kuhusu Tundu Lissu:
1) Enzi ya bunge la Spika Anne Makinda, Tundu Lissu ndiyo alikuwa "Rejea" ya mambo yote ya kisheria pale Bungeni, ambapo spika alilazimika kutafuta ushauri wa Andrew chenge baada ya kutoridhishwa na "performance" ya George Mcheche Masaju wakati huo akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. chenge aliishia kusema "alichosema Tundu Lissu ni sahihi". Tundu Lissu aliitendea haki nafasi hiyo, bila kujali kama yeye ni mtu wa upinzani. alikuwa anatema sheria tupu.
2) ukirudi nyuma kidogo, Tundu Lissu aliwasaidia wananchi zaidi ya 400 waliokuwa mahabusu au kufungwa wengine kwa kesi feki za mauaji, kosa lao kubwa ni "kupinga" uwekezaji kule Nyamongo. walizuliwa kesi za kuchomekea. Tundu Lissu alifanya kazi hiyo bila gharama yoyote kwa wananchi hao. aliishia kukamatwa na serikali ya Mkapa. Kitendo hiki kinamuweka katika level ya pekee, kama mpambanaji, mtetea haki za wanyonge, asiyetaka faida yake binafsi, na ambaye amepata mateso na kadhia nyingi kwa ajili tu ya kutoa huduma bure kwa wanyonge hao.
3) Mwanzoni, Spika Anne Makinda aliingia mkenge kwa kumtaka Tundu Lissu athibitishe madai yake kuhusu "Majaji feki". Thesis aliyoishusha Tundu Lissu, na ambayo ilipatikana pia mitandaoni, ilikuwa na majibu maridhawa pamoja na ushahidi wazi kabisa. huo ndio ukawa mwisho wa Spika kuwataka Wabunge wa upinzani "kuthibitisha" kauli, hasa watu kama Lema au Tundu Lissu.
Mwanzoni Profesa Kabudi alipotinga bungeni, niliandika uzi kuhusu mtanange wa Kabudi na Tundu Lissu, nikilinukuu gazeti la Raia Mwema ambalo lilikuwa linaangalia hali itakavyokuwa katika Bunge hili ambapo sasa watakuwepo manguli wa Sheria, wakiwemo Profesa Kabudi na Naibu Spika Tulia Ackson. Nilitabiri kwamba Tundu Lissu ataibuka kidedea, kutokana na hoja kadhaa. Mojawapo ni hizi zifuatazo:
1) wakati Tundu Lissu amepambana sana kwenye field, mara kadhaa mahakamani ama ajikitetea mwenyewe, au akitetea wananchi wengine, Profesa Kabudi yeye ni bingwa katika nadharia.
2) Tunaweza kusema kwamba Tundu Lissu ni zaidi pia kwa sababu yeye ameanza miaka mingi kushughulika na sheria katika uwanja wa siasa. Kabudi amekuwa zaidi sheria za darasani na za kisomi. Sasa hapa wamepambana mahali ambapo ni sheria katika siasa, ambalo ni eneo la kujidai la Tundu Lissu
3) kuna hoja moja kubwa sana. Tundu Lissu yupo upande wa walala hoi, anapigania haki, mwanaharakati, ambaye ana morali wa hali ya juu sana: HIGHLY MOTIVATED! Kabudi yeye analinda mfumo, wenye madhambi na madhaifu mengi. Mfumo unaonyanyasa raia. analazimika kutafuta namna ya kuokoa mfumo kandamizi, kuupaka rangi na kuupulizia pafyumu ili harufu ya mizoga ambayo inaandamana na serikali kandamizi, isisikike. Katika majibizano haya ya sasa, Kabudi anaremba remba ili kulinda mfumo, na anadiriki kuongea vitu ambavyo ni nje ya sheria, ili kulinda mfumo. hata kule Marekani, alitamka mambo ambayo siyo kweli. Tundu Lissu alimjibu na kumkosoa, Kabudi hakujibu. na sasa hivi pia Lissu anaonesha makosa ya kisheria anayofanya Kabudi katika jitihada zake za kulinda mfumo. katika mazingira ya aina hiyo, Kabudi hawezi kufua dafu kwa Lissu.