sasa mara nyingi hakuna mikataba baina ya watu binafsi na wahusika wengine wowote kwa minajili ya kufanya miradi ya serikali, kama kuna ufujaji wa fedha za uma hilo ni jambo jingine kabisa nje ya hiyo mikataba, ila ukae ukijua kua watumishi wa serikali wengi wao ni hawa hawa ndugu zetu tunaoka nao mtaani, tunawaona kila siku na tunashirikiana nao, na wengine hata ni wanachama wa ukawa, kwahiyo wanaweza kua wanashiriki kuiba fedha za serikali halafu wanadai tena serikali haitimizi majukumu yake wakati wanachangia kuingiza hasara inayopelekea kusimama kwa miradi mingi, halafu unakuta tena fedha zitokanazo na ufujaji serikalini zinawekezwa kwenye miradi binafsi ya watu hao, na mapato ya miradi hiyo inatumika kufadhili kampenzi za vyama vya huko upinzani tena, kwahiyo ndugu kuna mzunguko mkubwa sana wa ufisadi, usipigie kelele serikali ya CCM tu, tunaishi na mijizi huku mtaani na bado tunailea, kwa ujumla tuache wizi watanzania wenzangu, tunajitia hasara wenyewe, ushauri tu