Uchaguzi 2020 Lissu aanza kutumia Chopa. Kutikisa Bagamoyo, Kibaha na Chalinze leo

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Tundu Antipas Lissu, Mgombea Urais kupitia CHADEMA anayeaminiwa na wengi kushinda Urais mwaka huu leo anaanza rasmi kuruka angani kwa kutumia Chopa maalum.

Baada ya mapumziko ya siku 2 mgombea huyo leo anatarajiwa kuingia mkoani Pwani kwa kishindo ambapo atafanya mikutano mikubwa ya kampeni katika miji ya Kibaha, Chalinze na Bagamoyo.

Mara baada ya awamu ya kwanza kuzindua kampeni kwenye kanda zote 10 kwa sasa lengo kubwa ni kufanya mikutano mingi ya kukutana na wananchi kwa kila mkoa na kila Jimbo la Uchaguzi.

#Niyeye2020
 
Back
Top Bottom