UCHAGUZI MKUU 2015 CHADEMA TUKO PEKE YETU HUKU VYAMA VINGINE VYA 'UPINZANI' TAYARI VIKIPATA BEI HATA KABLA YA MBIO KUANZA
Ujumbe wa Profesa Lipumba ni neema na baraka kwa wapigania ukombozi wa kweli kupata picha halisi ya aina ya kambi ya upinzani tulionayo kabla ya kuchelewa sana.
Kama Lipumba anadiriki kutoa kauli ya kumshushia hadhi kiasi hiki kwa mtindo huu kwa vyombo vya habari, je anapokua faraghani na CCM uvundo wa mazungumzo yao yatakuaje?
CHADEMA sikilizeni na tupate kuimarika azma zaidi na zaidi; The Strongest Political Party in a scarthing Revolution against all odds and ills in a Nation is the party that seeks to stand its ground ALONE while surrounded by a critical mass of the electorate. Hili la Prof Lipumba nalo ni KIHUNZI nacho tutakiruka kwa uweza wake Mwenyezi Mungu hadi tufike kule WaTanzania wanakotutaka tukawafikishe tena bila kuchoka!!!
Siku CHADEMA kitakapogundua ukweli huu mchungu ya kwamba katika vita vya ukombozi wa walalahoi kuna chama kimoja tu na utitiri wa vyama vya 'upinzani' vilivyogeuka kuwa vibanda vya 'wafanyabiashara', nasema siku wapiga kura nasi tutakapo tambua ukweli huu na kupiga kura CHADEMA bila kutawanya kura hata moja nje - ni siku hiyo ndipo ukombozi wa kweli utakapowadia kwetu nchini bila chenga wala unafiki. Na siku hiyo ninayozungumzia ni siku ile isiokua na jina katika mwezi Oktoba 2015.
WaTanzania Walalahoi tulio wengi, naamini wengi mtakua mmepigwa na butwa baada ya kusoma ujumbe huu toka CUF dhidi ya CHADEMA lakini ni vema imejulikana mapema kwamba chama pekee cha upinzani nchini ni kimoja tu vingine vikigeuka mighahawa ya CCM kuja kutumika kutafuta kushinda azma yetu kutaka mabadiliko kama ambavyo tulivyoshuhudia vyama vikitumika kwenye uchaguzi nchi jirani ya Kenya.
Lipumba tumekusikia, amani tunakutakia; ni kawaida penye siagi watu kuegemea na usomi wao wote kupotelea pindi tumbo linapotokea kuwa ndicho mzania wa kufikiria!!
Nenda utokomee mwanakwetu, nenda, Lipumba nenda, wala usijali kitu WaTanzania watu wadogo wanaolia kwa machungu ya kuonewa na kutamani kupata mtetezi na mfariji kwao!!
Lipumba nenda; alimradi familia yako imekula vizuri ikashiba, hata kama UFISADI umetanda kila kona ya nchi na watu kukosa haki, nasi huku uswahilini shiba yako ni neema tosha kwetu na ndio maana kwa kauli moja tunakushangilia na Chama Cha Wananchi CUF kwa ujumbe huo hapo juu!