Lipumba 'aisigina' CHADEMA bungeni

Lipumba 'aisigina' CHADEMA bungeni

Kila mtu huyaona mambo kwa maono tofauti kutegea na imani na mtazmo wake,kwangu mimi naona kunaukweli fulani katika hii taarifa ya lipumba.
 
Hakuna mtu mzima ambaye huongea pumba kabisa katika maneno kumi ya lipumba yawezekana nusu au robo tatu yakawa na ukweli.
 
Mh. Lipumba unaheshimika hebu chambuzi zako jitahidi zisiwe na dosari au mwandishi kaongeza ya kwake? Maana utakuja ulizwa hivi Nawewe ni Professor?

Profesa Lipumba ana haki ya kusema lile analoamini hata kama litapata watu wawili kwa kila watu kumi kwa lile alilolisema. Profesa Lipumba 1995 aligombea urais akashindwa; 2000 akagombea tena akashindwa; 2005 akagombea tena akashindwa; 2010 akagombea tena akashindwa. Ninaomba yeyote mwenye kujua siri ya kushindwa kwake kwa mara zote anapogombea urais. Pili, ninaomba yeyote mwenye ushawishi mvuto anishawishi kwa nini na kwa yapi niendelee kumwamini Profesa huyu wakati alikuwa mshauri mchumi wa Rais huko nyuma na matokeo hasi ya ushauri wake yanayoonekana hadi leo hata kumfanya Profesa mwenyewe kwa kujua au kusahau, kuanza kubeza ushauri wake mwenyewe kwa sera mfu za serikali alizozitumikia huko nyuma?
 
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amesema vurugu zinatokea ndani ya Bunge hivi sasa zinasababishwa na kuyumba kwa Kambi Rasmi ya Upinzani. Akizungumza Dar es Salaam jana, alisema hatua hiyo inatokana na Kambi ya Upinzani kupoteza uwezo wa kujenga hoja za mashiko na mbinu madhubuti za kuwabana wabunge wa CCM bungeni.

Alisema Bunge limekuwa na vurugu hali inayosababishwa na baadhi ya wabunge kutotii kanuni za Bunge na kiti cha Spika Anne Makinda kuyumba katika kusimamia kanuni za chombo hicho.

Alisema mhimili huo wa Bunge hivi sasa unaonekana ni kituko kwa wananchi hali inayosababishwa na wabunge kubeba hoja za vyama na si za wananchi.

Alisema kumekuwa na tabia mbaya kwa baadhi ya wabunge wa CHADEMA ambao wamekuwa wakifuata mfumo wa CCM wa kwenda bungeni na hoja zinazobeba chama chao na si Watanzania wote kama jinsi CCM wanavyofanya.

"Kambi Rasmi ya Upinzani imeshindwa kulinda utaratibu mzuri wa kutetea maslahi ya umma bila jazba na hoja zenye mashiko kama jinsi ilivyokuwa miaka ya nyuma CUF ilipokuwa ikiongoza kambi hiyo.

"CUF tunaitaka Kambi Rasmi ya Upinzani ijipange upya kwa utaratibu ulio na mikakati mizuri ya kutetea hoja za wananchi bungeni bila kuyumbishwa na wabunge wa CCM.

"Bunge la hivi sasa limekuwa na vurugu za hapa na pale hasa wabunge kutotii kanuni za Bunge. Mfano wabunge kuzomea ovyo, tabia za kutovumiliana, kutotii amri ya spika, wabunge kutohudhuria vikao vya Bunge. Hii yote inatokana na meza ya Spika kupoteza sifa za kuliongoza Bunge.

"Hasa pale spika anakuwa anafanya uamuzi unaoubeba upande wa CCM na kupuuza upande wa upinzani ama kutupilia mbali hoja za upinzani kwa sabau zisizo za msingi.

"Hali kadhalika kuyumba kwa kuruhusu kujadili jambo ambalo lipo chini wa muhimili mwingine wa dola yaani Mahakama na bado hukumu ya jambo hilo haijatolewa," alisema Profesa Lipumba.

Mwenyekiti huyo wa CUF, alisema kuwa kutokana na hali hiyo hivi sasa Bunge limekuwa na matumizi mabaya ya muda kwa kuwa na ubishi usio na tija yoyote ama maslahi kwa wananchi.

Alisema wabunge wamekuwa wakiwaingilia wabunge wenzao kwa hoja na miongozo isiyo na mashiko wanapozungumza ili mardi tu awe amemvuruga mwenzake asiendeleee kuchangia kwa lengo la kutaka kuua hoja ya mbunge mwengine.

Kutoka gazeti la Mtanzania
 
Kwa nini kila mara vulugu zinapotokea Mkuu wa kambi ya upinzani, Mh. Mbowe huwa hayupo bungeni?

Kuna kuwa kama njama fulani zinakuwa zimepangwa ili labda ionekane Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzania hahusiki kwa nia mbadala ku-protect image fulani ya chama.

Kama angekuwepo wakati vulugu zinafanyika lazima watu wangetaka kuona anafanya nini kuhusiana na wabunge wake wanaopiga kelele za hovyo bungeni.

There's something fishy in CHADEMA!!

Is this happen by coincidence?.
 
Kwenye bold hapo, moja ya hoja za Mbowe katika hotuba ya kuchangia bajeti ya ofisi ya waziri mkuu ilihusu suala la Lwakatare. Is this not a party issue?

Hii haikuwa issue ya kitaifa bali ilijikita zaidi kwenye maslahi ya chama.

Wewe kweli akili hamnazo, swala la ugaidi ni swala la chama?? Understand the motive behind,, alichosema mbowe ni comparison kati ya kesi halisi za ugaidi na kesi feki...kesi halisi hazishughulikiwi na kesi feki ndio zinashughulikiwa kiasi kwamba wananchi tunakosa imani na serikali.
 
Chama Cha Wananchi (CUF), kimesema vurugu zinazoendelea bungeni zinasababishwa na Kambi Rasmi ya Upinzani inayoongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, kushindwa kujenga hoja na mbinu za kuwabana wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema wabunge wa Chadema wana tabia ya kufuata mfumo wa kwenda bungeni na hoja zinazobeba chama chao na si za Watanzania wote kama jinsi CCM wanavyofanya.

“Kambi rasmi ya upinzani imepoteza uwezo wa kujenga hoja za mashiko na mbinu madhubuti za kuwabana wabunge wa CCM bungeni na badala yake Chadema, wamekuwa na tabia mbaya ya kubeba chama chao,” alisema Profesa Lipumba.

Alisema kambi rasmi ya upinzani pia imeshindwa kulinda utaratibu mzuri wa kutetea masilahi ya umma bila jazba na hoja zenye mashiko kama ilivyokuwa miaka ya nyuma ilipokuwa ikiongozwa na CUF, Kiongozi huyo alisema kambi ya upinzani inapaswa ijipange upya kwa utaratibu na mikakati mizuri ya kuteta hoja za wananchi bila kuyumbishwa na wabunge wa CCM.

“Bunge usiwe uwanja wa kuonyesha mbwembwe za chama bali uwe uwanja wa kutetea haki za wananchi, wabunge wanapaswa wabadilishe mitazamo ya kuona bungeni ni sehemu ya kujionyesha kisiasa na chama chako kinafanya nini nje ya Bunge,” alisema Lipumba.

Alisema viongozi wa Serikali wanapaswa kubadilika kuhusu namna ya kutoa majibu bungeni.

Profesa Lipumba alisema mawaziri wengi wanakuwa wakitoa majibu mepesi katika maswali ya msingi yanayoulizwa na wabunge wa upinzani.

Alisema Bunge linatumia muda na pesa za walipakodi vibaya kwa baadhi ya wabunge kuwa na ubishi usiokuwa na tija, kutoleana matusi na wengine kuingilia hoja za wenzao bila sababu za msingi.

Profesa Lipumba pia alisema Spika wa Bunge, Anne Makinda amepoteza uwezo wa kuliongoza Bunge.



Source: Gazeti la mwananchi

Baba na mwana wanaimba na kucheza............
 
Tangia CUF ijiunge na CCM, Lipumba amekuwa akianza kutoa pumba naye.
Hoja ya Mnyika ya maji darisalamu ilikuwa inataka kuleta maji kwa wanachama wa CHADEMA tu???
Hoja ya Nassari ya Elimu je, ilikuwa elimu kwa wana CHADEMA tu???

Umesahau hoja ya Msigwa kutaka vimini viruhusiwe ZNZ. Hoja ya Lema kuwa Waislam wanapendelewa na jk
 
Profesa Lipumba ana haki ya kusema lile analoamini hata kama litapata watu wawili kwa kila watu kumi kwa lile alilolisema. Profesa Lipumba 1995 aligombea urais akashindwa; 2000 akagombea tena akashindwa; 2005 akagombea tena akashindwa; 2010 akagombea tena akashindwa. Ninaomba yeyote mwenye kujua siri ya kushindwa kwake kwa mara zote anapogombea urais.......

Sababu za kushindwa na CCM waulize Slaa na Mbowe maana wote wamepigwa chini na CCM kwa nyakati tofauti, tofauti yao Slaa alikuwa makini sana mpaka akafanikiwa kuliona kontena la kura feki kule mbeya pamoja na kupewa taarifa za siri na watu wake walokuwa kwenye system juu ya mpango wa kuiba kura zake lakini hawakumpa mbinu ya kuzuia wizi huo!
 
basi inamaana Wa_tz ni wajinga? mbona wanapenda CDM kiasi hiki ?
 
wewe inakuuma nini?kama yupo kama hayupo wewe inakunyima kula?bogus!
Kwa nini kila mara vulugu zinapotokea Mkuu wa kambi ya upinzani, Mh. Mbowe huwa hayupo bungeni? Kuna kuwa kama njama fulani zinakuwa zimepangwa ili labda ionekane Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzania hahusiki kwa nia mbadala ku-protect image fulani ya chama. Kama angekuwepo wakati vulugu zinafanyika lazima watu wangetaka kuona anafanya nini kuhusiana na wabunge wake wanaopiga kelele za hovyo bungeni. There's something fishy in CHADEMA!! Is this happen by coincidence?.
 
Mwenzake katika ndoa amemkurupusha akaseme haya aliyosema.Utumwa ni kitu kibaya sana
 
Nawashauri cuf Lipumba akizungumza na waandishi muwe na camera then mnatoa cd hapa analishwa maneno amechambua kila sehemu hadi Kenya kagusia mabepari humu jamiifourm wanamlukia 2015 wafuasi Wa chadema wanarudi ccm atakaa mgombea anaekubalika na Mfumo kikwete atakuwa hayupo Ndio kula mlizozi pata 2010 manias kulikuwa
 
Walaka Wa kanisa Ndio uliowabeba chadema kila Mtu anajua kwa sera zipi mlizonazo kiboko yenu mwigulu
 
Chama Cha Wananchi (CUF), kimesema vurugu zinazoendelea bungeni zinasababishwa na Kambi Rasmi ya Upinzani inayoongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, kushindwa kujenga hoja na mbinu za kuwabana wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema wabunge wa Chadema wana tabia ya kufuata mfumo wa kwenda bungeni na hoja zinazobeba chama chao na si za Watanzania wote kama jinsi CCM wanavyofanya.

“Kambi rasmi ya upinzani imepoteza uwezo wa kujenga hoja za mashiko na mbinu madhubuti za kuwabana wabunge wa CCM bungeni na badala yake Chadema, wamekuwa na tabia mbaya ya kubeba chama chao,” alisema Profesa Lipumba.

Alisema kambi rasmi ya upinzani pia imeshindwa kulinda utaratibu mzuri wa kutetea masilahi ya umma bila jazba na hoja zenye mashiko kama ilivyokuwa miaka ya nyuma ilipokuwa ikiongozwa na CUF, Kiongozi huyo alisema kambi ya upinzani inapaswa ijipange upya kwa utaratibu na mikakati mizuri ya kuteta hoja za wananchi bila kuyumbishwa na wabunge wa CCM.

“Bunge usiwe uwanja wa kuonyesha mbwembwe za chama bali uwe uwanja wa kutetea haki za wananchi, wabunge wanapaswa wabadilishe mitazamo ya kuona bungeni ni sehemu ya kujionyesha kisiasa na chama chako kinafanya nini nje ya Bunge,” alisema Lipumba.

Alisema viongozi wa Serikali wanapaswa kubadilika kuhusu namna ya kutoa majibu bungeni.

Profesa Lipumba alisema mawaziri wengi wanakuwa wakitoa majibu mepesi katika maswali ya msingi yanayoulizwa na wabunge wa upinzani.

Alisema Bunge linatumia muda na pesa za walipakodi vibaya kwa baadhi ya wabunge kuwa na ubishi usiokuwa na tija, kutoleana matusi na wengine kuingilia hoja za wenzao bila sababu za msingi.

Profesa Lipumba pia alisema Spika wa Bunge, Anne Makinda amepoteza uwezo wa kuliongoza Bunge.



Source: Gazeti la mwananchi
Hawa maprofesa njaa hawa Cuf wapiganie ndoa yao waachane na Chadema
 
sitoshangaa kama unaweza kumuuliza mama aliyekuzaa hv na wewe ni mama? sa utashindwa kumuliza lipumba kama naye ni prof...nyie tena wasomi nguli wa nchi hii mnawezekana, sentensi zenu tatu za kingereza ushajiona newton

Ndg Jitahidi kusoma na kuelewa kitu kilichoandikwa, coment yangu haijanipa kuamini kuwa maneno kama hayo yametoka kwa mtu kama yeye na ndio maana nikauliza au mwandishi kaongeza ya kwake? Kingine ni kuwa inabidi ufahamu umama unakuja kiasili kutokana na maumbile maana ni mwenyezi mungu tu ndie asie kosea lakini u professor unasomewa na proffesor sio mungu kuwa hakosei na kwa mtu kama yeye nikashauri awe makini na mwisho kwa ujue kwa watu wanaotumikia jamii kama yeye wanapokosa umakini heshima yao hushuka na pengine kupunguza ushawishi kwa wanao mwamini ni hilo tu
 
ndo kilichowapeleka huko unadhani watafanya nini tofauti na hicho?!!!
 
Back
Top Bottom