Profesa gani ? Kwa maneno anayoongea hapo sidhani kama profesa au ndio kuchumia tumbo? K ama hana kazi mwambie aje nimpe kazi ya kufagia workshop yangu ,i will pay him better i promise
Ndoa tamu jamani.
Prof. anahitaji ku recharge!. Labda akachimbue kitabu tena. Hivi hakuna refresher programs za watu kama hawa? Maana sasa taalumu kapoteza, siasa kapoteza na chama kaua! Prof tafadhali!Namheshimu sana Prof. Lakini naona kajichanganya mno katika hoja hii. Anaposema wapinzani wanashindwa kujenga hoja halafu wakati huo huo anasema mawaziri wanatoa majibu mepesi, hapo anamaanisha nini?Majibu mepesi kwa maswali gani? Waliyojiuliza mawaziri wenyewe au kutoka upinzani. Kama ni kutoka upinzani amewezaje kujua kwamba jibu ni jepesi iwapo swali halikuwa na hoja ya msingi kwa wa-Tz kama alivyodai yeye mwenyewe?Binafsi nimeona Mh. Lipumba ameshindwa kujieleza.
Ya kale baba, enzi hizo!!!!!!!!! Historia,.tukaweke makumbusho.. Usisahau kwamba duniani hakuna permanency wala constancy!. Kila kitu na watu hubaddilika. Ukifahamu hii, hutadharau unachokiona leo kwa kuwa unaamini ulichosikia miaka 20 iliyopita. Ingekuwa hivyo, bado angekuwa nao. Hakuna mtu anayependa kupoteza kizuri.Unadhihirisha umbumbu wako kama haumjui waulize wamarekani na waingereza, uganda, kenya ni nani pr Lipumba.
Ndoa tamu jamani.
Unadhihirisha umbumbu wako kama haumjui waulize wamarekani na waingereza, uganda, kenya ni nani pr Lipumba.
Chama Cha Wananchi (CUF), kimesema vurugu zinazoendelea bungeni zinasababishwa na Kambi Rasmi ya Upinzani inayoongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, kushindwa kujenga hoja na mbinu za kuwabana wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema wabunge wa Chadema wana tabia ya kufuata mfumo wa kwenda bungeni na hoja zinazobeba chama chao na si za Watanzania wote kama jinsi CCM wanavyofanya.
"Kambi rasmi ya upinzani imepoteza uwezo wa kujenga hoja za mashiko na mbinu madhubuti za kuwabana wabunge wa CCM bungeni na badala yake Chadema, wamekuwa na tabia mbaya ya kubeba chama chao," alisema Profesa Lipumba.
Alisema kambi rasmi ya upinzani pia imeshindwa kulinda utaratibu mzuri wa kutetea masilahi ya umma bila jazba na hoja zenye mashiko kama ilivyokuwa miaka ya nyuma ilipokuwa ikiongozwa na CUF, Kiongozi huyo alisema kambi ya upinzani inapaswa ijipange upya kwa utaratibu na mikakati mizuri ya kuteta hoja za wananchi bila kuyumbishwa na wabunge wa CCM.
"Bunge usiwe uwanja wa kuonyesha mbwembwe za chama bali uwe uwanja wa kutetea haki za wananchi, wabunge wanapaswa wabadilishe mitazamo ya kuona bungeni ni sehemu ya kujionyesha kisiasa na chama chako kinafanya nini nje ya Bunge," alisema Lipumba.
Alisema viongozi wa Serikali wanapaswa kubadilika kuhusu namna ya kutoa majibu bungeni.
Profesa Lipumba alisema mawaziri wengi wanakuwa wakitoa majibu mepesi katika maswali ya msingi yanayoulizwa na wabunge wa upinzani.
Alisema Bunge linatumia muda na pesa za walipakodi vibaya kwa baadhi ya wabunge kuwa na ubishi usiokuwa na tija, kutoleana matusi na wengine kuingilia hoja za wenzao bila sababu za msingi.
Profesa Lipumba pia alisema Spika wa Bunge, Anne Makinda amepoteza uwezo wa kuliongoza Bunge.
Source: Gazeti la mwananchi
Hoja zinaletwa kihuni,kila mbunge anamatatizo yake jimboni kwake.nafikiri ugeni wa bungeni,na wote waliofukuzwa ni mara yao ya kwanza kuingia bungeni.
Asante profesor kwa kuliona hilo, hapa juzi kati niliweka uzi unaonyesha jinsi "wabunge wachadema wanavyokera sana" bungeni hawa mambumbu na waendeshwa na hisia wakaleta vioja kama walivyowabunge wao na kukosa hoja za kuwatetea wabunge wao matokeo yake wanaanza mbona mbona n wewe usubiri waje utakiona cha mtema miwa.
Hoja zinaletwa kihuni,kila mbunge anamatatizo yake jimboni kwake.nafikiri ugeni wa bungeni,na wote waliofukuzwa ni mara yao ya kwanza kuingia bungeni.