Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,502
- 9,282
Mwanafunzi (13) wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Maguja, Wilaya ya Ruangwa anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumlawiti mwanafunzi mwenzake wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Likangara.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo, Foka Dinya alisema mtuhumiwa anadaiwa kufanya kitendo hicho Februari 5 saa tano mchana.
Alisema kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kumetokana na baba wa mtoto anayedaiwa kufanyiwa kitendo hicho kumbaini kijana wake akiwa amekosa uchangamfu na kutembea kwa shida.
Dinya Alisema mtoto huyo alipouliza akaeleza kile alichofanyiwa na mwenzake.
Alisema kutokana na maelezo ya baba wa mlalamikaji, alilazimika kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi kisha mtuhumiwa akakamatwa na kufanyiwa mahojiano.
Alisema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani baada ya kukamilika kwa taratibu za kiupelelezi.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo, Foka Dinya alisema mtuhumiwa anadaiwa kufanya kitendo hicho Februari 5 saa tano mchana.
Alisema kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kumetokana na baba wa mtoto anayedaiwa kufanyiwa kitendo hicho kumbaini kijana wake akiwa amekosa uchangamfu na kutembea kwa shida.
Dinya Alisema mtoto huyo alipouliza akaeleza kile alichofanyiwa na mwenzake.
Alisema kutokana na maelezo ya baba wa mlalamikaji, alilazimika kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi kisha mtuhumiwa akakamatwa na kufanyiwa mahojiano.
Alisema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani baada ya kukamilika kwa taratibu za kiupelelezi.