Mafilili ni mmoja wa watu ambao huwa nawaheshimu sana akiwemo
ZeMarcopolo japo mpo against CHADEMA. Lakini katika hiyo hoja niliyoweka alama nyekundu, mzee umejishusha sana. Imeku-under-represent. Yaani umeonekana mweupe vibaya sana.
Hivi kwa kauli zile za akina Mwigulu ambazo hazina hata chembe ya ukweli unataka isiombwe miongozo? Kwa kauli kama za akina Serukamba, Kingwagallah na Silinde unataka isiombwe miongozo? Ulishawahi kuwasikia CHADEMA wakiomba miongozo dhidi ya Filikunjombe? CHADEMA wapo kwa ajili ya maslahi ya Tanzania na watanzania, kama CCM wangekuwa wanajenga hoja zenye nia ya kulijenga taifa hakuna mtu ambaye angeomba miongozo. Sasa akina Mwigulu kila wakisimama bungeni wanataja CHADEMA, utafikiri bungeni tumewatuma wakaijadili CHADEMA.
Inapotokea mtu anapotosha ukweli kwa maslahi ya chama badala ya kuangalia interest za nchi; kama ambavyo huwa anafanya Mwigulu au Wasira hivi kwanini wasiombe miongozo? Jaribuni wakati mwingine kushirikisha bongo zenu kabla ya kukurupuka na kuandika humu. Uandishi kama huu unawafanya mjidhalilishe, maana unawafanya muonekane kuwa ni watu mnayeyafikilia matumbo yenu tu na si taifa.
Be careful mkuu.