LUCAS Kadawi Limbu, mwenyekiti wa taifa wa chama cha siasa cha ACT-Tanzania, ameibuka na kumtuhumu Msajili wa vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, kuingilia mwenendo wa kesi ya madai dhidi ya Zitto Kbawe na genge lake.
Aidha, Limbu anatuhumu Jaji Mutungi kuwabeba wahalifu waliovamia chama chake, kukibadilisha nembo, kadi na katiba. Anaripoti Pendo Omary
(endelea).
Limbu aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Jumapili kuwa kitendo cha msajili cha kuruhusu ACT-Tanzania kubadilishwa jina, ni kuingilia uhuru wa mahakama na kutoa maamuzi nje ya mahakama.
Anasema, Huyu ni Jaji wa Mahakama Kuu. Amewahi kuwa Msajili wa Mahakama ya Rufaa na hakimu wa mahakama ya mkoa. Anajua taratibu, kwamba kuna kesi mahakamani na hivyo, siyo sahihi kuupa upande mmoja haki, wakati shauri halijaamuiriwa.Kauli ya Limbu imefuatia tamko la msajili la Ijumaa 24 Aprili mwaka huu, kuwa ACT- Tanzania imeruhusiwa kubadili jina na kuwa ACT- Wazalendo.
Limbu na wenzake watatu, waliwasilisha mahakamani 30 Januari mwaka huu, maombi ya kuitaka mahakama kumzuia Samson Mwigamba, Prof. Kitila Mkumbo na mawakala wao, kutojihusisha na chama hicho.
Amewatuhumu kufanya mapinduzi ndani ya chama; kuteka chama; kubadilisha bendera, nembo na sasa jina la chama. Kesi hiyo imepewa Na. 1 ya mwaka 2015.
Anasema, Msajili anajua kuwa kuna kesi iko mahakamani. Lakini yeye kwa maslahi yake binafsi, anaingilia uhuru wa mahakama na kutoa maamuzi ya kuifuta ACT- Tanzania na kuingiza chama kingine cha ACT Wazalendo.
Anasema madai kuwa Zitto na genge lake wameteka chama chake Alliance Change and Transparency (ACT-Tanzania) kinadhihirishwa na taarifa ya Jaji Mutungi kwa vyombo vya habari inayotaka ACT Tanzania, kurudisha cheti cha usajili walichopewa kwa jina hilo ili wapatiwe kingine chenye jina la ACT Wazalendo.
Limbu amesema Jaji Mtungi akiwa pia ni mwanasheria aliyebobea anayafanya hayo akijua jambo lolote likiwa mahakamani halitakiwi kufanyiwa marekebisho.
Tayari nimeiandikia barua Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuhusu wasiwasi wangu kwamba Jaji Mtungi anapewa rushwa ndio maana anafanya haya maamuzi kwa makusudi, ameeleza Limbu.
Amesema, Msajili Msaidizi, Sisty Nyahoza alieleza gazeti la MAWIO Jumatatu iliyopita kuwa chama kilicho kwenye orodha ya vyama hadi siku hiyo ni ACT Tanzania.
Alipoulizwa na mwandishi wa gazeti hilo kuwa chama cha ACT Wazalendo kipo na kinaongozwa na Zitto Kabwe alijibu
sikijui chama hicho na hapa kwetu hakipo.
Anasema, Leo ACT ina kadi tatu tofauti. Je, kukubali na kuruhusu mabadiliko makubwa hayo ameshaingilia hatma ya kesi yetu. Anajua tutashidwa. Huu ni mpango mkakati ambao unafanywa na kila mtu sasa anajua. Nina mtaka Jaji Mutungi awambie watanzania kuna nini nyuma ya ACT Wazalendo.
Akizungumzia hatma ya chama chake, Limbu amesema ACT Tanzania bado ipo. Ofsi ya msajili impe Kabwe jukwaa. Asajili chama chake. Atuache na chama chetu. Huu ni uhaini.
TUHUMA ZA LIMBU NA CHADEMA DHIDI YA ACT-WAZALENDO.
Na. Jashia Khamisi Maarufu.
Kumekuwepo na upotoshaji unaojirudia rudia kati ya Limbu na chams cha ACT -Wazalendo,limbu amekuwa akitoa matamko mbalimbali yenye nia ovu ya kuchafua taswira ya chama na kuuaminisha umma kuwa chama kina Mgogoro.
Naomba niweke kumbukumbu sahihi kwa wale walioanza kusahau.
Chama cha ACT-Wazalendo kilisajiliwa tarehe 05/05/2014.
Kwa mujibu wa Sheria chama kinaposajiliwa hutakiwa kufanya uchaguzi wa kidemokrasia ndani ya Mwaka mmoja.
Kama Chama kisipofanya uchaguzi,basi msajili wa vyama vya siasa anayomamlaka ya kukifuta.
Hivyo kamati kuu ya muda ya Chama cha ACT-Wazalendo ilikutana mjini Singida na kujadiliana kuhusu kufanya uchaguzi wa kidemokrasia ndani ya Chama,uchaguzi huru na haki.
Limbu akaomba uchaguzi ufanyike kwenye ngazi za chini lkn usifanyike kwa ngazi ya Mwenyekiti taifa.
Wajumbe walikataa na kumkumbusha misingi na malengo ya uanzishwaji wa Chama,hivyo kikao kikaamua kuwa Limbu kama anautaka uentekiti wa Chama basi agombee na akifanikiwa kuwashawishi wajumbe atachaguliwa kuwa Mwenyekiti.
Baada ya Limbu kuona ombi lake limegonga Mwamba,alipofika Dar es Salaam akaitisha kikao cha dharura kilichohudhuriwa na wajumbe saba na akakiita kikao cha kamati kuu.
Katika kikao kile akatangaza kuwavua uanachama katibu Mkuu Ndugu Samson Mwigamba,Kitila Mkumbo,Mwanasheria wa Chama ,Makamu Mwenyekiti na kuwafuta uanachama wajumbe wote ambao hawakuunga mkono ombi lake la kubaki madarakani bila kufanyika uchaguzi.
Taarifa ya Limbu ilikuwa inaratibiwa kwa ustadi mkibwa na Viongozi waandamini wa Chadema kwa Lengo la Kumkomoa Zitto Kabwe ambae walipata tetesi kuwa endapo akifukuzwa Chadema kuwa atahamia ACT-Wazalendo.
Kwakuwa Chama kinaposajiliwa huwa mali ya Umma na si mali binafsi ya mtu,kwakuwa vyama vyote lazima viwe na katiba inayovindesha ambayo ndio itakuwa rejea ya mwisho kunapotokea utata wowote,kwakuwa swala la Uchaguzi ni swala Msingi kwa chama chochote ndanu ya nchi yetu,Limbu na maamuzi yake hayakupuuzwa,ilibidi kamati kuu ambayo ndiyo halali ikutane haraka baada ya kuitwa na katibu Mkuu.
Katika kile kikao,pamoja na Mambo mengine,swala la Limbu lilojadiliwa na kufanyiwa maamuzi.
Limbu akavuliwa madaraka ya uenyekiti kwa kuvunja katiba ya chama kwa makusudi.
Limbu alijua kuwa yeye kama mwenyekiti,hakuwa na Mamlaka ya kuitisha kikao chochote cha Kamati kuu au halmashauri kuu,Limbu alijua kuwa kwa Mujibu wa katiba ya ACT-Wazalendo,Mwenye mamlaka ya kuitisha vikao ni katibu mkuu wa chama,hivyo Limbu alikuwa na Agenda ya siri ya kukivuruga chama kwa maelekezo kutoka Viongozi wa juu wa Chadema.
Kwanini Viongozi wa Chadema wanahusishwa katika kadhia hii? (Fuatilia utaelewa)
Mara baada ya kikao lilichomfukuza Limbu,kikao kilichohudhuriwa na wajumbe zaidi ya 63 kutoka mikoa mbalimbali,Kikao kiliamua kuwasimamisha uongozi wote waliohusika kuvuruga chama kwa mujibu wa katiba ya ACT-Wazalendo.
Mara baada ya maamuzi,Limbu kwa kusaidiwa na Saidi Kubenea (Kiongozi Mwandamizi na Muhariri wa gazeti la Mawio)walikwenda mahakama kuu kupinga maamuzi ya kikao
Walihangaika pamoja kwenye korido ili kuzuia kikao cha kamati kuu kubariki maamuzi yaliyofanywa na halmashauri kuu,lkn Limbu na kubenea waliambulia patupu baada ya kila mwanasheria waliemuomba kuwasaidia kukataa baada ya kuona kesi haina kichwa wala miguu.
Limbu baada ya kukosa utetezi mahakamani akaenda kwa msajili wa vyama vya siasa na kudai kuwa amepata taarifa kuwa Zitto atakuja kwenye chama chake kwa kukaribishwa na Mwigamba na Kitila ,hivyo Msajili amzuie Zitto asijiunge na ACT-Wazalendo.
Msajili akatumia busara ya kawaida tu ,kuita pande zote zipeleke utetezi ili kuangali nani yupo sahihi.
Baada ya Msajili kupitia utetezi wa pande zote,na kurejea vifungu vya katiba ya Chama,Msajili alikubaliana kuwa Limbu kama mwenyekiti hakuwa na mamlaka ya kuitisha kikao chochote,hivyo vikao alivyotumia kufanyia maamuzi ni vikao Batili,
Pamoja na hayo,Msajili alisema kuwa hata kama Limbu angekuwa na mamlaka ya kuitisha vikao,Vikao hivyo vilipaswa kuhudhuriwa na zaidi ya nusu ya wajumbe ili viwe vikao halali.
Hivyo kwa kikao cha watu karibu 70 kuhudhuriwa ma watu sana ,sio tu ni uvunjaji wa katiba ya Chama bali ni uvinjaji wa sheria ya usajili wa vyama vya siasa.
Msajili akasisitiza kuwa hapendi kuona vyama vinaendeshwa kiujanjaujanja bali lazima vifanye chaguzi zake kwa mujibu wa sheria,akamshauri Limbu kukubaliana na maamuzi ya vikao halali vya chama na akamtaka agombee kama wenzake watakavyogombea ili kuwapata viongozi waliochaguliwa na wanachama.
Limbu akaondolewa kwenye orodha ya wawakilishi wa vyama kwenye vikao vya TCD (Tanzania Centre for Democracy).
Mgogoro uliokuwa ukipewa coverage sana na Magazeti ya Mawio na Tanzania Daima ambayo ni mali za Viongozi wandamizi wa Chadema.
Chama kilipotangaza ratiba ya Uchaguzi kuanzia ngazi ya Tawi hadi taifa Limbu hakugombea nafasi yoyote ya kuchaguliwa.
Uchaguzi ulipohitimishwa na kutangaza uzinduzi rasmi wa Chama mnano 29-03-2015
Limbu aliibuka kwa kasi Mpya huku taarifa za mawasiliano yake na Viongozi wa Chadema zikiwa wazi kabisa.
Limbu kwa Msaada wa Chadema akaenda kufungua kesi kuweka Zuio la Mkutano Mkuu na Uzinduzi wa chama huku akiwa na madai mapya ya madai ya fedha dhidi ya katibu Mkuu bw.Samson Mwigamba.
Viongozi wa Chadema waliwaondoa wasiwasi vongozi wao wa wilaya Mikoa na Kanda kuwa wasihofie Ujio wa ACT-Wazalendo kwa kuwa tayari kuna zuio mahakamani na kamwe chama hakitazinduliwa.taarifa hizi niliambiwa na Mwenyekiti na katibu ea chadema wa wilaya ni ayoishi ambao niwafuasi wa ACT-Wazalendo huku wakiwa viongozi wa chadema.
Magazeti ya Chadema yaani Mawio na Tanzania Daima yakawa hayaandiki habari nyingine zaidi ya ACT-Wazalendo yapigwa marufuku kufanya Uzinduzi.
Wanasheria wa chama cha ACT wakafika mahakani kukitetea Chama na mwisho mahakama ikaamua kuwa ACT-Wazalendo iendelee na kazi zake kwani kesi ya Msingi inamuhusu Mwigamba binafsi.
Uzinduzi ukafanyika kwa mafanikio makubwa,ACT-Wazalendo ikapata viongozi wapya wenye ari na kiu ya kukieneza Chama,Matangazo ya Uzinduzi yalirushwa na Kituo cha (ITV) ,Chadema wakachanganyikiwa,wakaona kana fedha ns jitihada zilizotumika kuhujumu chama Zimeliwa bure bila mafanikio.
Wakaibuka na Madai mapya ,Madai ikawa kuhoji Fedha za Uzinduzi zimepatikana wapi?
Hoja za Limbu Zikafa,wakasema kuwa kujenga chama ni kazi kubwa saana,kuwa Chama cha ACT-Wazalendo ni chama cha FACEBOOK,JAMIIFORUMS na TWEETER.
Wakatamba kuwa waende field waone ugumu wa kazi na wakakejeli kuwa hawatapata hata wa kuwasikiliza..
Chama kikaanza mikutano yake
Kikaanzia Ruvuma,Njombe,Iringa,Morogoro,Dodoma,Singida,Tabora,Kahama,na Shinyanga.
Mwitiko wa watu ukawa sawa na Kivumo cha Kimbunga,hamasa ya Mikutano ikawa kubwa kuliko maadui wa ACT-Wazalendo walivyotegemea.
Kikao cha haraka cga Chadema kikaitishwa Mkoani Pwani,Madhara ya mikutano ya Chama yakaatajwa,hivyo mpango mkakati wa kuvuruga mikutano ya ACT-Wazalendo ukawekwa.
Ikawa kuhakikisha Chadema wanawatangulia ACT-Wazalendo kuhakikisha wanawabia wananchi ubaya wa ACT-Wazalendo.
Wakawakataza kuhudhururia mikutano ya ACT-Wazalendo kwa madai kuwa wamekuja kuvuruga upinzani.
Wakafanya ,hivyo Mwanza,Musoma,na Simiyu.
Tofauti na matarajio yao,umati uliojitokeza kwenye mikutano ya Mwanza ,Musoma na Simiyu ilikuwa salamu kuwa wananchi wameiasi Chadema na matumaini yao kubaki ACT-Wazalendo.
Waliotangulia Mbele kuvuruga wakawa kama ndio wanaisafishia njia ACT-Wazalendo.
Madai Mapya yakaibuka,awamu hii wakamtumia tena Limbu ambae alishandwa majaribio yake yote.
Limbu akaandaliwa Press conference ili atie ya moyoni.
Limbu akaibuka na hoja zilezile za Mnyika,kuwa Fedha za Uzinduzi na Mikutano ACT-Wamezipata wapi?
Akahoji mamlaka ya ACT-Wazalendo kubadilisha jina lake la awali la ACT-Tanzania.
Limbu akahoji uhalali wa ACT-Wazalendo kubadilisha kadi ,Bendera na nembo ya Chama.
Haya ni maswali ambayo sikutegemea kusikia yakiulizwa na Limbu pamoja na waliomtuma
Limbu kabla ya kuuliza swala la fedha za mikutano,alipaswa kijiuliza yeye wakati anazunguka mikoani kutafuta wanachama ili kusajili chama,alipata wapi fedha za kizunguka mikoa 10 ya Tanzania Bara na mikoa 2 ya Unguja na pemba wakati chama hakikuwa na ruzuku?
Kama angekumbuka jinsi alivyopata fedha basi asinge hoji vitu ambavyo anamajibu,huenda hakujiuliza swali hilo kwa lengo la kupata ulaji toka kwa waliomtuma...
Kihusu Kubadilisha Jina la Chama,Chadema na Limbu wanajua kama Sheria ya vyama vya siasa inaruhusu kibadilisha Katiba,Nembo,Jina,na hata rangi za bendera.
Chama cha PPT maendeleo kilibadilisha jina lake na kujiita APPT maendeleo lkn si Chadema wala Limbu waliohoji uhalali wa kubadilisha jina,huenda kwakuwa APPT haikuwa na Zitto,Kitila na Mwigamba.
Chadema yenyewe ilibadisha katiba yake ya 2004 mnamo mwaka 2006 katiba ambayo ndiyo inatumika sasa.lkn si limbu wala Chadema yenyewe iliyohoji mabadiliko hayo pamoja na kuwa yalifuta ukomo wa madaraka kwa viongozi wajuu.
Chadema ilibadili nembo yake toka ile ya vidole viwili (Chadema Vema)na kuwa na nembo ya M4C lkn hakuna aliehoji mabadiliko hayo huenda kwa kuwa yalifanywa na watu wenye hati miliki ya upinzani Tanzania.
Chadema ilibadili Rangi ya Bendera yoka rangi (Light Bluu, Nyeupe na Nyeusi) na kuongeza rangi Nyekundu kwenye Bendera na vifaa vyote vya uenezi ikiwemo kadi na miongozo ya Chama lkn hakuna aliethubutu kudai kuwa Msajili alihongwa na chadema .
Kuibuka kwa Limbu upya ni mwendelezo wa ushindi kwa ACT-Wazalendo kutokana na wanaomtumia kumpa hoja dhaifu ambazo kila Mwananchi anazipuuza.
Nimalizie kwa kutoa ushauri kwa Viongozi wa ACT-Wazalendo kuwa,Tanzania inamambo mengi ya kuzungumziwa kwa lengo la kuwaletea nafuu wananchi waliokata tamaa.
Baada ya Chadema kushindwa kufanya siasa za Maswala (Isues)na kijilita kufanya siasa nyepesi za kutaja majina ya watu,Chadema imekosa mvuto mbele ya watu.
Watu wameanza kuipuuza na kuwaunga mkono ACT-Wazalendo.
Kuibuka kwa aki na Limbu,kinalenga kuwaondoa kwenye ajenda za Msingi,kunalenga kupotosha nia njema Mliyonayo kwa Nchi yetu.
Wasiwaondoe njiani,sambazeni uzalendo kila kona ya Tanzania hasa tunapoelekea uchaguzi Mkuu .
Source ya habari ni kwa hisani ya
M2 wa Makao Makuu.