Elections 2015 Licha ya kukubalika, Jina la Lowassa halitafika hata CC!

Wanabodi,

Hii ni tetesi ya habari mbaya kwa wapenzi wa kipenzi cha watu, Waziri Mkuu Mtaafu, Edward Lowassa kuwa pamoja na Mhe. Lowassa kuwa ndie mtu anayekubalika sana kuliko mtu mwingine yoyote ndani ya CCM, wale wasiolitakia mema taifa hili, wamepania kupanga njama za kumhujumu kwa kuhakikisha kuwa jina lake halitaingia hata ndani ya kikao cha CC kujadiliwa!, wamepanga kumchinjia baharini kwenye kamati ya maadili, itakayoyajadili majina wagombea kabla ya kuyaingiza kwenye Kamati Kuu, kujadiliwa!.

Lengo la hujuma hiyo ni kufuatia Lowassa kukubalika kupindukia, jina lake likifika tuu CC, hakuna wa kumkata, hivyo wahafidhina wa CCM, wanaounga mkono kambi ya mmoja wa wagombea, wameapa kuhakikisha jina la Lowassa, halivuki kisingiti cha kamati ya maadili, hivyo kumchinjia rasmi baharini, ili mgombea wao apete kwa mteremko!.

Naomba nisitaje chanzo cha habari hizi, kwa kutumia kanuni ya "the confidentiality of the source"
ila kwa vile hizi ni tetesi tuu, zitakapothibitika ndipo nitaweka source!.

Kama kawaida yetu jf, habari kama hizi ambazo hazijathibitishwa, zimeletwa humu hivi hivi zilivyopokelewa, ili wewe kama mwana jf, be the first to know!, na information is power!, hivyo kutoa fursa kwa wenye uwezo wa kuizuia hii mipango dhalimu inayopangwa, kutaka kuwakosesha Watanzaia mgombea kipenzi chao, chaguo la wengi, na mwenye uwezo usio tia shaka kuyamaliza matatizo yote ya taifa letu Tanzania.

Hii ni thread ya info tip, tuu, hivyo naomba nisiulizwe swali lolote kuhusu hii news tip for your info tuu.

NB. Chama cha Mapinduzi ni taasisi huru yenye uwezo wa kufanya shughuli zake kwa uhuru vile ambavyo wataona wenyewe inafaa, ikiwemo vigezo na jinsi ya kuwachagua wagombea wake, ila kwa sisi ambao ni wakereketwa wa mustakali mwema wa nchi hii, kamwe hatutakubali, kuona watu wenye uwezo na wanaokubalika na wengi, wakienguliwa kwa mizengwe tuu, kitu ambacho CCM imekuwa ikikifanya mara nyingu huko nyuma na labda ni kweli ndicho walichopanga kukifanya mwaka huu!, yaani CCM imekuwa ikiwaengua wagombea wazuri kwa mizengwe na ikabaki salama!, lakini this time, nimewasikia baadhi ya wana CCM kindakindaki, kuwa wamejiapiza, this time CCM ikimuengua chaguo lao kwa mizengwe, patachimbika!.

Pasco

Sasa wewe Pasco unalilia nini? Mwenyekiti wenu alishasema kuwa watu waliojitokeza hawana sifa akiwamo na EL, hivyo akawaomba wanachama kuwashawishi wagombea wengine, yeye lowasa kaamua kuwashawishi watu ili wamshawishi. So tegemea tetesi yako kuwa kweli coz wewe mwenyewe uko jikoni.
 
Mimi nadhani kama hawatampitisha na uku ikiaminika kuwa anaungwa mkono na watu wengi ndani na nje ya chama chake kwanini asigombee kupitia chama kingine.
 
Heshima mbele mkuu.Lowasa ni kweli kabisa anapendwa na wengi lakini kwa mimi mwaka huu sijaona mgombea mahususi toka vyama vyote.Lakini kuna baadhi ya masuali huwa najiuliza,Ni mgombea gani ndani ya CCM hana kashfa ya ufisadi?.Je baada ya EL kuenguliwa kutokana na ufisadi hatujaona tena au kuthibitisha ufisadi mwingine baada ya yake?.Je kama viongozi wote ni wachafu ndani ya ccm itabidi wawapitishe kuangalia nani mchapakazi zaidi ingawa ana makandokando?.Je ccm itakapo acha kumpitisha kuwania uraisi ana ujasili wa kuhama chama?.Na nini kitakachotekea ndani ya ukawa baada ya EL kuacha kupitishwa ndani ya CCM?.Na je hatuoni kwamba baadhi ya wagombea wa UKAWA kila mtu atahisi kuishinda ccm imeyobaki dhaifu baada ya EL kuondoka?.Je hao mashekhe na Maaskofu wanao mpigania EL kuwa raisi wanahitaji nini kutoka kwake?.Mimi nafikili ccm wawe makini sana na uamuzi wowote ule watakao fanya.Na pia Ukawa wawe makini sana kama EL akihama chama mana kila mgombea wa ukawa anaweza hisi anazo nguvu za kuishinda ccm dhaifu baada ya EL kuondoka na kundi kubwa na hivyo ikawa ni mwazo wa UKAWA kusambaratika.

Misconstrued feelings. No objective analysis.
Pole
 
kama tunaamini katika utafiti, wakimbwaga EL , nimefuatilia ni mara ya pili utafiti unaonyesha kuwa ni EL na Dr. Slaa, hayo tuachie ccm wataamua wenyewe, ila njia ya kwenda Ikulu mshale unagongea upande wa UKAWA kwa sasa, Mungu amechoshwa na ufisadi wa ccm , ameamua kuwapiga upofu wasijui la kufanya kuelekea October
 
Wanabodi,

Hii ni tetesi ya habari mbaya kwa wapenzi wa kipenzi cha watu, Waziri Mkuu Mtaafu, Edward Lowassa kuwa pamoja na Mhe. Lowassa kuwa ndie mtu anayekubalika sana kuliko mtu mwingine yoyote ndani ya CCM, wale wasiolitakia mema taifa hili, wamepania kupanga njama za kumhujumu kwa kuhakikisha kuwa jina lake halitaingia hata ndani ya kikao cha CC kujadiliwa!, wamepanga kumchinjia baharini kwenye kamati ya maadili, itakayoyajadili majina wagombea kabla ya kuyaingiza kwenye Kamati Kuu, kujadiliwa!.

Lengo la hujuma hiyo ni kufuatia Lowassa kukubalika kupindukia, jina lake likifika tuu CC, hakuna wa kumkata, hivyo wahafidhina wa CCM, wanaounga mkono kambi ya mmoja wa wagombea, wameapa kuhakikisha jina la Lowassa, halivuki kisingiti cha kamati ya maadili, hivyo kumchinjia rasmi baharini, ili mgombea wao apete kwa mteremko!.

Naomba nisitaje chanzo cha habari hizi, kwa kutumia kanuni ya "the confidentiality of the source"
ila kwa vile hizi ni tetesi tuu, zitakapothibitika ndipo nitaweka source!.

Kama kawaida yetu jf, habari kama hizi ambazo hazijathibitishwa, zimeletwa humu hivi hivi zilivyopokelewa, ili wewe kama mwana jf, be the first to know!, na information is power!, hivyo kutoa fursa kwa wenye uwezo wa kuizuia hii mipango dhalimu inayopangwa, kutaka kuwakosesha Watanzaia mgombea kipenzi chao, chaguo la wengi, na mwenye uwezo usio tia shaka kuyamaliza matatizo yote ya taifa letu Tanzania.

Hii ni thread ya info tip, tuu, hivyo naomba nisiulizwe swali lolote kuhusu hii news tip for your info tuu.

NB. Chama cha Mapinduzi ni taasisi huru yenye uwezo wa kufanya shughuli zake kwa uhuru vile ambavyo wataona wenyewe inafaa, ikiwemo vigezo na jinsi ya kuwachagua wagombea wake, ila kwa sisi ambao ni wakereketwa wa mustakali mwema wa nchi hii, kamwe hatutakubali, kuona watu wenye uwezo na wanaokubalika na wengi, wakienguliwa kwa mizengwe tuu, kitu ambacho CCM imekuwa ikikifanya mara nyingu huko nyuma na labda ni kweli ndicho walichopanga kukifanya mwaka huu!, yaani CCM imekuwa ikiwaengua wagombea wazuri kwa mizengwe na ikabaki salama!, lakini this time, nimewasikia baadhi ya wana CCM kindakindaki, kuwa wamejiapiza, this time CCM ikimuengua chaguo lao kwa mizengwe, patachimbika!.

Pasco

Pasco you have conflict of interest in this EL tetesi story.
EL is your client, as PR firm, so the public should take such words as ‘Lowasa kipenzi cha Watanzania wengi' with maximum caution.
 
kama tunaamini katika utafiti, wakimbwaga EL , nimefuatilia ni mara ya pili utafiti unaonyesha kuwa ni EL na Dr. Slaa, hayo tuachie ccm wataamua wenyewe, ila njia ya kwenda Ikulu mshale unagongea upande wa UKAWA kwa sasa, Mungu amechoshwa na ufisadi wa ccm , ameamua kuwapiga upofu wasijui la kufanya kuelekea October

Watafiti wa aina hiyo ndio kuna mswada umepitishwa ili itungwe sharia wafungwe
 
Wanabodi, Hii ni tetesi ya habari mbaya kwa wapenzi wa kipenzi cha watu, Waziri Mkuu Mtaafu, Edward Lowassa kuwa pamoja na Mhe. Lowassa kuwa ndie mtu anayekubalika sana kuliko mtu mwingine yoyote ndani ya CCM, wale wasiolitakia mema taifa hili, wamepania kupanga njama za kumhujumu kwa kuhakikisha kuwa jina lake halitaingia hata ndani ya kikao cha CC kujadiliwa!, wamepanga kumchinjia baharini kwenye kamati ya maadili, itakayoyajadili majina wagombea kabla ya kuyaingiza kwenye Kamati Kuu, kujadiliwa!.

Ndiyo maana Mkapa alikuita KANJANJA! Unaandika vitu ambavyo huna ujuvi navyo! Soma kwanza katiba ya CCM kabla ya kuleta vapour zako jukwaani.

FYI, Kamati ya maadili ya CCM haina uwezo na mamlaka ya kukuta jina la mgombea yeyote wa Urais wa JMT, hata kama mgombea huyo SIFA yake pekee ni UFISADI.

Kamati ya maadili ya CCM hujadili majina yote ya wagombea na kuyapatia grades A,B,C,D&F na kuyapeleka majina ya wagombea wote kwenye CC ya CCM.

Kikao chenye madaraka ya kukata majina ya wagombea ni CC ya CCM pekee yake.

User yako ni verified lakini bado unaandika vapour kiasi hiki!
 
Misconstrued feelings. No objective analysis.
Pole
Mkuu unapopinga kitu then we huonyeshi kitu kinachoweza tokea mbeleni basi we pia ni TATIZO.Sisi wengine tusio na vyama lakini tunao amini katika wana mageuzi wa kweli huwa tunampongeza mtu na kumkosoa mtu na kumuonesha namna ya kufanya.Sasa wewe unaonyesha kwamba ni hisia tu hakuna ukweli,Unasahau kwamba kila kinachozungumzwa au kutendwa huwa ni hisia tu kabla ya ukweli haujabainika.
 
Heshima mbele mkuu.Lowasa ni kweli kabisa anapendwa na wengi lakini kwa mimi mwaka huu sijaona mgombea mahususi toka vyama vyote.Lakini kuna baadhi ya masuali huwa najiuliza,Ni mgombea gani ndani ya CCM hana kashfa ya ufisadi?.Je baada ya EL kuenguliwa kutokana na ufisadi hatujaona tena au kuthibitisha ufisadi mwingine baada ya yake?.Je kama viongozi wote ni wachafu ndani ya ccm itabidi wawapitishe kuangalia nani mchapakazi zaidi ingawa ana makandokando?.Je ccm itakapo acha kumpitisha kuwania uraisi ana ujasili wa kuhama chama?.Na nini kitakachotekea ndani ya ukawa baada ya EL kuacha kupitishwa ndani ya CCM?.Na je hatuoni kwamba baadhi ya wagombea wa UKAWA kila mtu atahisi kuishinda ccm imeyobaki dhaifu baada ya EL kuondoka?.Je hao mashekhe na Maaskofu wanao mpigania EL kuwa raisi wanahitaji nini kutoka kwake?.Mimi nafikili ccm wawe makini sana na uamuzi wowote ule watakao fanya.Na pia Ukawa wawe makini sana kama EL akihama chama mana kila mgombea wa ukawa anaweza hisi anazo nguvu za kuishinda ccm dhaifu baada ya EL kuondoka na kundi kubwa na hivyo ikawa ni mwazo wa UKAWA kusambaratika.

Nakubaliana na wewe kaka hakuna msafi 100% kila huyu ana lake.
sasa mbaya zaidi, hao wengine ni watu wa hewala hewala lakini huyu Mh. hata kama ana mapungufu lakini ni mtu mchapa kazi, bora huyu kuliko mtu ambaye atakuwa hawezi hata kufungua mdomo kukemea pale panapoharibika.
hao ambao waliopo sasa hivi tumeshuhudia mangapi? Escrow hiyo bado inatikisa na hili ndio jinamizi la kufungia mwaka halijakata roho bado.

Kama tunataka msafi 100% basi tusubiri malaika toka mbinguni waje kutuongoza.
Nawasilisha
 
Halafu as journalist unapopata taarifa hutakiwi kuitoa kwa kuegemea upande mmoja na ushasema ni tetesi mbn km kwa upande mwingine ushaziamini tayari, kwa hiyo hata c wanajaJF unataka tuwe upande upi?
 
Pasco na wenzio naona kama ushabiki wenu kwa EL unataka kuvuka mipaka ya taratibu na kanuni za chama chenu. Hamuoni kuwa kelele zenu kwa siku za hivi karibuni zinaashiria kuwa mnajaribu kukitishia chama chenu kwamba kisithubutu kuliondoa jina la huyo mtu wenu katika kinyang'anyiro cha urais. Hakuna taasisi inayoweza kufaya kazi kwa kutegemea sauti za wapambe kama nyie. Hata hivyo EL siyo kipenzi cha Watanzania zaidi ya nyie mnaofanya yote haya kwa influence ya malipo
 
Wanabodi,

Hii ni tetesi ya habari mbaya kwa wapenzi wa kipenzi cha watu, Waziri Mkuu Mtaafu, Edward Lowassa kuwa pamoja na Mhe. Lowassa kuwa ndie mtu anayekubalika sana kuliko mtu mwingine yoyote ndani ya CCM, wale wasiolitakia mema taifa hili, wamepania kupanga njama za kumhujumu kwa kuhakikisha kuwa jina lake halitaingia hata ndani ya kikao cha CC kujadiliwa!, wamepanga kumchinjia baharini kwenye kamati ya maadili, itakayoyajadili majina wagombea kabla ya kuyaingiza kwenye Kamati Kuu, kujadiliwa!.

Lengo la hujuma hiyo ni kufuatia Lowassa kukubalika kupindukia, jina lake likifika tuu CC, hakuna wa kumkata, hivyo wahafidhina wa CCM, wanaounga mkono kambi ya mmoja wa wagombea, wameapa kuhakikisha jina la Lowassa, halivuki kisingiti cha kamati ya maadili, hivyo kumchinjia rasmi baharini, ili mgombea wao apete kwa mteremko!.

Naomba nisitaje chanzo cha habari hizi, kwa kutumia kanuni ya "the confidentiality of the source"
ila kwa vile hizi ni tetesi tuu, zitakapothibitika ndipo nitaweka source!.

Kama kawaida yetu jf, habari kama hizi ambazo hazijathibitishwa, zimeletwa humu hivi hivi zilivyopokelewa, ili wewe kama mwana jf, be the first to know!, na information is power!, hivyo kutoa fursa kwa wenye uwezo wa kuizuia hii mipango dhalimu inayopangwa, kutaka kuwakosesha Watanzaia mgombea kipenzi chao, chaguo la wengi, na mwenye uwezo usio tia shaka kuyamaliza matatizo yote ya taifa letu Tanzania.

Hii ni thread ya info tip, tuu, hivyo naomba nisiulizwe swali lolote kuhusu hii news tip for your info tuu.

NB. Chama cha Mapinduzi ni taasisi huru yenye uwezo wa kufanya shughuli zake kwa uhuru vile ambavyo wataona wenyewe inafaa, ikiwemo vigezo na jinsi ya kuwachagua wagombea wake, ila kwa sisi ambao ni wakereketwa wa mustakali mwema wa nchi hii, kamwe hatutakubali, kuona watu wenye uwezo na wanaokubalika na wengi, wakienguliwa kwa mizengwe tuu, kitu ambacho CCM imekuwa ikikifanya mara nyingu huko nyuma na labda ni kweli ndicho walichopanga kukifanya mwaka huu!, yaani CCM imekuwa ikiwaengua wagombea wazuri kwa mizengwe na ikabaki salama!, lakini this time, nimewasikia baadhi ya wana CCM kindakindaki, kuwa wamejiapiza, this time CCM ikimuengua chaguo lao kwa mizengwe, patachimbika!.

Pasco
pasco wa jf siku hizi hueleweki,mara ulie na chadema,mara ccm!...,acha wafu wazikane
 
Kwani uko ccm nani msafi when it comes to Ufisadi?
Tena akikatwa jina ndo vzr coz naamini ana watu wengi tu humo ccm ambao ataondoka nao!!!
Lichama liendelee kuvunjika
 
Hivi kaka Pasco unaamini hadi leo kuwa Edward Lowassa atakuwa Rais wa Tanzania? Kwa lipi hasa? Mtakuwa na madodoki na magunzi mangapi kumsafisha? Kuongozwa naye ni pigo kwa nchi na vita dhidi ya ufisadi

Wewe unataka nani awe Rais, ebu tuondolee umasaburi wako hapa
 
Jaman hata EL angekuwa mkweli why asitoboe ukweli wote wa Richmond na hapo ndipo kashfa ya ufisadi itamuepuka lkn anapokaa kimyaa sasa anapokaa kimya anamaanisha nn, mtu anayetaka kugombea nafasi kubwa namna hiyo ya uongozi hlf ana tuhuma kubwa ya ufisadi na hataki kuutolea ufafanuzi wkt alisema angesema Nchi ingekuwa pabaya why asiseme na ni kikubwa gani ambacho anakiepuka km hao anaoogopa kuwataja leo cc tunawaona wasafi tena weupe hata kwa darubini hawana hata kirusi cha ufisadi
 
Back
Top Bottom