JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 3,177
- 7,472
Dar es Salaam, 4 Juni 2025
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimesikitiswa na kinalaani vikali uamuzi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa kuzuia upatikanaji wa mtandao wa kijamii wa X (zamani Twitter), jambo ambalo limethibitishwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Jerry Silaa, kupitia mahojiano ya moja kwa moja kwenye televisheni.
LHRC inaitaka Serikali ya Tanzania kuchukua hatua zifuatazo mara moja:
1. Kurejesha upatikanaji wa Mtandao wa X, Clubhouse, Telegram na majukwaa mengine ya kidijitali yaliyofungiwa.
2. Kuhakikisha uwazi katika mchakato wa udhibiti wa kidijitali na kuwashirikisha wadau katika kuandaa sera za usimamizi wa maudhui zinazoenzi haki za binadamu.
3. Kuheshimu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na mikataba ya kimataifa kuhusu kulinda haki ya kujieleza, kupata taarifa, na uhuru wa kidijitali.
LHRC inatoa wito kwa wananchi, asasi za kiraia, na jamii ya kimataifa kusimama pamoja kwa nguvu moja kutetea na kulinda uhuru wa kidijitali nchini Tanzania
Alichokisema Waziri Silaa, soma hapa ~ Waziri Silaa: X(Twitter) walianza kuruhusu picha za ngono, ukiona hupati kitu mtandaoni uje Serikali inafanya kazi kumlinda mlaji