Lets go deep zaidi in this, as great thnkerz.....!!

Lets go deep zaidi in this, as great thnkerz.....!!

Ibrahim K. Chiki

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2011
Posts
594
Reaction score
163
Kiukweli, leo wana jf naomba tuongee deep zaidi, ni nini hasa kilichosababisha mgogoro wa libya? je walibya wanampinga ghadafi kwa sababu gani hasa? je ni nini kilichochochea machafuko ya libya? je wanaotaka mabadiliko libya ni waaasi au waandamanaji? je ni kufuata mkumbo? na je ni haki ipi hasa wanayoitaka? naomba tuache ushabiki wa kipuuzi na tutoe facts za msingi kama great thnkerz.
 
ngoja waje wachambuzi wa mambo ya kisiasa....... me naweza kuwa bias kidogo!!!!!!!!!!!!
 
Yap, bt if u choose nat to b biasd inawezekena, changia as a great thnker na c kwa ushabiki. gec u cn do that.

Huo ni mkakati tu wa kuifanya Israel ikae kwa raha mustarehe pale mashariki ya kati.
Kwani Saudia ,Bahrain,Qatar Jordan , Iraq zote ziko chini ya USA NA Mshirika wake ISRAEL
. bado ni hizo Libya, Iran na Syria. Tawala hizo tatu zikishaanguka na hao jamaa wakishawaweka
wafuasi waotu . jua basi hakuna vita wala kelelel za vita tena hapo mashariki ya kati.
 
"To really reduce population, quickly, you have to pull all the males into the fighting and you have to kill significant numbers of fertile age females…." The quickest way to reduce population is through famine, like in Africa, or through disease like the Black Death" (Thomas Ferguson - State Department Office of Population Affairs).
 
Ile ni vita ya kiuchumi tu, kinachoendelea pale ni kwamba jamaa wanahitaji mafuta ya libya, na wameshindwa kuyapata chini ya ghadafi, hivyo wanataka wamuondoe wapachike mtu wao . Wale walibya wanaosapoti gadafi kuondolewa wengi wao wamenunuliwa, wengine wanafuata mkumbo na wengine hawana akili ya kuelewa wapowapo tu.
 
waTanzania bwana..Kila siku porojo Libya, Ghana, UGanda...je-discuss maendeleo yenu na nyie basi...lol
wazuri sana kuchambua wenzenu..kujichambua wenyewe kwa wenyewe hamuwezi :ranger:
 
Fukuto dhidi ya Gaddaffi linasababishwa na utawala wake Wa kiimla na jinsi ambavyo yeye na familia yake wameshikilia mhimili wa uchumi wa nchi. Mipango ya badaye ya Ghaddaffi ilikuwa ni kumrithisha mwanaye Islam uongozi wa nchi mara yeye atakapofikia stage ya incompetence. Gaddaffi anawapa wananchi wake elimu bure, matibabu bure pamoja na kuwajengea wazee makazi maalum lakini hiyo fedha haitoki mfukoni mwake bali ni raslimali ambayo mwenyezi Mungu amewapatia Walibya wote waifaidi. Kuwa mwananchi ambaye unalelewa kama kuku kisasa (broiler) kwa kupewa vyakula na malazi wakati Huna uhuru kujieleza, huna nafasi ya kuchagua kiongozi umtakaye, huna uhuru wa kuonyesha uwezo wako wa uongozi inakuwa ni kiini macho.

Yeye Gaddaffi alimpindua mfalme Idris mwaka 1967 na ametawala kwa takriban miaka 42 si awaachie na wengine watawale?
 
Fukuto dhidi ya Gaddaffi linasababishwa na utawala wake Wa kiimla na jinsi ambavyo yeye na familia yake wameshikilia mhimili wa uchumi wa nchi. Mipango ya badaye ya Ghaddaffi ilikuwa ni kumrithisha mwanaye Islam uongozi wa nchi mara yeye atakapofikia stage ya incompetence. Gaddaffi anawapa wananchi wake elimu bure, matibabu bure pamoja na kuwajengea wazee makazi maalum lakini hiyo fedha haitoki mfukoni mwake bali ni raslimali ambayo mwenyezi Mungu amewapatia Walibya wote waifaidi. Kuwa mwananchi ambaye unalelewa kama kuku kisasa (broiler) kwa kupewa vyakula na malazi wakati Huna uhuru kujieleza, huna nafasi ya kuchagua kiongozi umtakaye, huna uhuru wa kuonyesha uwezo wako wa uongozi inakuwa ni kiini macho.

Yeye Gaddaffi alimpindua mfalme Idris mwaka 1967 na ametawala kwa takriban miaka 42 si awaachie na wengine watawale?


Stuxnet hio ni moja tu ya assumptions katika ma assumptions kibao... Naamini kua umepitia yoote, na katika yote hayo umeona hii ndo inanguvu. OK I respect that ... but moja ya inchi ambao inajimejihusisha katika hayo mashambulizi ni Britain, utawala walo nao umechukua miaka zaidi ya 300, na kiongozi anarithi toka ndani ya family. Kwanini waon unaona nisawa kuvamia mtu ambae ame reign kwa miaka 41 tu???
 
waTanzania bwana..Kila siku porojo Libya, Ghana, UGanda...je-discuss maendeleo yenu na nyie basi...lol
wazuri sana kuchambua wenzenu..kujichambua wenyewe kwa wenyewe hamuwezi :ranger:


LOL... Ya kwetu yametushinda... kila mtu anaficha sura na jina... Hakuna hope yet, na tukitafakari saana waweza kuta unataka kujifia huko.. Nani anataka kufa?? Hakuna, na ushahidi ni idadi ya watu walotibiwa/wanaotibiwa/wataotibiwa kwa kikombe...
 
Huo ni mkakati tu wa kuifanya Israel ikae kwa raha mustarehe pale mashariki ya kati.
Kwani Saudia ,Bahrain,Qatar Jordan , Iraq zote ziko chini ya USA NA Mshirika wake ISRAEL
. bado ni hizo Libya, Iran na Syria. Tawala hizo tatu zikishaanguka na hao jamaa wakishawaweka
wafuasi waotu . jua basi hakuna vita wala kelelel za vita tena hapo mashariki ya kati.

Hata kama Libya na Israel ni mahasimu je unadhani Israel hakuwa anastarehe kwa ajili yake!?hivi inatosha kuwa sababu?
 
naungana na mawazo kuwa walibya walishamchoka ghadafi. nadhani Qadaffi alikosea exit strategy. angeyaona mapema yasingetokea haya yote na angejiandaa vizuri zaidi. tatizo lake alikuwa anazidi kupata picha ya kutawala zaidi na eneo kubwa zaidi eg afrika nzima. anyway hayo ni ya kwake. kwamba kutolewa kwa huduma za kijamii bure hiyo haiwezi kuwafanya walibya wasitake kuona mtawala tofauti. ni hulka ya mtu kumchoka mtawala huyohuyo kila siku kwa nchi ambayo c ya kifalme.

nikiwazacho mimi, waandamanaji hawakuwa na mkakati mwingine zaidi ya kuendelea kuandamana, kama walivyofanya majirani wa tunisia na misri. ghadaffi alijua kuwa akiwaachia hivyo watamwondoa kwani angekuwa defenceless. waandamani wa amani hutawanywa kwa mabomu ya machozi na maji ya kuwasha. ila hiyo haiwazuii kurudi tena kesho. so yeye akataka kuwafunza adabu wasirudi kesho. ndo hapo alipoanza kutumia ndege za kivita na vifaru kuwafunza adabu. na ili kuleta uhalali, akawavuta wakimbilie kwenye kambi ya jeshi na kuitena na kuchukua silaha uchwara zisizo na madhara makubwa. na kwa vile watakuwa na silaha, sasa hawa hawawezi kuwa waandamani wa amani, bali insurgents. so hapo ni vita kwa vita. kama mkakati wa kivita, akayaamuru majeshi yake yawe yana retreat kurudi westwards towards tripoli ili hawa 'insurgents' waone wanapata ushindi mkubwa na wa haraka. hapo ndo kiama kilipowakuta walipokaribia sirte (kwao Ghadafi). walipewa kibano na kurudishwa kule walikotoka. na kama sio interference za nato sasa hizi wapinzani wangeshavushwa mpaka na misrata kurudi kwa ghadaffi. hii ni tafsiri yangu ya kinachoendelea libya.

binafsi siamini sana kuwa yanaoendelea ndani ya nchi za kiarabu ni influence ya israel USA etc. nadhani kwa mara ya kwanza tumeona waarabu wakiandamana bila ya kuchoma bendera za israel au nchi za magharibi. hii inaonesha kuwa masuala yao ni ya ndani ya nchi zao wenyewe tofauti na propaganda kuwa wanasukumwa na mataifa ya nje (magharibi). in fact mara nyingi mataifa ya magharibi huwa tayari yana kiongozi mbadala ambaye atakuja baada ya kutoka yule wasiyemtaka. hali ni tofauti kidogo na ilivyotokea kwa mataifa ya uarabuni. tz misri mpaka leo ni jeshi linatawala, likijiandaa kurudisha utawala kwa raia. angekuwepo mtu tayari huyo ndo angechukua nchi waqt akiandaa uchaguzi etc.
 
Back
Top Bottom