Leticia Nyerere atimkia CCM

Leticia Nyerere atimkia CCM

Mapengo 17

R I P
Joined
Mar 28, 2014
Posts
1,228
Reaction score
618
Nimepata taarifa kutoka kwa mmoja wa rafiki zangu aliyepo Dar es Salaam, ameniambia kwamba Mbunge wa Viti Maalum Chadema, Leticia Nyerere, amehamia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Tangu awali mbunge huyo alisakamwa na maneno mengi kutoka kwa viongozi wa Chadema akiwemo kwamba aachane na ubunge ndani ya Chadema ili ajiunge na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuliko kuendelea kukipigia debe chama hicho akiwa upinzani.

Hata hivyo, mbunge huyo anadaiwa kufanya matendo ya kujipendekeza kwa CCM kabla ya kujiengua na chama chake cha awali.

Leticia.jpg

Mbunge wa Viti maalumu Chadema mkoani Mara, Leticia Nyerere, (katikati) akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dar es Salaam jana kuhusu kuhama kutoka chama chake cha chadema na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kulia ni mtoto wake,Helena Nyerere na Julia Nyerere.
 
Makongoro Nyerere alimwabia aache kulitumia jina la Nyerere ndo maana kaamua aende ccm
 
Huyu dada anaenda kutumika tu huko CCM.
Hakuna jipya atakalopata na sana sana hata ubunge hatapata.
 
Hana jipya huyo.kama wabunge kamili wameondoka lakn tupo imara.huyo aendn tu hana madhara kwetu.
 
Ivi Leticia nyerere ni NANI? Alisoma wapi na kwanini chadema walimpa ubunge ? Nisaidie wadau
 
Hbari ya Mjini kwa sasa ni CDM, UKAWA na Lowasa ............ wengine sidhani kama watapata media coverage kwa sasa. Huoni hata Magufuli kwa sasa hasikiki na wala hajulikani yuko wapi kwa sasa!!
 
Leticia Nyerere kuhamia chadema wamejenga uadui na familia ya Nyerere. watakosa kura za Mkoa Wa Mara kwani Leticia ana nguvu kule.
 
Kweli nimeamini hakuna anayemwamini Zitto Kabwe.Said Arfi kagoma kwenda ACT,Shibuda hataki kusikia jina la Zitto huyu bi Pekupeku Leticia karudi nyumbani sasa wale wabunge 50 aliodai watajiunga ACT walikuwa ni maruani au majini ya Kigoma Mwandiga.
 
Ni vema amerudi akasaidiane na binti yake... bila kumsahau shemeji yake Maco.. Sasa itajulikana, je CCM na ukoo wa Nyerere wapo pamoja na hizo siasa za wanaCCM za wakati huu?
 
Back
Top Bottom