Leo zamani (kabrasha la kumbukumbu)

Leo zamani (kabrasha la kumbukumbu)

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,644
Reaction score
860,887
Tunaanza rasmi leo tarehe 9/9/2016

Kila siku ina tukio lake kwenye historia ya dunia...nilitamani siku nyingi tuwe na kitu kama hiki kama ilivyo kwa redio Tumaini...kule photos kuna kitu kama hiki kinatukumbusha mengi sana...lakini kwenye habari za kawaida hatuna

Nitajitahidi kwa kadiri ya uwezo wangu kuweka kila siku matukio yaliyotokea tarehe na mwezi kama leo

1:9/9/1990 ndio ilikuwa siku ambayo alipinduliwa na kuuwawa kikatili aliyekuwa rais wa Liberia marehemu Samuel Doe

Matukio mengine ya tarehe ya leo -kumbukumbu ya kifo cha Mao zhe Dong rais wa china mwaka 1976

-Kuzaliwa kwa James Siang'a raia wa Kenya aliyekuwa kocha maarufu wa Simba

☆☆☆Kesho nitaendelea nakaribisha na wengine pia wanaopenda historia waweke matukio wanayoyajua
 
1473396627393.jpg
James Siang'a
1473396638251.jpg
Samuel Doe
1473396656519.jpg
Mao dze Dong
 
Safi sana, mkuu hii ungeweka kama uzi maalumu wa kumbukumbu ya matukio duniani
 
Mkuu nimependa wazo lako!Hii itatufanya tulete hapa kumbukumbu za mambo mengi sana
Kila siku ina tukio lake kwenye historia ya dunia...nilitamani siku nyingi tuwe na kitu kama hiki kama ilivyo kwa redio Tumaini...kule photos kuna kitu kama hiki kinatukumbusha mengi sana...lakini kwenye habari za kawaida hatuna
Nitajitahidi kwa kadiri ya uwezo wangu kuweka kila siku matukio yaliyotokea tarehe na mwezi kama leo
9/9/1990 ndio ilikuwa siku ambayo alipinduliwa na kuuwawa kikatili aliyekuwa rais wa Liberia marehemu Samuel Doe
Matukio mengine ya tarehe ya leo -kumbukumbu ya kifo cha Mao zhe Dong rais wa china mwaka 1976
-Kuzaliwa kwa James Siang'a raia wa Kenya aliyekuwa kocha maarufu wa Simba

☆☆☆Kesho nitaendelea nakaribisha na wengine pia wanaopenda historia waweke matukio wanayoyajua
 
2: leo ni tarehe 10-09
1968 rais wa Malawi Hastings Kamuzu Banda adai baadhi ya maeneo ya Tanzania ni ya Malawi na akatishia kuyachafua mojawapo ya maeneo hayo ni Tukuyu
1846 mvumbuzi wa cherehani bwana Howe aruhusu watu wengine watengene cherahani
Mojawapo aliyepata ruhusa hiyo ni bwana SINGER ambaye vyerehani vyake ni maarufu mpaka leo
Leo ni uhuru wa Guinea Bissau mwaka 1973 nchi ndogo ya Afrika wakati huo ikiwa na wakazi takriban milioni moja
 
Dr. Hastings Kamuzu Banda aka rais wa muyaya (rais wa maisha)
1473481835476.jpg
1473481980597.jpg
alitawala Malawi 1961-1994 na alifariki November 25 mwaka 1997 South Africa
 
Back
Top Bottom