Kwanini YESU alifunga? Kwa nini sisi tunafunga? Kuna uhusiano gani katika kufunga kwa YESU siku 40 na majilio ya pasaka? Je Pasaka ililetwa na YESU au ilikuwepo kabla?
...somo: Kumbukumbu 26:4-10; Warumi 10:8-13; Luka 4:1-13
tunaanza rasmi ni wakati wa Kwaresima ambapo tunapata nafasi kumtolea Mungu zile siku arobaini kama njia ya kumshukuru kwa ajili ya huruma na ukombozi wake katika Mwanae Yesu Kristo. Pia wakati huu Kanisa latupatia nafasi ya kufanya toba, na hivyo kabla ya Jumapili hii tunapakwa majivu usoni ili kuungama adharani udhaifu wetu, na kukubali mwaliko wa Kanisa kufanya kitubio, tukiwa tayari kwa neema ya Mungu kumshinda Shetani.
Basi wakati huu wa Kwaresima tunaitwa kumuiga Kristo aliyemshinda Shetani kwa kifo na ufufuko wake.
Kwenye Injili, tunasikiliza habari ya Yesu akiongozwa na Roho njangwani ambapo anajaribiwa mara tatu na Shetani.
Majaribio yenyewe na msimamo wa Yesu ni mfano mkubwa kwetu sisi. Lengo la majaribio hayo ni kutusaidia kuelewa jinsi Yesu anapinga kila jaribio.
Yesu anakataa kutawaliwa na njaa na hivyo anaepuka kishawishi cha kutumia uwezo wa Ki-Mungu ili ageuze jiwe liwe mkate.
Anakataa pia kutumia njia ya mkato ya kuwaakikisha watu kwamba yeye kweli ni Mwana wa Mungu.
Majaribio ya Yesu jangwani yatusaidia kuona kwamba Yesu aliyashinda kwa kukubali kuishi chini ya matakwa ya Baba, badala ya kukubali kushindwa na tamaa zake binafsi.
Yesu alishinda majaribio hayo kwa sababu aliishi kikamilifu maisha ya ki-roho, na hivyo akaweza kuzuia tamaa za ki-mwili kutomtawala. Ingekuwa rahisi sana kuruka kutoka kwa mnara wa Hekalu. Kitendo hicho kingewaakikisha watu kwamba yeye ni Mwana wa Mungu, lakini Yesu alishinda jaribio hilo.
Tunapoanza wakati huu wa Kwaresima, majaribio ya Yesu na jinsi aliyashinda yawe kwetu mfano tungefuata. Ikiwa tungetaka kumfuata Yesu kwa uaminifu na utiifu, lazima tuweke kando wakati ambao tungeweza kuwa peke jangwani ili tutafakari umaana wa wito wetu kama wafuasi wake; wakati tungeomba Mungu msaada wake na nguvu za neema yake.
Kwaresima ni wakati tunapogudua huruma na msamaha wa Mungu katika Mwanae Yesu;
Kama Yesu tuwe tayari kupambana na majaribio.
Tukimwamini Yesu na kuishi katika Roho wake, hata sisi pia tutashinda vishawishi hata ingawa ni vikali.
Kwaresima ni wakati tunapoitika wito wa Mungu kujuta dhambi zetu na kugeuka kabisa na kuwa wapya maishani mwetu.