Leo nimekumbuka kesi ya Ukiwaona Ditopile Mzuzuri, ilipelekea mahabusu kugoma kwenda mahakamani siku tano Dar wakidai dhamana yake ifutwe

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,447
7,831
Katika suala lililoitikisa fani ya sheria na utoaji haki ni tukio la miaka 17 iliyopita kutokana na mlolongo wa matukio yaliyojiri baada ya kufunguliwa mashitaka ya mauaji kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora wa wakati huo, Ukiwaona Ditople Mzuzuri baada kumpiga risasi dereva wa daladala, Hassan Mbonde (33) mwaka 2006.

Pia, soma=> Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

Kesi ya mshitakiwa huyo ilisababisha mahabusu katika magereza ya Dar es Salaam na kwingineko, kugoma kuingia kwenye magari kwenda mahakamani kwa ajili ya kusikilizwa kesi zao. Mgomo huo wa siku tano haukuwahi kutokea nchini.

Upelelezi wa kesi dhidi ya Ditopile ulichukua miezi minne tu hadi mashitaka kubadilishwa kutoka mauaji ya kukusudia na kuwa mauaji ya kutokusudia, na hivyo kupewa dhamana.

Hilo liliwakasirisha sana mahabusu wengine waliokuwa wakingojea kesi zao (pamoja na zile kesi za mauaji), ambazo baadhi yao walikuwa mahabusu kwa miaka kadha. Walitaka nao wafanyiwe uharaka wa namna hiyo katika kuchunguza kesi zao, la sivyo dhamana ya Ditopile ifutwe.

dito.0.jpg

Askari kanzu wakimpeleka Athumani Ukiwaona Ditopile Mzuzuri lupango mara baada ya kusomewa shtaka la mauaji mbele ya hakimu mkazi, Michael Lugulu mahakama ya Kisutu November 06, 2006.​


Kesi ya Ditopile ili-trend kwa matukio mengi ikiwemo ndugu wa Ditopile kuwarushia maneno na kuwafanyia vurugu ikiwemo kuwamwagia maji waandishi wa habari waliokuwa wanafatilia kesi hiyo kwa madai ya 'kuishikia bango'. Baada ya tukio hilo kesi ya Ditopile ilitawala 'Front Page' zote za magazeti makubwa na prime ya TV stations 'waandishi wakilipa kisasi'

Pia kapteni Ditopile akiwa mahabusu, alipata bahati ya kutembelewa na Rais aliye madarakani wakati huo, Jakaya Kikwete akisema ni rafiki yake wa siku nyingi.

Ndani ya miezi minne uchunguzi ulikamilika na kesi yake ikabadilishwa kutoka mauaji ya kukusudia kwenda mauaji bila kukusudia.

Baada ya kesi kubadilishwa, Ditopile alitoka nje kwa dhamana.

images (26).jpeg

Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakimfariji mjane wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Marehemu Ukiwaona Ditopile Mzuzuri huko nyumbani kwake Upanga. Kulia ni Mariam Ditopile mtoto wa marehemu na nyuma ya Rais ni mtoto wa Rais, Rashid Chodo Kikwete.(April 21, 2008)

Hata hivyo, mwaka 2008 ikiwa bado kesi yake haijapata hukumu, kapteni Ditopile aliaga dunia katika hoteli ya Hilux mkoani Morogoro akiwa na mke Mdogo. Sababu ilitajwa kuwa mshtuko wa moyo.

Pia, Soma=> Ukiwaona Ditopile afariki dunia
 
Katika suala lililoitikisa fani ya sheria na utoaji haki ni tukio la miaka 17 iliyopita kutokana na mlolongo wa matukio yaliyojiri baada ya kufunguliwa mashitaka ya mauaji kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora wa wakati huo, Ukiwaona Ditople Mzuzuri baada kumpiga risasi dereva wa daladala, Hassan Mbonde (33) mwaka 2006.

Pia, soma=> Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

Kesi ya mshitakiwa huyo ilisababisha mahabusu katika magereza ya Dar es Salaam na kwingineko, kugoma kuingia kwenye magari kwenda mahakamani kwa ajili ya kusikilizwa kesi zao. Mgomo huo wa siku tano haukuwahi kutokea nchini.

Upelelezi wa kesi dhidi ya Ditopile ulichukua miezi minne tu hadi mashitaka kubadilishwa kutoka mauaji ya kukusudia na kuwa mauaji ya kutokusudia, na hivyo kupewa dhamana.

Hilo liliwakasirisha sana mahabusu wengine waliokuwa wakingojea kesi zao (pamoja na zile kesi za mauaji), ambazo baadhi yao walikuwa mahabusu kwa miaka kadha. Walitaka nao wafanyiwe uharaka wa namna hiyo katika kuchunguza kesi zao, la sivyo dhamana ya Ditopile ifutwe.

Kesi ya Ditopile ili-trend kwa matukio mengi ikiwemo ndugu wa Ditopile kuwarushia maneno na kuwafanyia vurugu ikiwemo kuwamwagia maji waandishi wa habari waliokuwa wanafatilia kesi hiyo kwa madai ya 'kuishikia bango'. Baada ya tukio hilo kesi ya Ditopile itawala 'Front Page' zote za magazeti makubwa na prime ya TV stations 'waandishi wakilipa kisasi'

Pia kapteni Ditopile akiwa mahabusu, alipata bahati ya kutembelewa na Rais aliye madarakani wakati huo, Jakaya Kikwete akisema ni rafiki yake wa siku nyingi.

Nimesahau hukumu ilivyokuwa lakini miaka miwili baadae(2008), kapteni Ditopile aliaga dunia katika hoteli ya Hilux mkoani Morogoro akiwa na mke Mdogo.
Ukiwaona Omar Ramadhan Mwinshehe Ditopile Mzuzuri.

Jamaa kama sikosei ndio alieanzisha style ya mtuhumiwa kuingia mahakamani ukiwa umejifunika uso.
 
Katika suala lililoitikisa fani ya sheria na utoaji haki ni tukio la miaka 17 iliyopita kutokana na mlolongo wa matukio yaliyojiri baada ya kufunguliwa mashitaka ya mauaji kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora wa wakati huo, Ukiwaona Ditople Mzuzuri baada kumpiga risasi dereva wa daladala, Hassan Mbonde (33) mwaka 2006.

Pia, soma=> Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

Kesi ya mshitakiwa huyo ilisababisha mahabusu katika magereza ya Dar es Salaam na kwingineko, kugoma kuingia kwenye magari kwenda mahakamani kwa ajili ya kusikilizwa kesi zao. Mgomo huo wa siku tano haukuwahi kutokea nchini.

Upelelezi wa kesi dhidi ya Ditopile ulichukua miezi minne tu hadi mashitaka kubadilishwa kutoka mauaji ya kukusudia na kuwa mauaji ya kutokusudia, na hivyo kupewa dhamana.

Hilo liliwakasirisha sana mahabusu wengine waliokuwa wakingojea kesi zao (pamoja na zile kesi za mauaji), ambazo baadhi yao walikuwa mahabusu kwa miaka kadha. Walitaka nao wafanyiwe uharaka wa namna hiyo katika kuchunguza kesi zao, la sivyo dhamana ya Ditopile ifutwe.

Kesi ya Ditopile ili-trend kwa matukio mengi ikiwemo ndugu wa Ditopile kuwarushia maneno na kuwafanyia vurugu ikiwemo kuwamwagia maji waandishi wa habari waliokuwa wanafatilia kesi hiyo kwa madai ya 'kuishikia bango'. Baada ya tukio hilo kesi ya Ditopile itawala 'Front Page' zote za magazeti makubwa na prime ya TV stations 'waandishi wakilipa kisasi'

Pia kapteni Ditopile akiwa mahabusu, alipata bahati ya kutembelewa na Rais aliye madarakani wakati huo, Jakaya Kikwete akisema ni rafiki yake wa siku nyingi.

Nimesahau hukumu ilivyokuwa lakini miaka miwili baadae(2008), kapteni Ditopile aliaga dunia katika hoteli ya Hilux mkoani Morogoro akiwa na mke Mdogo.
Ditopile na Jakaya ni washikaji miaka hiyo, ni watoto wa mjini na ni watu wa Ilala ndiyo Dar es Salaam
 
Ile kesi ilikuwa na mafunzo mengi sana kwa viongozi wa Serikali. Kwamba cheo ni dhamana. Kiburi si Uungwana. Pamoja na madaraka yote uliyonayo, hauna haki ya kutoa uhai wa mtu, kwa sababu tu gari yako imegongwa, na gari yenyewe imenunuliwa kwa pesa za walipa kodi.

Halafu gari yenyewe Ina insurance fully covered. Asubuhi yake angepewa gari nyingine. Lakini kwa kulewa madaraka akajisahau. Ubongo wa yule dogo ukamwagwa.

Raisi mstahafu, pamoja na shutuma nyingi anazopewa, hapa ndipo alipoonyesha ukomavu wa akili; kwamba umeua mtu asiye na hatia, basi tuache sheria ichukue mkondo wake. Ushkaji tuweke pembeni.

Ile ilikuwa bab kubwa. Na jela akaenda kumtembelea. Kwamba, yeye Rais Kikwete na mtuhumiwa wametoka mbali sana (damudamu) lakini suala la kumua yule kijana litaamuluwa na mahakama. That was really cool .
 
Kwa hivyo unataka kusema nini baada ya Mbunge Ditto.. kutaka wapinga DP World wadhibitiwe?
Au unamkumbusha kuwa makini na mdomo wake asije kuamsha hasira za raia juu ya kumbukumbu mbaya za familia yao?
Ditopile alishafariki mkuu
 
Back
Top Bottom