Leo nimekumbuka Enzi ya simu za kuomba kwa operator na Barua Bila Stamp!

Leo nimekumbuka Enzi ya simu za kuomba kwa operator na Barua Bila Stamp!

Kimwakaleli

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2018
Posts
12,212
Reaction score
17,005
Habari Wana JF,Miaka ya nyuma huko1960.......1990,Tuliokuwepo, unaenda posta unakoroga simu kwa operator,anskuitikia unataka namba baadae anakuunganisha unaongea na kutumbukiza hela ya muda wa Maongezi .
Kama huna hela unasema reverse call,akikubali unayempigia kwamba itaingia kwenye bill yake,tunaanza kuongea,kimbembe akikutolea nje!Huna budi kurudi mtupu na ujumbe wako kichwani!

La pili ni hili la barua,huna stamp unaituma hivyohivyo! Mwenye jina anapelekewa karatasi ya kuonyesha kuna jambo lake,Akienda anakutana na Madai ya stamp!Analipa na kupewa barua.

Hii Leo imenikumbusha mbali kuna barua,nimeambiwa Lazima ipitie posta na nilishasahau mambo ya posta,Enzi hizo stamp Senti Tano,Kumi, Hamsini,Sasa hivi elfu,elfu mbili hadi Tano kutegemeana na inakoenda.
Mlikuwa Enzi hizo mnakimbuka Nini?Siku hizi kila kitu kama kiganja Cha mkono!
 
Umenikumbusha mbali sana me hii huduma nimeitumia mno kuwasiliana na mshua na mpk leo no yetu ya simu naikumbuka😂😂🔥
 
Umenikumbusha mbali sana me hii huduma nimeitumia mno kuwasiliana na mshua na mpk leo no yetu ya simu naikumbuka😂😂🔥
Mimi Nakumbuka ya uncle mpaka Sasa anayo, alikuwa anakataa hizi za mkononi!Tukamsajilia kinguvu ndo kaanza kuzoea hizi smartphone,baada ya kuona Zina Mambo mengi.
 
Back
Top Bottom