Papa Mobimba
JF-Expert Member
- Dec 6, 2018
- 1,153
- 1,359
Kwanza ningependa kuwapa hongera watu wote walioamua kwenda kupima bila kujali majibu yalikuwaje. Kwa kweli kitendo cha kuamua kwenda kupima ni ujasiri wa hali. Mimi sikuwahi kuupata ujasiri huo mpaka mama alipotishia kuwa kama tusingeende kupima basi angesitisha huduma.
Sikuwa na jinsi ya kufanya, siku mbili hizi nimekuwa nawaza sana. Sasa leo nikasema ngoja nijipeleke mwenyewe kwanza. Ili nijue afya yangu kabla mama hajanipeleka kwa nguvu atakapogomea kutoa huduma.
Nikaenda hospitali. Nilipofika nikamwambia yule mhudumu. Nimekuja kupima kwa utashi na hiyari yangu mwenyewe. Najua kuna majibu ya aina mbili. Sitaki maelezo yoyote mengine naomba nipime. Jamaa akanielewa akanitoba akatoa damu. Sio siri nilitetemeka wakati nasubiri majibu. Nikasikia harufu ya kikwapa wakati asubuhi nilipaka deodorant. Dakika tano hizi nilikuwa kwenye hali ngumu sana.
Niliwaza mademu wote niliowahi kukutana nao. Baadae nikajipa moyo mbona kuna watu wanaishi na maambukizi. Mimi sitakuwa wa kwanza. Mhudumu akanistua. "Uko tayari kwa majibu yako". Hapo ndipo nilisikia harufu zaidi ya kikwapa. Midomo ikakauka. Nikajikamua. Nikamjibu "Ndio maana nimekuja kupima".
"Hauna HIV. HAUNA UKIMWI". Nikamuangalia. Nikashusha pumzi kwa nguvu. Nikamjibu. Asante sana. Nimetoka hapo nikajipongeza kwa Mirinda ya baridiiii.
Sasa nikirudi home. Nitamwambia wife, achague twende tupime wapi. Aseme mwenyewe. Nitajifanya sijapima. I hope na yeye atakuwa poa. Pengine amekwisha pima ndio maana kaanza figisu figusu. Nitawapa mrejesho.
Sikuwa na jinsi ya kufanya, siku mbili hizi nimekuwa nawaza sana. Sasa leo nikasema ngoja nijipeleke mwenyewe kwanza. Ili nijue afya yangu kabla mama hajanipeleka kwa nguvu atakapogomea kutoa huduma.
Nikaenda hospitali. Nilipofika nikamwambia yule mhudumu. Nimekuja kupima kwa utashi na hiyari yangu mwenyewe. Najua kuna majibu ya aina mbili. Sitaki maelezo yoyote mengine naomba nipime. Jamaa akanielewa akanitoba akatoa damu. Sio siri nilitetemeka wakati nasubiri majibu. Nikasikia harufu ya kikwapa wakati asubuhi nilipaka deodorant. Dakika tano hizi nilikuwa kwenye hali ngumu sana.
Niliwaza mademu wote niliowahi kukutana nao. Baadae nikajipa moyo mbona kuna watu wanaishi na maambukizi. Mimi sitakuwa wa kwanza. Mhudumu akanistua. "Uko tayari kwa majibu yako". Hapo ndipo nilisikia harufu zaidi ya kikwapa. Midomo ikakauka. Nikajikamua. Nikamjibu "Ndio maana nimekuja kupima".
"Hauna HIV. HAUNA UKIMWI". Nikamuangalia. Nikashusha pumzi kwa nguvu. Nikamjibu. Asante sana. Nimetoka hapo nikajipongeza kwa Mirinda ya baridiiii.
Sasa nikirudi home. Nitamwambia wife, achague twende tupime wapi. Aseme mwenyewe. Nitajifanya sijapima. I hope na yeye atakuwa poa. Pengine amekwisha pima ndio maana kaanza figisu figusu. Nitawapa mrejesho.
