Leo matapeli wa simu wamechachamaa

MASOLWA WEWE NA MWENZIO KALANGASA MNANIHESHIMU MIMI BABU YENU MLIKUJA NIKAWAPA NDAGU ISIYO NA MAKAFARA MKAFUATA MASHARTI MKAPATA UTAJIRI MKAJA KUNISHUKURU ILA NASIKITIKA SANA YULE NDUGU YAKO WA BUKOBA NIMEMPA NDAGU AKIWA MBALI KAPATA MALI HANIJUI SIMJUI HATAKI KUJA KUNIONA ANANITUMIA TU PESA ASIZANI MAGARI NA MAJUMBA KAFIKA ANAWEZA BAKI BILA KITU NA WEWE BADILISHA DAWA KWENYE MAGARI NIPIGIE NIKUPE MAELEKEZO

nimetumiwa hii Mimi
 
MASOLWA WEWE NA MWENZIO KALANGASA MNANIHESHIMU MIMI BABU YENU MLIKUJA NIKAWAPA NDAGU ISIYO NA MAKAFARA MKAFUATA MASHARTI MKAPATA UTAJIRI MKAJA KUNISHUKURU ILA NASIKITIKA SANA YULE NDUGU YAKO WA BUKOBA NIMEMPA NDAGU AKIWA MBALI KAPATA MALI HANIJUI SIMJUI HATAKI KUJA KUNIONA ANANITUMIA TU PESA ASIZANI MAGARI NA MAJUMBA KAFIKA ANAWEZA BAKI BILA KITU NA WEWE BADILISHA DAWA KWENYE MAGARI NIPIGIE NIKUPE MAELEKEZO
Nimetumiwa hii
 
Kuna ambao nawafahamu na wanaishi mtaa wanyuma kwa gff wangu. Huwa wanapigia watu na kujifanya customer care kuwaambia umeshinda bonus then kupata hiyo bonus kuna namba za kuingiza na kwenye simu uwe na salio ukukubali tu imekula kwako. Kuna siku hata mimi nilipigiwa nilistuka mapema na kupiga namba ya customer care wakasema namba sio yao nikawaambia basi ni tapeli huyo wanasema inabidi nikatoe taarifa polis nikaona wajinga hawa nawapa namba za matapeli then nikatoe taarifa ofisini.
 
Mbona yangu hai trace eneo?
 
Mjukuu wangu ndagu niliyokukabizi hiyo uwe makini na pesa hizo zinazokuja usiogope ndio mafanikio yako si nilikwambia utafanikiwa kwa mda mfupi sasa umeona mwenyewe na siri hiyo usitowe kwa mtu yoyote unipigie nikuelekeze.-0746656038
 
Hata Mimi nmemjibu utumbo hajawah uonaaaa[emoji23] [emoji23] [emoji23] et xmass grant hiiiiiii
 
Vyuma vimekaza watu hawana hela za kwenda hta kwa mganga hakuna hela ya kuchzea now dayz
 
Mie juzi katika mtandao mmoja kuna ID ya mwana DADA mashauri mjini anauliza maswali ukijibu anasema anakupa zawadi simu ya Iphone, nikajibu akaja inbox akaniambia nitume namba yangu ya simu kisha atampa mhasibu wake ili nimtumie 20,000/- ili alipie TRA ndio wanipe zawadi yangu, duh nikauliza sasa ni zawadi au ?? nikaumbulia matusi
 
Mbona yangu hai trace eneo?
Hata yangu inaonesha eneo nilipo mimi tu (sms na calls)
Nimejitahidi sana kubadili lakini kila ninayodownload ni hivyo hivyo
Mimi nimetumiwa hii, Mjukuu wangu ile dawa iko tiyari dawa ya kumvuta aliye mbali pete ya bahati, utajiri wa haraka, masomo, biashara na zindiko la nyumba. No 0624964853
 
Mkuu hatari sana hawa viumbe waje na mbinu nyingine hii imeshndkana
 
Mkuu pole sana kwa kukosa zawad toka kwa mlimbwende tutajie bas ni nan c o sepenga huyoo
 
Mie nimepigiwa kutoka biko sport kuwa nimeingia kwenye droo ya kwenda kutizama mechi live Uingereza, nimemskiliza wee akaona sina wenge akaamua akate simu.
 
ABARI ZA LEO NDUGU YANGU ILE NAFASI YA JESHI ULIYONIOMBA IMEPATIKANA KAMA UPO TAYALI TUWASILIANE
Namvutiaga tu pumzi huyu
 
Tapeli mwingine ndiyo kamaliza kunipigia akijifanya kuwa yeye ni mtu wa customer care wa tigo na kuwa nimepewa bonus ya sh, 195,000/= kwa kile alichoeleza kuwa ni kutokana na kuwa mtumiaji mzuri wa tigo pesa, hivyo aliniuliza kama nina shilingi ngapi kwenye tigo pesa na kumjulisha kuwa nina balance ya Milioni mbili. Mara baada ya kumjulisha hivyo akaniambia ngoja atume. Mpaka sasa sijapokea bonus yangu. Kwa yeyote anayeweza tusaidiane kumtafuta huyu tapeli maana ninapo jaribu kupiga namba yake inaita tu, hivyo naomba tusaidiane kwa kutumia namba hii ili nitumiwe bonus yangu namba: 0678773177
 
Leo kweli wameamua mwingine huyu......

Your mobile number has been Awarded 960,000 Euros in the 2017 Toyota Xmas Award Grants. To receive, contact Dr. Marcus via email: toyotaxmasgrants@gmail.com


nilichomjibu siri yangu.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] mkuu hata mm nimepokea msg hii kama lisaa limoja lililopita [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…