Leo 5/11/2017 naacha pombe rasmi

273

Member
Sep 12, 2017
63
82
Salam zenu wakuu,

Kama kichwa kinavyojieleza,

Ndugu zangu nimefikia uamuzi huu kutokana na ushauri mfupi na mzito kutoka kwa kaka yangu na pia kwa kuwa naona nafsi inamsuta sana.

Niseme tu nimeamua kuchana na pombe kutokana na sababu zifuatazo;
1. Ni kinyume na mafundisho ya kiimani.

2. Tangu nianze kunywa huu ni mwaka wa 5 sioni faida yoyote zaidi ya hasara kama za kupoteza simu, kupoteza pesa, kupoteza heshima, kupoteza baadhi wa watu wa msingi na sana sana kupoteza utu wangu.

3. Natokea familia ya kimasikini sana hivyo naona kuendelea kunywa pombe na kama naisaliti familia yangu.

4. Nimetathmini kuwa kuendelea kunywa pombe ni kuisaliti nafsi yangu, kumsaliti "my future wife" na pia kuwasaliti wanangu ambao bado wapo kiunoni mwangu (nitapoteza sifa mojawapo ya kuwa baba bora)

Kiufupi sioni faida za kuendelea kunywa pombe, naacha kunywa pombe rasmi hivyo ndgu zngu naomba mnikumbuke ktk sala.

Zaidi zaidi nipo mbioni kuachana na anasa nyingine ya kupenda wanawake, changamoto kubwa ktk hili ni kuwa sijawahi kukutana na mwanamke aliye commited(naweza kumpenda kwa dhati ila akaja kunitenda baadae) hivyo nakua sipo commited to a girl i be with, ila naamini yupo mmoja nilieandaliwa na Mungu na nitakutana nae tu naamini katika kipindi kifupi kijacho tujenge maisha.

Kwaheri pombe niilikupenda sana sana tena sana lakini mahala salama pamenipenda zaidi.
 
sijaiona sababu ya msingi hata moja we jamaa imani yenyewe tunafundishwa mpe pombe mwenye shida asahau shida zake unadhan Mungu hajui ok na hizo sababu nyingine nazo hazina mashiko mbona TBl wamevunja bei we unataka kuacha /unaleft where are you lefting to??
 
Ati ulishauriwa na kaka yako Daaah we acha zako bhana mimi nina miaka 37 sasa hivi ila nachoamini huwezi kuacha bia Kwa kushauriwa na mtu bali wewe mwenyewe uamue hata anasa nyingine ni mpaka we mwenyewe uamue kuacha
 
Nafurahi kuona kuwa umefika wakati muafaka na sababu sahihi za kuacha pombe...

uonapo unakwama au vishawishi vya kuacha vinakuzidia karibu pm nitakupa mbinu za kushinda majaribu na utafanikiwa.

Ila tambua hatua uliyochukuwa ni rahisi kutamka ila ngumu kutekeleza kwa vitendo.

Endele kumwomba mungu akupe ujasiri wa kutimiza azma yako njema.
 
Mkuu huoni kama unaenda kinyume na Sera ya mkulu "VIWANDA" huoni kuwa watu wote wakifanya maamuzi kama yako viwanda vya bia vitakufa.!!!
 
Kupata moja au mbili sio mbaya kama kipato kinaruhusu, kumbuka hata nabii Íssa akibariki maji yakawa pombe kwenye arusi ya kanaan. Pombe sio dhambi ila ukizidisha matokeo yake unaongea lugha ya mapicha. Mimi nikipata moja baada ya kazi uwezo wa kufikiria unaongezeka, pombe ni rafiki yangu wa siku nyingi nilikulia kwenye pipa la mbege
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom