Lema: Tutakwenda Mtwara kuwasha Moto!

Lema: Tutakwenda Mtwara kuwasha Moto!

babalao 2

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
5,425
Reaction score
3,300
MBUNGE wa Arusha Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Godbless Lema amesema kuwa Chama hicho kitakwenda kuwasha moto katika Mkoa wa Mtwara ili kuhakikisha gesi haitoki mkoani humo.

Katika hatua nyingine Lema alidai kuwa alivuliwa Ubunge kwa ajili ya kukataa dili la Rais Jakaya Kikwete la kumtaka kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mkutano huo ulihudhuriwa na watu wachache kutokana na kuzuiwa na Jeshi la Polisi huku wananchi waliofika kumsikiliza wakiwa wamekaa mbali na uwanja wakihofia huenda askari Polisi wangefika uwanjani hapo.

Watu walianza kusogea katikati ya uwanja baada ya Lema kuwasili uwanjani hapo ambapo wengi waliohudhuria mkutano huo walikuwa ni vijana.

Akihutubia katika mkutano huo katika Viwanja vya Barafu, Lema alisema kuwa, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma hana mamlaka ya kuzuia mikutano ya kisiasa kufanyika kipindi cha Bunge.

Alisema kuwa Watanzania wanasema gesi ya Mtwara haitoki na Chadema watahakikisha kuwa wanahamasisha wananchi kuhakikisha gesi haitoki mkoani humo.

Alisema kuwa, sasa amerudi tena bungeni mpaka Mungu atakapopenda na si binadamu.

Alisema kuwa hata Rais Jakaya Kikwete akiendelea kuzimua watahakikisha kuwa wanamtoa madarakani kabla ya mwaka 2015. Alisema kuwa sasa wataanza kuiamsha Dodoma na watahakikisha katika kipindi cha Bunge wanatembelea karibu kata zote za Mkoa wa Dodoma.

"Nitaanza kuamsha Dodoma kwenye matawi niliyofungua ikiwemo Chuo Kikuu cha Dodoma, Chuo cha Mipango na Chuo cha Madini na kila moja ana wajibu wa kutafuta ukombozi wake" alisema.


Hii ni kwa mujibu wa HabariLeo

Kwa nini bado polisi wanawatisha wakazi wananchi kusikiliza mikutano ya vyama vya upinzani? Na pia hao wakuu wa mikoa na wilaya wanadharaulika na jamii kila kukicha kutokana na maamuzi yao yasiyo na mbele wala nyuma kwa jamii tunaomba muelewe mnaongoza wananchi wa vyama vingi sio ccm pekee.

Kuhusu gesi naomba chadema hilo suala muwaelimishe tu wananchi na sio kwenda kuchochea vurugu tumieni busara ya hali ya juu tena kusubiri kwanza kama muafaka utashindikana ndipo mjitokeze.
 
hata wananchi wa kigoma wanatakiwa wadai mji unaotakiwa kujengwa kigamboni ukajengwe kigoma maana kikwete aliwaambia wananchi wa kigoma kwamba,kigoma itakuwa dubai, huko nako moto uwashwe
 
Wewe unaishi DAR. Ungekuwa Mtwara, 100% ww ni miongoni ya wanaopinga dhuluma. "Wana Mtwara Gas kwanza uhai baadae". Kuwa mwana Mtwara pingana na dhuluma, uhai sio kitu, ukiwa kama serikali utadhalilika, sababu unaemdhurumu kila kunapokucha anakuwa na kitu kipya na kizuri zaidi ya jana. Tuache dhuluma kaka tutaumbuka.
 
CHADEMA ishuke Mtwara na Lindi kuwajulisha wananchi kwamba ni Kinana wa CCM ndiye aliyeamua akiwa kwenye bodi kule ARTUMAS kuwapokonya gesi kupeleka mkoani kwao na swahiba wake ambaye anamshikilia ulaji pale. M4C itangaze sera ya majimbo na faida zake kwa walalahoi nchini.
 
hapa pinda atalia maana ametoka kuwa omba msamaha wana mtwara sasa lema akienda si atawatibua upya na sekeseke litaanza upya..
 
Hana mshipa wa aibu, alichelewa wp kwenda kuchochea wakati ule moto ulipokuwa mkubwa ikawa kila mtu anatoa tamko,wanasiasa wana tabu sana.sidhan kama lema amewahi kuipenda amani ya tanzania.akanze kuwashawishi arusha tanzanite isitoke mererani, m$*#@ sana
 
Chadema waache kudandia hoja za wananchi.Na waache tabia ya kutafuta sehemu yenye kamgogoro halafu wao wanaenda kwa hoja ya kwamba eti wanaenda kuwasha moto.Kitendo cha wao kudai eti wanaenda kuwashamoto Mtwara katika kipindi hiki ambapo serikali iko katika hatua ya kutafuta maridhiano na wana Mtwara kwa njia za kidiplomasia; Kwa lugha nyengine ni kwamba CHADEMA wanataka kwenda kufanya uchochezi na kuhakikisha wanavuruga harakati za maridhiano na hivyo kufanya maridhiano kuwa magumu kwa maslahi kidogo tu yakupata umaarufu wa kisiasa.Nawasihi CHADEMA watangulize maslahi ya taifa mbele kuliko kujitafutia umaarufu rahisi kwa kusababisha na kuchochea migogoro na mifarakano.
 
MBUNGE wa Arusha Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Godbless Lema amesema kuwa Chama hicho kitakwenda kuwasha moto katika Mkoa wa Mtwara ili kuhakikisha gesi haitoki mkoani humo.
Yule bibi anatishia kugeuza gesi maji na CHADEMA wao wanatishia kuchoma gesi tukose wote!! Gesi na moto haviendani wakulu...

:becky::becky::becky:
 
kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika Zito kabwe yuko jimboni mwake wakati wabunge wenzake wakiwa dodoma,na kuna taarifa kuwa anajiandaa kwa maamuzi magumu,ambayo yanahusishwa na mkutano wa cdm uliyomalizika juzi diamond jubilee
 
hapa pinda atalia maana ametoka kuwa omba msamaha wana mtwara sasa lema akienda si atawatibua upya na sekeseke litaanza upya..
jana niliwaamia paka Jimmy Liverpool na Arushaone kuwa Lema anatikisa nchi haitawaliki wanabisha, wanasema kuna mtu kaniibia password, loh!
ni mbunge yupi katika historia alishawahi kuitaja ikulu wazi wazi kuwa inahusika na hukumu yake ya kuvuliwa ubunge na ikulu kwa hofu baada ya rufaa akarudishiwa ubunge wake? au ni mbunge yupi ameshawahi kuitetemesha nchi hadi mitambo ya bunge ikazimwa?
aliyesema che guavala amekufa ni muongo.
 
Last edited by a moderator:
Amechelewa jamvini karamu imeshaliwa!
 
kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika Zito kabwe yuko jimboni mwake wakati wabunge wenzake wakiwa dodoma,na kuna taarifa kuwa anajiandaa kwa maamuzi magumu,ambayo yanahusishwa na mkutano wa cdm uliyomalizika juzi diamond jubilee

Wewe kweli ni Chura tena mkubwa tofauti nawale wa kihansi,kwanza unatakiwa uludi shule ili ujue mengi kama taratibu za bunge,na ujue kuandika majina yawatu angalau.Haitwi zito,ni Zitto.Nyie ambao uelewa wenu uko makalioni ndio mitaji ya Ccm
 
Chadema waache kudandia hoja za wananchi.Na waache tabia ya kutafuta sehemu yenye kamgogoro halafu wao wanaenda kwa hoja ya kwamba eti wanaenda kuwasha moto.Kitendo cha wao kudai eti wanaenda kuwashamoto Mtwara katika kipindi hiki ambapo serikali iko katika hatua ya kutafuta maridhiano na wana Mtwara kwa njia za kidiplomasia; Kwa lugha nyengine ni kwamba CHADEMA wanataka kwenda kufanya uchochezi na kuhakikisha wanavuruga harakati za maridhiano na hivyo kufanya maridhiano kuwa magumu kwa maslahi kidogo tu yakupata umaarufu wa kisiasa.Nawasihi CHADEMA watangulize maslahi ya taifa mbele kuliko kujitafutia umaarufu rahisi kwa kusababisha na kuchochea migogoro na mifarakano.
Wewe ni mbulula, serkali hii haina kiwango cha kupewa naafasi ya maridhiano. Maslahi ya taifa yapi unazungumzia chini ya chama kilichojaa ufisadi..! Moto utawashwa kama kawaida, hakuna gesi kutoka Mtwara..! Acha nikupasulie yai, mradi huu wa gesi ni deal la kupata hela za uchaguzi 2015..!
 
Wewe ni mbulula, serkali hii haina kiwango cha kupewa naafasi ya maridhiano. Maslahi ya taifa yapi unazungumzia chini ya chama kilichojaa ufisadi..! Moto utawashwa kama kawaida, hakuna gesi kutoka Mtwara..! Acha nikupasulie yai, mradi huu wa gesi ni deal la kupata hela za uchaguzi 2015..!
kwa hiyo hata wana mtwara wakijadiliana na serikali (jalia) wanamtwara wamekubali kwa hiyari yao kwamba gesi iende dar, ninyi (CHADEMA) Mtahakikisha mnatatoka Arusha hadi mtwara kuhakikisha mnavuruga maridhiano hayo? (sisemi gesi ni lazma iende dar lakn).
 
Hana mshipa wa aibu, alichelewa wp kwenda kuchochea wakati ule moto ulipokuwa mkubwa ikawa kila mtu anatoa tamko,wanasiasa wana tabu sana.sidhan kama lema amewahi kuipenda amani ya tanzania.akanze kuwashawishi arusha tanzanite isitoke mererani, m$*#@ sana

Hapo kwenye rangi nyekundi,kama tusi na wewe *1000000:der:
 
kwa hiyo hata wana mtwara wakijadiliana na serikali (jalia) wanamtwara wamekubali kwa hiyari yao kwamba gesi iende dar, ninyi (CHADEMA) Mtahakikisha mnatatoka Arusha hadi mtwara kuhakikisha mnavuruga maridhiano hayo? (sisemi gesi ni lazma iende dar lakn).

A na B ni sawa.
 
kwa hiyo hata wana mtwara wakijadiliana na serikali (jalia) wanamtwara wamekubali kwa hiyari yao kwamba gesi iende dar, ninyi (CHADEMA) Mtahakikisha mnatatoka Arusha hadi mtwara kuhakikisha mnavuruga maridhiano hayo? (sisemi gesi ni lazma iende dar lakn).

Huu nao ni miongoni mwa ile mitambo ya kupika majungu aliosema Kinana?
 
MBUNGE wa Arusha Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Godbless Lema amesema kuwa Chama hicho kitakwenda kuwasha moto katika Mkoa wa Mtwara ili kuhakikisha gesi haitoki mkoani humo.

Katika hatua nyingine Lema alidai kuwa alivuliwa Ubunge kwa ajili ya kukataa dili la Rais Jakaya Kikwete la kumtaka kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mkutano huo ulihudhuriwa na watu wachache kutokana na kuzuiwa na Jeshi la Polisi huku wananchi waliofika kumsikiliza wakiwa wamekaa mbali na uwanja wakihofia huenda askari Polisi wangefika uwanjani hapo.

Watu walianza kusogea katikati ya uwanja baada ya Lema kuwasili uwanjani hapo ambapo wengi waliohudhuria mkutano huo walikuwa ni vijana.

Akihutubia katika mkutano huo katika Viwanja vya Barafu, Lema alisema kuwa, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma hana mamlaka ya kuzuia mikutano ya kisiasa kufanyika kipindi cha Bunge.

Alisema kuwa Watanzania wanasema gesi ya Mtwara haitoki na Chadema watahakikisha kuwa wanahamasisha wananchi kuhakikisha gesi haitoki mkoani humo.

Alisema kuwa, sasa amerudi tena bungeni mpaka Mungu atakapopenda na si binadamu.

Alisema kuwa hata Rais Jakaya Kikwete akiendelea kuzimua watahakikisha kuwa wanamtoa madarakani kabla ya mwaka 2015. Alisema kuwa sasa wataanza kuiamsha Dodoma na watahakikisha katika kipindi cha Bunge wanatembelea karibu kata zote za Mkoa wa Dodoma.

"Nitaanza kuamsha Dodoma kwenye matawi niliyofungua ikiwemo Chuo Kikuu cha Dodoma, Chuo cha Mipango na Chuo cha Madini na kila moja ana wajibu wa kutafuta ukombozi wake" alisema.


Hii ni kwa mujibu wa HabariLeo

Kwa nini bado polisi wanawatisha wakazi wananchi kusikiliza mikutano ya vyama vya upinzani? Na pia hao wakuu wa mikoa na wilaya wanadharaulika na jamii kila kukicha kutokana na maamuzi yao yasiyo na mbele wala nyuma kwa jamii tunaomba muelewe mnaongoza wananchi wa vyama vingi sio ccm pekee.

Kuhusu gesi naomba chadema hilo suala muwaelimishe tu wananchi na sio kwenda kuchochea vurugu tumieni busara ya hali ya juu tena kusubiri kwanza kama muafaka utashindikana ndipo mjitokeze.

Eeeh huyu mchagga kilaza anasema atahakikisha gesi haitoki mtwara! hii kaitoa wapi mbona mawazo yake yako tofauti na ya wana mtwara! mpelekeni elimu ya watu wazima huyu mchagga aache kuropoka na kudandia mambo asiyoyajua au albda anazungungumzia gesi ya wana arusha kama wanayo
 
kwa hiyo hata wana mtwara wakijadiliana na serikali (jalia) wanamtwara wamekubali kwa hiyari yao kwamba gesi iende dar, ninyi (CHADEMA) Mtahakikisha mnatatoka Arusha hadi mtwara kuhakikisha mnavuruga maridhiano hayo? (sisemi gesi ni lazma iende dar lakn).
Shida yetu si kuvuruga maridhiano, ni kuufahamisha uma jua ya haki zao, kukabiliana na deal za kifisadi. Ikiwa kutakuwa na mutual benefit we have no problem..! Wanamtwara wamenyanyasika vya kutosha (hata barabara ya lami hawana) itakuwa ni uendawazimu gesi yao iondoke hivi hivi bila kuwanufaisha. Ndo maana wote wamekula kiapo gesi kwanza uhai baadaye
 
Back
Top Bottom