Lema na Sugu kesho nendeni bungeni

Lema na Sugu kesho nendeni bungeni

zimebaki siku ngapi bunge kuvunjwa rasmi wewe bibi?
Umemuuliza swali zuri sana, yeye kasahau kuwa Mwenyekiti wake wa Chama JK amepangiwa Jumatano ijayo ambayo ni tarehe 8 akalivunje bunge.

Kwa hiyo imebaki kama siku moja na nusu ya mijadala ya bunge kabla halijvunjwa rasmi.

Kwa hiyo hayo masaa machache sana yaliyobaki ya uhai wa bunge, nawaaminia makamanda wetu akina Mbowe,Lema,Sugu,Wenje, Kafulila,Nassari, Halima Mdee na wengineo wa Ukawa watakomaa kisawaswa kuhakikikisha hawa maccm hawatufungi wananchi goli la mkono kwenye miswada hiyo ya gesi na mafuta.
 
Watanzania ndio akili zetu zilipoishia hapo.. Kwahiyo wote wakifukuzwa then miswada maCCM wakiipitisha itakuaje?? Tunawaona wabunge wetu wakipambana kule ndani, vipi sie huku nje mbona hatuonyeshi kujali??

Yaani miTanzania tunashindwa hata kujikusanya Jumatatu tutie timu wizara ya Nishati au Ikulu sie tumekalia majungu kwenye mitandao.. No wonder CCM ikishinda kwa kishindo tena uchaguzi mkuu huu. Sijui tumelaaniwa na nani sisi..
 
Wapo dodoma tayari kamanda ngoma ndio kwanza mbiiiichiiii jumatatu tunaanza moja mpaka wafukuze ukawa wote

mkuu leo jumamosi kuna bunge. wahakikishe wanaendeleza pale walipoishia wenzao... nje ya hapo ni usaliti. hatuna imani na wabunge wa ccm kamwe katika kulinda raslimali zetu...
 
J3 wapinzani waendelee kuzuia huo muswaada .Pamoja na Kinana kuwalipua wabunge wa ccm kwamba wana pitishapitisha tu sheria zinazoumiza wananchi bado yanaendelea kukubali

mkuu usimuamini mwanaccm yeyote dini yao ni ufisadi na kulindana.
 
kama nyerere alitutunzia raslimali hizo kwa muda wote huu..tunashindwa nini kuwa na subira? tegemeo letu kwa sasa ni ukawa pale bungeni. nje ya ukawa hatuna imani pale bungeni. wabunge wa ccm wamegeuka kuwa madalali wa wezi wa rasilimali zetu....kina mbowe hakikisheni hamrudi nyuma..
 
Sehemu-ya-wabunge-wa-upinzani-620x308.jpg

Baadhi ya wabunge wa UKAWA waliotimuliwa bungeni, walipokuwa kwenye mvutano na askari wa bunge

[h=1]Wabunge 10 UKAWA watimuliwa Bungeni[/h]Posted by: Dany Tibason 9 hours ago 562 Views


WABUNGE 10 wa Kambi Rasmi ya Upinzani wanaounda Umoja wa Katiba ya wananchi (UKAWA), wametimuliwa Bungeni kile kilichoelezwa utomvu wa nidhamu na kudharau kiti cha Spika. Anaandika Dany Tibason … (endelea).
Wabunge hao wametimuliwa baada ya kutiwa hatihani na Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge inayoongozwa na Brigedia Jenerali Mstaafu Hassan Ngwilizi kwa madai ya kukiuka kanuni za Bunge kwa kudharau amri halali ya Spika wa Bunge Anna Makinda.
Kwa mujibu wa Ngwilizi aliyesoma hukumu hiyo Bungeni, wabunge wanne wamepata adhabu ya kutohudhuria vikao vyote vilivyosalia katika mkutano huu wa 20, wawili vikao vikao viwili na wengine watapata hukumu yao leo baada ya kusikilizwa na Kamati hiyo.
Amesema waliofungiwa vikao vyote vilivyosalia na kutopata fursa ya kumshuhudia Rais Jakaya Kikwete akivunja Bunge Julai tisa mwaka huu, waligoma kutoa utetezi wao, wakitaka wapate fursa ya kuja na mawakili wao kujitetea.
Brigedia Ngwilizi aliwataja waliofungiwa vikao vyote vya mkutano huu wa 20 ni John Mnyika (Ubungo), Paulin Gekul, (Viti Maalum), Tundu Lissu (Singida Mashariki) Felix Mkosamali (Muhambwe) na Moses Machali (Kasulu Mjini).
Waliofungiwa kuhudhuria vikao viwili ni Peter Msingwa (Iringa Mjini), Mbarouk Mohamed Mbarouk (Ole). Mwenyekiti huyo aliwataja watakapata adhabu baada ya kuhojiwa leo ni pamoja na Joseph Selasini (Rombo), Khalifa Suleman Khalifa (Gando), Rashid Ali Abdallal (Tumbi)

Akichangia hoja ya kuwafungia wabunge hao, Mbunge wa Karatu, Mchungaji Israel Natse ambaye ni mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Maadili, amesema walikubaliana kuwaruhusu watuhumiwa waje na mawakili wao kama walivyoomba, lakini ameshangazwa na hukumu iliyosomwa na Ngwilizi amesema wabunge hao hawakujitetea, hivyo hawakutendewa haki.

Mbunge wa Chake chake, Mussa Haji Kombo alihoji kwanini Kamati hiyo imeamua kutoa adhabu jana wakati bado kuna watuhumiwa wanaopaswa kuhojiwa leo.
Akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge, Lissu amesema watu wenye hatia siku zote ni waoga na Bunge hili ni la watu waoga.
Amesema wabunge walioitwa kwenye Kamati hawakujitetea kwani waliomba kuja na mawikili wao na ndio utaratibu na kanuni za Bunge.
"Kwenye Kamati wote tulitaka tuje na mawakili wetu, ndani ya Bunge hatukupata fursa ya kujitetea. Mnakumbuka hivi karibuni Mbunge wetu, Joseph Mbilinyi, alipelekwa kwenye Kamati hii, akaomba kwenda na wakili wake. Leo sisi tumepata adhabu hiyo bila kujitetea." Amesema Lissu.
Lissu alirejea hoja ya aliyekuwa Mbunge wa Chadema, Zitto Kabwe kwamba mwaka 2007 alihukumiwa na Kamati hiyo, alipata muda wa kujitetea kwenye Kamati na ndani ya Bunge, hivyo alishangazwa na adhabu waliyopata.
Mbunge huyo amesema wamepata adhabu hiyo ili kuwapisha wabunge wa CCM kupitisha miswada ya kuliibia gesi taifa, dhambi ambayo amesema wao hawako tayari kushiriki.
Akizungumzia kilichotokea asubuhi, Lissu amesema wote waliosimama asubuhi wakati Waziri wa Nishati na Madini akilazimisha kusoma miswada hiyo, walitaka kuomba mwongozo, utaratibu na kutoa taarifa, lakini Spika Makinda alikataa na ndio chanzo cha vurugu.
Juzi Spika aliahirisha kikao cha 41 cha Bunge, baada ya wabunge wa kambi rasmi ya upinzani inayoundwa na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kupinga Serikali kuleta miswada mitatu nyeti kwa hati ya dharula kwa madai kuwa wabunge hawajaisoma na wadau hawajapata muda zaidi wa kuijadili.
Miswada hiyo ambayo ni mwiba mchungu Bungeni ni pamoja na muswada wa Sheria ya Petroli, Muswada wa Usimamizi wa Mapato ya Mafuta na Gesi wa mwaka 2015 na Muswada wa Sheria ya Uwazi na Uwajibikaji katika taasisi za uchimbaji Tanzania wa mwaka 2015.
 
Jana nimemsikia mnyika anasema kuna vifungu katika sheria hizo havibadiliki yaani ina maana wakiamua leo ccm wanazifunga mpaka serikali zijazo yale yale ya kwenye madini
 
mil.230 na ujinga ujinga mwingine hakuna tofauti na si msaada kwangu.zaidi ya kama kitendo cha kusukutua kinywa....ili utoe uchafu mdoni upate radha ya kiingiacho kinywani.
 
wabunge wa ukawa waliobaki waliendeleze. kinyume na hapo niusaliti mkubwa hatukuwatuma bungeni kwenda kuisemea serikali bali kuwasemea wananchi nakuwatetea. walichofanyiwa wabunge wa ukawa ni jambo la kawaida katika uwakilishi.
 
Tena ilitakiwa wajipange, jana Mnyika hakutakiwa kusimama ili hata wakitimuliwa akina Lissu abaki kichwa mwingine wa miongozo. Hata waliobaki bado wanaweza kuitumia mbinu hii, wajigawe makundi matatu, kila kundi liwe na mbunge mmoja mahiri wa miongozo, kama leo wanatimuliwa hawa kesho wanaibuka wengine, katu wasikubali ku-rise wote kwa pamoja. Watumie hii strategy aisee.
 
Kamanda nasari kesho mjengoni akishirikiana na sugu lema na halima mdee
 
Kamanda nasari kesho mjengoni akishirikiana na sugu lema na halima mdee

kidogo halima wengine hawana cha kufanya zaidi ya kuzome,mnazalilisha maana ya kamanda kwa hawa jamaa
 
kinana ni mnafiki sanaaaaaaa, anaponda wabunge wa ccm wakat ser z\ kipuuzi anazotetea yeye ndio master mind
 
Leo makamanda wa ukweli katika Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wamefukuzwa Bungeni.

Kwa hiyo nawasihi makamanda wengine kama Lema na Sugu, kesho waende bungeni wakaongeze nguvu iliyopungua.

Sisi wananchi tuliyo wengi tunaamini Lema, Sugu wakienda bungeni wakishirikiana na makamanda wengine kama vile Wenje, Halima Mdee, Moses Machali, James Mbatia na kamanda mkuu wa kikosi chote cha UKAWA Freman Mbowe akikisheni hi sera ya gesi na mafuta haipitishi Bungeni kwa manufaa ya nchi.
Makamanda kwa faida
 
unachekesha kweli wewe. yaani lema na sugu wakaongeze nguvu bungeni? yakupigana au? maana kama ni kujenga hoja wale ni full zero brain.

Leo makamanda wa ukweli katika Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wamefukuzwa Bungeni.

Kwa hiyo nawasihi makamanda wengine kama Lema na Sugu, kesho waende bungeni wakaongeze nguvu iliyopungua.

Sisi wananchi tuliyo wengi tunaamini Lema, Sugu wakienda bungeni wakishirikiana na makamanda wengine kama vile Wenje, Halima Mdee, Moses Machali, James Mbatia na kamanda mkuu wa kikosi chote cha UKAWA Freman Mbowe akikisheni hi sera ya gesi na mafuta haipitishi Bungeni kwa manufaa ya nchi.
 
Back
Top Bottom