Lema na Sugu kesho nendeni bungeni

Lema na Sugu kesho nendeni bungeni

lendila

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2012
Posts
5,805
Reaction score
4,374
Leo makamanda wa ukweli katika Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wamefukuzwa Bungeni.

Kwa hiyo nawasihi makamanda wengine kama Lema na Sugu, kesho waende bungeni wakaongeze nguvu iliyopungua.

Sisi wananchi tuliyo wengi tunaamini Lema, Sugu wakienda bungeni wakishirikiana na makamanda wengine kama vile Wenje, Halima Mdee, Moses Machali, James Mbatia na kamanda mkuu wa kikosi chote cha UKAWA Freman Mbowe akikisheni hi sera ya gesi na mafuta haipitishi Bungeni kwa manufaa ya nchi.
 
J3 wapinzani waendelee kuzuia huo muswaada .Pamoja na Kinana kuwalipua wabunge wa ccm kwamba wana pitishapitisha tu sheria zinazoumiza wananchi bado yanaendelea kukubali
 
Wapo dodoma tayari kamanda ngoma ndio kwanza mbiiiichiiii jumatatu tunaanza moja mpaka wafukuze ukawa wote

Jumatatu kama haya majembe yatakuwepo dodoma itakuwa imekaa poa sana
 
J3 wapinzani waendelee kuzuia huo muswaada .Pamoja na Kinana kuwalipua wabunge wa ccm kwamba wana pitishapitisha tu sheria zinazoumiza wananchi bado yanaendelea kukubali

Unamuamini Kinana? KINANA ni msanii na mnafiki
 
Mkuu ni kama hujaeleweka,unataka ipitishwe kwa maslahi ya nani Kama ya wanachi hutaki
 
J3 wapinzani waendelee kuzuia huo muswaada .Pamoja na Kinana kuwalipua wabunge wa ccm kwamba wana pitishapitisha tu sheria zinazoumiza wananchi bado yanaendelea kukubali

Mkuu bemg ngoma ni kesho sio j3. Magamba yametengua kanuni so kesho bunge lipo. Wembe ni ule ule kesho.
 
Aisee nimeipenda hiyo ya kwamba Sugu,lema na wenje wapo Dodoma tayari...maskini MaCCM wa nataka kumuharibia bibi makinda CV yake aliyokuwa ameipalilia vizuri... Nina uhakika kutoka moyoni mama hakupenda hii miswaada iletwe ila basi inatakiwa alipe fadhila kwani hayo ndio kati ya masharti aliyopewa wakati anakabidhiwa cheo cha samwel sita. Watanzania tusikubali mafisadi wauze nchi jamani wanatafuta pesa za uchaguzi kutoka MCC WAMEAMBIWA WAKIPITISHA hii miswaada hela zinakuja kutoka MCC kabla ya oktoba
 
Mkuu ni kama hujaeleweka,unataka ipitishwe kwa maslahi ya nani Kama ya wanachi hutaki

Mmhh!! kwa hiki ulichokiandika nahisi AKILI ZAKO UMESHIKIWA NA KIKUNDI FULANI.
 
Mpaka kieleweke, hawa wahuni uhuni wao lazima usimamishwe kwa nguvu zote. Bunge wameligeuza kama makao ya makuu ya kupitisha uhuni wao badala ya kufanyia mambo mbali mbali yenye umuhimu na maslahi kwa Watanzania.

Wapo dodoma tayari kamanda ngoma ndio kwanza mbiiiichiiii jumatatu tunaanza moja mpaka wafukuze ukawa wote
 
pumbavu sana!!!!!!

Raslimali zetu zinatakiwa zitunufaishe wananchi wote hiyo mishwada ya sheria ina uharaka gani ya kudiscussiwa kwa muda hu bora isubiri tu bunge lijalo(baada ya GE)
 
Wapi Mbowe? Timu nzima ya UKAWA inabidi washuke mjengoni kesho kuanzisha varangati la nguvu, ila mjue kesho TBC hawataonyesha kitu kwani hawa wahuni hawatataka tuuone uhuni wao.

Wapi Kafulila aisee
 
Leo makamanda wa ukweli katika Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wamefukuzwa Bungeni.

Kwa hiyo nawasihi makamanda wengine kama Lema na Sugu, kesho waende bungeni wakaongeze nguvu iliyopungua.

Sisi wananchi tuliyo wengi tunaamini Lema, Sugu wakienda bungeni wakishirikiana na makamanda wengine kama vile Wenje, Halima Mdee, Moses Machali, James Mbatia na kamanda mkuu wa kikosi chote cha UKAWA Freman Mbowe akikisheni hi sera ya gesi na mafuta haipitishi Bungeni kwa manufaa ya nchi.

Wembe ni ule ule wakifanya vurugu watasimamishwa kushiriki vikao vyote.
 
Kesho moto wa Lema,Nassary,Wenje,Halima mdee ,Mbowe n.k watakuwepo bungeni hakuna muswada kupitishwa kihuni tena mwambie Obama kimeshanuka bungeni
 
Leo makamanda wa ukweli katika Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wamefukuzwa Bungeni.

Kwa hiyo nawasihi makamanda wengine kama Lema na Sugu, kesho waende bungeni wakaongeze nguvu iliyopungua.

Sisi wananchi tuliyo wengi tunaamini Lema, Sugu wakienda bungeni wakishirikiana na makamanda wengine kama vile Wenje, Halima Mdee, Moses Machali, James Mbatia na kamanda mkuu wa kikosi chote cha UKAWA Freman Mbowe akikisheni hi sera ya gesi na mafuta haipitishi Bungeni kwa manufaa ya nchi.

Toka lini mbowe kawa kamanda mkuu wa Ukawa.
 
pumbavu sana!!!!!!

Raslimali zetu zinatakiwa zitunufaishe wananchi wote hiyo mishwada ya sheria ina uharaka gani ya kudiscussiwa kwa muda hu bora isubiri tu bunge lijalo(baada ya GE)
Hivi haya maSisiemu yanamgeuza hata Mungu kama hakupiga hesabu yake vizuri kuihifadhi gesi yote hiyo kwenye ardhi yetu?

Hivi kwani Mungu kwani hakujua kuwa hata hayo mataifa mengine 'yalitamani' kupewa gesi hiyo lakini Mungu kwa kulipenda Taifa hili la TZ akatupa neema hiyo ya gesi nyingi sana ya 56 trillion cubic feet ambayo ukiiconvent kwenye mafuta unapata kama 10 billion barrels of crude oil.

Ukichukulia pipa moja la mafuta ghafi kwenye World market hata kwa bei ya 50 US dollars, unapata jumla ya thamani ya gesi yetu tuliyojaaliwa na Mwenyezi Mungu aliyotutunzia kwenye ardhi ya nchi hii kuwa yenye thamani ya 500 billion USD.

Kama bajeti yetu ya mwaka huu hii ilikuwa around 10 billion USD, hiyo tafsiri yake ni kuwa kwa source moja pekee ya mapato ya gesi yetu, tunaweza kuendesha bajeti yetu ya nchi kwa miaka 50 ijayo!

Hapo ndipo unapoweza kujua ni kwanini magamba wanaweweseka na kutaka kuikimbiza kwa spidi kali sana kwa hati ya dharula miswada hii ya mafuta na gesi ili rasilimali hizi ziwanufaishe wawekezaji wa nje na wao watawala na sisi wananchi tubaki kuwa watazamaji na hivyo tuwe tumefungwa goli la mkono na hao maccm!
 
Back
Top Bottom